Habari za Punde

Waziri wa habari akutana na balozi mpya wa Malawi nchini

 Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk  akisalimiana na Balozi wa Malawi Nchini Tanzania Hawa O. Ndilowe wakati alipowasili Ofisini kwake kwaajili ya kujitambulisha pia na kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusuUtalii Zanzibar.
 Afisa Ubalozi anaeshughulikia masuala ya Uchumi Tanzania Chinvano Kapeleta akizungumzia masuala ya Uchumi na Utalii na Viongoizi wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar.
 Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akifafanua jambo katika mazungumzo na Balozi wa Malawi Nchini Tanzania Hawa O. Ndilowe wakati walipokutana Ofisini kwake Zanzibar.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk katikati akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Malawi Hawa O.Ndilowe kulia yake na baadhi ya viongozi waliofika Ofisini kwake Zanzibar.

PICHA ZOTE NA MIZA OTHMAN-HABARI MAELEZO ZANZIBAR.


Na Ali Issa Maelezo Zanzibar. 26/5/2015

Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar  Said Ali Mbaruok  amesema ushirikiano katika Nyanja za utalii,utamaduni na michezo ndio njia pekee ya kukuza uhusiano uliopo kati ya Nchi ya Zanzibar na Malawi

Hayo ameyasema huko Wizara ya Habari  Utamaduni ,Utalii na Mchezo wakati alipokutana na Balozi mpya wa Malawi Nchini Tanzania Bi Hawa O.Ndilowe alipofika ofisini hapo kwa kujitambulisha kwa waziri huyo.

Amesema ushirikiano huo utafanya mataifa yao kutembeleana katika Nyanja hizo na kubadilisha mawazo na kuongeza uhusiano wao unaimarika kwa kukutana mara kwa mara.

“Tumekuwa na mashindano ya Kombe la Mapinduzi kila mwaka na nchi mbalimbali ambazo zinashiriki ni vyema Malawi nayo ikashiriki katika kombe hilo na ushirikiano wetu utakuwa zaidi”alisema Waziri Said.


Aidha Waziri huyo amesema kuwa kwa vile Malawi imepiga hatua kimaendeleo katika masuala ya utalii michezo na Utamaduni itakuwa ni faraja kubwa kushirikiana katika njia hizo na kuona Zanzibar nayo inasonga mbele katika nyanja hizo.

Waziri Mbarouk amemshukuru balozi huyo na kumtaka kufanya ziara nyengine ya kuitembelea Zanzibar pamoja na familia yake kwa  kujionea sehemu mbalimbali za vivutio vya kiutalii na kihistoria.

Nae Balozi Ndilowe amemshukuru Waziri kwa mapokezi hayo na kusema kuwa ushirikiano wa Malawi na Zanzibar ni ushirikiano wa muda mrefu,hivyo kushirikiana katika masuala ya utalii, utamadu na michezo ni kukuza uhusiana wao uliopo.

Amesema atazishawishi nchi nyengine pamoja na wageni mbalimbali kuja kutembelea Zanzibar katika Nyanja tofauti kwa lengo la kuleta maendeleo ya nchi na Mataifa yao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.