Habari za Punde

TRA Zanzibar yawakumbusha Walipa kodi ya mapato mwisho kulipia ni tarehe 30 Septemba 2016




TANGAZO 

TRA ZANZIBAR INAWAKUMBUSHA WAFANYABIASHARA WOTE WA UNGUJA NA PEMBA, KWAMBA TAREHE YA MWISHO YA KULIPIA AWAMU YA TATU YA KODI YA MAPATO YAANI INCOME TAX NI TAREHE 30 SEPTEMBA 2016.

 MALIPO YA KODI YATAKAYOLIPWA BAADA YA TAREHE 30 SEPTEMBA 2016 YATALIPWA PAMOJA NA ADHABU YA KUCHELEWESHA MALIPO.

 AIDHA WAFANYABIASHARA WANAKUMBUSHWA KWAMBA, TAREHE YA MWISHO YA KUWASILISHA RITANI ZA MWISHO ZA KODI YA MAPATO (INCOME TAX) KWA MWAKA WA MAPATO UNAOISHIA TAREHE 31 MACHI 2016 NI TAREHE 30 SEPTEMBA 2016. 

TUNAWAOMBA WAFANYABIASHARA WOTE WAZINGATIE MUDA WA KULIPA KODI NA KUWASILISHA RITANI ZA MWAKA, ILI KUEPUKA KULIPIA KODI ITAKAYOAMBATANA NA ADHABU. 

KWA UFAFANUZI ZAIDI UNAWEZA KUFIKA KATIKA OFISI ZA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA) ZILIZOPO MAYUGWANI KWA UNGUJA NA KILIMATINDE CHAKECHAKE KWA PEMBA, 

‘‘PAMOJA TUNAJENGA TAIFA LETU’’

 Imetolewa na: 
Kitengo cha Elimu na Huduma kwa Mlipakodi 
Mamlaka ya Mapato Tanzania-Zanzibar 
Simu nambari 0242232923 
S. L. B. 161 ZANZIBAR
 Barua pepe: trazanzibar@tra.go.tz 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.