Habari za Punde

Dk Mahadhi amtembelea Balozi wa Malawi nchini Kuwait


Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili Ubalozi wa Malawi na kupokelewa na mwenyeji wake, Mhe. Balozi Wilfred Ali (hayupo pichani). Dkt. Maalim alimtembelea Balozi huyo wa Malawi kwa lengo la kumshukuru kutokana na mchango mkubwa wa Ubalozi huo katika kufanikisha ufunguzi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Kuwait. Hata hivyo, Balozi Maalim, alimuhakikishia Balozi Ali utayari wa Tanzania kuendelea kushirikiana na Malawi na jamii nzima ya kidiplomasia nchini Kuwait.

Balozi Dkt. Mahadhi pamoja na mwenyeji wake Mhe. Ali wakiendelea na mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.