Habari za Punde

UN Yawaenzi Walinzi Wake wa Amani Waliopoteza Maisha.

Na MwandishiMaalum, New York

Umoja wa Mataifa,  jana   Mei 19 umefanya hafla maalumu ya siku ya Kimataifa ya Walinzi wa Amani  wanaohudumu katika Misheni mbalimbali za Kulinda Amani chini ya kofia ya Umoja wa Mataifa.

Katika hafla hiyo jumla ya walinzi 129 wanajeshi na polisi waliopoteza maisha mwaka jana kwa kushambuliwa na makundi ya wapiganaji wenye silaha, matukio ya kigaidi, ajali na kuumwa walikumbukwa na kuenziwa kwa mchango wao.

Miongoni mwa Mashujaa hao  129 kutoka nchi  50, wapo mashujaa watatu kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mashujaa hao ni Sgt. Musa Abdrahamani Yusuf, Cpl. John Leornad Mkudena Pte.Juma Ally Khamis.
 
Hafla hiyo maalum ya kutambua mchango wa walinzi hao wa Amani na ambao wamejitolea maisha yao kwa ajili ya kuwalinda na kuokoa maisha ya wananchi wasio kuwa na hatia katika nchi zinazokabiliwa na vita na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe iliongozwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban Ki  Moon.

Mwakilishi wa Kudumu wa  Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi, ndiye aliyepokea medali maalum za mashuja hao watatu kwa niaba ya familia zao.


Medali waliyotunukiwa mashujaa hao na wengine inatambuliwa kama medali ya  Dag Hammarskjold.

Hafla ya mwaka huu,   pamoja na kutambua mchango wa mashujaa hao 129 ,  pia  ilitambua kwa namna yapekee na kwa mara ya kwanza, mchango na kujitolea wa hali ya juu ulikofanywa na Kapteni Mbaye Diagneraiaya  Senegal,aliyepoteza maisha mwaka 1994 wakati akiokoa maisha ya wanyarwada wakati wa mauaji ya kimbali.

Kapteni Mbaye Diagne ameeziwa rasmi katika maadhimisho ya mwaka huu kwa kupewa medali maalum iliyopewa jina la  Medali ya Mbaye Diagne, medali ambayo alikabidhiwa mjane wa Mbaye Bibi Yacine Mar Diophuku akishuhudiwa na watoto wake wawili.

Kapten Mbaye Diagne alikuwa mwangalizi wa Amani nchini Rwanda, kwa ushujaa mkubwa na bila ya kujali hatariiliyokuwaikimkabilialitumialorikuwafichanakuwapelekamahalisalamamamiayawanyarwadawakatiwamauajiyakimbaliya Rwanda.
Kwa kutambuaushujaanauthubutu wake huo, Baraza la Usalamalilibunimwaka 2014 medaliyaKaptenMbayeDiagneambayowatakuwawanatunukiwawanajeshi,  polisinaraiaambaowameonyeshauthubutunaushupavuwahaliyajuukiasi cha kupotezamaishayaowakatiwakitekelezamajukumuyao.
Akizungumzawakatiwahalfahiyoambayoilibebamajonziyaainayake,  KatibuMkuuwaUmojawaMataifa, Ban Ki Moon,  alielezakwamba,  hadikufikiamweziwannemwakahuu, jumlayawalinziwa Amani  3,400 wakiwamowanajeshi, polisinaraiawalikuwawamepotezamaishatangukuanzishwawashughulizaulinziwa Amani kwakofiayaUmojawaMataifamiaka 70 iliyopita.
“Wakatileotunawaenzinakuwakumbukamashujaahawa 129 kutokamataifa 50 waliopotezamaishayaomwakajanawakatiwakitekelezajukumu la kuwalindawananchiwengine,  jana ( Mei 18) walinziwenginewatanowanaohudumuhuko  Mali  wamepotezamaishabaadayakushambuliwa”. AkasemaBan  Ki Moon kwahuzuni.



Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa  Balozi Tuvako Manongi akiwa ameshika medali  ya  Dag Hammarskjold waliyotunukiwa  mashujaa watatu watanzania ambao wamepoteza maisha mwaka jana wakati wakihudumu katika Misheni za kulinda Amani  za Umoja wa Mataifa. kushoto kwa Balozi ni Luteni Kanal  George Ita'ngare, mshauri wa  masuala ya kijeshi  katika Uwakilishi wa Kudumu na  kulia ni  Bw,Herve Ladsous,  Katibu Mkuu Msaidizi Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya  Operesheni za Ulinsi wa Amani  za Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Ban Ki Moon, akimvisha Bibi Yacine Mar Diop medal maalum ya   Kapteni Mbaye Diagne ambaye alikuwa ni  mume wa Bibi Yacine, Kapteni Diagne aliuawa mwaka 1994 wakati wa mauaji ya kimbali ya Rwanda. medali hiyo  maalum imebuniwa na  Baraza  la Usalama kwa kutambua ushujaa na uthubutu wake na kujituma kwake kwa hali ya juu hadi  kupelekea kupoteza maisha.  Kapteni  Diagne anakumbukwa  kwa namna alivyookoa maisha ya mamia ya wanyarwanda kwa kuwaficha kwenye lori na kuwapeleka  mahali salama kabla ya  yenye mwenyewe kuuawa
Balozi Tuvako Manongi  akiandika katika kitabu cha  kuwaeni walinzi wa amani wa  Umoja wa Mataifa waliopotea maisha mwaka jana. miongoni mwa mashujaa 129 waliokumbukwa  wapo watanzania watatu ambao ni Sgt. Musa Abdrahamani Yusuf, Cpl John Leornad Mkude na Pte. Juma Ally Khamis 
Sehemu ya  washiriki wa hafla ya siku ya Kimataifa ya Walinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa hafla hiyo ilifanyika  jana Mei 19

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.