Habari za Punde

            TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kampuni ya Rafiki Network inawaarifu kwamba itafanya Tamasha la Michezo na Utamaduni linalojulikana kama“ Pemba Weekend Bonanza” litakalofanyika kisiwani Pemba kuanzia tarehe 28  hadi 30 Julai mwaka 2017.

Tamasha hilo litajumuisha matukio mbali mbali kama vile mchezo wa ng’ombe, resi za baiskeli, mashindano ya kuogelea na resi za ngalawa.

Mchezo wa ng’ombe utafanyika siku ya Ijumaa tarehe 28 Julai, 2017, majira ya lasiri katika viwanja vya skuli ya Chwale, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Aidha, resi za baiskeli ambazo zitafanyika kwa mizunguko mwili tafauti zitakuwa siku ya Jumamosi tarehe 29 na Jumapili tarehe 30 Julai katika maeneo na utaratibu ufuatao:

Siku ya Jumamosi, tarehe 29 Julai, resi za baiskeli hatua ya mchujo, zitafanyika kwa kujumuisha makundi matatu yanayokimbia kwa kupitia barabara tatu tafauti kiswani Pemba kama ifuatavyo:
 - Resi za Baisikeli kutoka Mkoani hadi Uwanja wa Gombani (Stadium) Chake Chake Pemba
- Resi za Baisikeli kutoka Gando hadi Uwanja wa Gombani (Stadium) Chake Chake Pemba.
- Resi za Baisikeli kutoka Konde hadi Uwanja wa Gombani (Stadium) Chake Chake Pemba.
Washindi 10 kutoka kila kikundi na barabara zilizotajwa hapo juu wataingia katika hatua ya fainali za resi za baiskeli zitakazofanyika siku ya Jumapili kama ilivyotajwa hapo awali. 

Fainali za resi za basikeli zitaanzia Uwanja wa Gombani hadi Vumawimbi, Makangale Pemba majira ya saa 1 kamili asubuhi.

Kwa upande mwengine, kutakuwa na mashindano ya kuogelea baharini yatakayofanyika siku ya Jumapili, Tarehe 30 Julai 2017 katika fukwe za Vumamwimbi. 

Shindano hili litawashirikisha waogeleaji mbali mbali nchini ambao washiriki wapatao 100 watachuana katika mpambano huu.

Mwisho, kutakuwa na resi za ngalawa zitakazofanyika tarehe 30 Julai, 2017, pia katika fukwe za Vumawimbi Pemba. 

Shindano litashirikisha ngalawa takribani 20 kutoka maeneo mbali mbali Kiswani Pemba kama vile Tumbe, Kiuyu, Msuka, Shumba Mjini, Mwambe na Mnarani.

Tamasha hili limedhaminiwa na ZURA (Zanzibar Utility Regulatory Authority) na litarushwa hewani na kituo  cha Televisheni cha AZAM ambao ni washirika wenza wa Kampuni ya Rafiki Network.

Kwa niaba ya Rafiki Network, tunapenda kuwashukuru na kuwaomba watanzania wote kushiriki kwa njia moja au nyengine katika kufanikisha tamasha hili.

Mwisho kabisa, tunaomba na tunakaribisha vyombo vya habari kuja na kuripoti matukio haya ya kihistoria kwa maslahi ya maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa jumla.  

Rafiki Network Co. L.t.d : “akufaayekwadhiki….!”
Ahsanteni,
Ali Othman Ali
MkurugenziwaHabarinaMahusiano
RAFIKI NETWORK CO. LTD


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.