Habari za Punde

Hazina SACCOS Kujenga Kitega Uchumi “NJEDENGWA” Dodoma.


Kamishina wa Sera kutoka Wizara ya Fedha, Mipango na Uchumi Bw. Augustine K. Ollal akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Wawakilishi wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina Saccos) leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chama hicho Bw. Eligius A. Mwankenja.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina Saccos) wakifuatilia Mkutano Mkuu wa Tatu wa Chama hicho kilichofanyika leo katika ukumbi wa Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina Saccos) Bw. Eligius A. Mwankenja (wa kwanza kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Hazina Saccos leo jijini Dar es Salaam. Watatu kutoka kushoto mstari wa mbele ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bw.  Eligius A. Mwankenja.(Picha na: Maelezo)

Na: Frank Shija – Maelezo.
CHAMA cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina Saccos kimepanga kujenga kitega uchumi cha kisasa kupitia mradi wa njedengwa katika Mkoa wa Dodoma ili kuendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhamishia makao makuu ya shughuli  za Serikali mjini humo.

Hayo yamebainishwa  na leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Eligius Mwankenja wakati wa mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama hicho, na kuongeza kuwa mradi huo katika hatua ya utafiti wa kiuchumi na fedha.

Mwankenja amesema kuwa wapo katika hatua za awali za kuanza utekelezaji wa mradi huo ambao zabuni yake inatarajiwa kutangazwa mwezi wa Aprili 2017.

“Mradi wa Njedengwa upo mbioni kuanza tunategemea utakuwa chachu ya maendeleo ya Chama chetu kwa kutuingizia kipato kutokana na shuguli zitakazokuwa zikifanyika kupitia mradi huo”. Alisema Mwankenja.

Aliongeza kuwa kupitia mradi huo wanatarajia kujenga hoteli ya kisasa, kumbi za kufanyia mikutano, majengo la Ofisi, , Viwanja vya Michezo na bwawa maalum la kuogelea.

Mpaka sasa tayari upembuzi yakinifu wa hali ya eneo hilo imekwishafanyika ambapo mradi huo utajengwa kwa ubia baina ya mwekezaji kupitia utaratibu wa Jenga, Endesha na Hamisha (Build, Operate and Transfer - BOT) ambapo mwekezaji atagharamia ujenzi wote na kuendesha kwa muda ambao utakualiwa ndani ya mkataba.

Palimo na mafanikio hakukosi kuwa na chamagamoto, Mwenyekiti wa Bodi ya Hazina Saccos anasema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo kwa sasa ni ufinyi wa ofisi ukizingatia kwamba idadi ya wananchama imeendelea kuongezeka toka wanachama 100 mwaka 1972 wakati Hazina Saccos ilipoanzishwa hadi kufikia zaidi ya 5000 mwaka huu.

Changamoto hii inasababisha pia kuongezeka kwa mahitaji ya wanachama wanaohitaji kupatiwa mikopo, hivyo inakilazimu chama kubuni njia mbada za kukuza na kuongeza mtaji ili kukabiliana na hali hiyo.


Mradi wa Njedengwa ni mradi wa uwekezaji wa Hazina Saccos katika kuhakikisha wanawekaza ili kukuza mtaji wa Chama chao kwa lengo la kuhakikisha kinawahudumia wanachama wake wote i kulingana na mahitaji yao kwa wakati.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.