NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAZAZI na walezi ambao watoto wao wanaendelea kuokota
karafuu zinazoanguka chini “mpeta” wamesema kwa kipindi hichi cha msimu wa zao
la karafuu, waalimu wa vyuo vya Qur-an wataendelea kuwakosa watoto, hasa siku
za mwisho mwa wiki.
Walisema
kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa watawalazimishe wabakie kwenye madrassa na
skulini, lakini siku mbili za mwisho wa wiki, wawasamehe maana hufuatana nao
katika kazi ya kuokota mpeta.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu wananchi hao wa vijiji vya Ngomeni, Chambani, Mtambile,
Mtuhaliwa, Wambaa, Mwambe, Kiwani, Pujini na Mgelema walisema lazima wawashajishe watoto kuokota
karafuu.
Mmoja
katia ya wazazi hao Hamida Issa Ussi wa Bwegeza Mwambe, alisema kwa vile
wanapokuwa na watoto wake wanne, hujipatia kati ya shilingi 32,000 hadi
shilingi 40,000 kwa siku, hafikirii wanawe kuwakatisha kuokota mpeta kwa siku
mbili kwa wiki.
“Mimi
wanangu siku zote tano huwataka na kuwalazimisha kushiriki kwenye masomo,
lakini kwa siku za Jumamosi na Jumapili, waalimu wa madrassa au skuli kwa
masomo ya ziada hawapatikani”,alisema.
Asha
Mselemu Habibu wa Pujini, alisema kutokana na hali yake ya maisha ya watoto
sita ambao baba yao ameshafariki miaka imnne sasa, lazima watoto wake wamsaidie
huduma za siku.
“Maisha
kwa sasa ni magumu na hasa ambao ni sisi wajane hatuna mtu wa kumtegemea,
kipindi kuna riziki ya karafuu na keshokutwa yaondoka, lazima watoto tutoke
pamoja”,alieleza.
Aidha
mzazi huyo alisema mwanawe mmoja anasoma darasa la kumi akitarajiwa kufanya
mitihani miezi michache ijayo, lakini suala la huduma za ndani kwa kipindi
hichi nae linamgusa.
Kwa
upande wake Mwanaisha Kassim Ussi, alisema hata vyuo vya Qur-an wapo baadhi ya
waalimu wamekubali kuvifunga kwa wanafunzi wanaookota mpeta, maana wamekuwa
wahazuiliki.
“Alfjairi
swala swala kwa siku za Jumamosi na Jumapili watoto wote wakiwemo wangu watano,
huwa tunatoka kwenda Ngomeni kuokota karafuu, na mimi wala siwazuii maana siku
tano za wiki zawatosha kusoma”,alifafanua.
Mwalimu
mmoja wa madrasaa Mwambe wilaya ya Mkoani, Mcha Hassan Jaku, alisema ana idadi
ya wanafunzi 45 kwenye madrassa yake, ingawa kwa siku za mwishoni mwa wiki
huopungua mara tatu.
“Wanafunzi
ninaobaki nao kuhudhuria madrassa kwa siku za Jumamosi na Jumapili, ni wale
ambao wazazi wao wanafanyakazi serikali pekee, lakini wengine wote huwenda
Ngomeni na Mtambile kuokota mpeta”,alifafanua.
Hata
hivyo alisema, wapo baadhi ya wazazi waliotaka madrassa hizo kwa kipindi hichi
kufungwa hasa mwishoni wa mwiki, ingawa yeye na kamati yake ilikataa.
Msaidi
mwalimu mwalimu wa madrsaa Hassan Haji Hassan wa Chambani, alisema wamefika
pahala wamechoka kuvutana na baadhi ya wazazi na sasa wamewaachia watoto ili
kushiriki uokotaji mpeta.
“Tokea
tunawapiga, kisha tukamua kuwafukuza madrssa lakini wameendelea kuwazuia watoto
wao, na sisi wanaokuja kwa siku mbili hizo za mwisho wa wiki tunawasomesha,
lakini naamini msimu wa uvunaji wa karafuu ukimalizika watakuja kama
kawaida”,alisema.
Mkuu
wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdulla, ameendelea kutoa tamko lake la
kuwataka wazazi na walezi kutowaruhusu watoto wao na wao wenyewe wasiokote
mpeta.
Alisema
kwanza watoto hao wanatakiwa kuhudhuria kwenye mdarassa na skulini ili
kukabiliana na mitihani ya taifa, ambayo inatarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Serikali
za wilaya na mikoa kisiwani Pemba, zilishapiga marufuku tokea mwanzoni mwa
msimu, kwamba hakuna mwanamke wala mtoto anaeruhusiwa kuokota mpeta, kwa mdai
ya kuongozeka vitendo vya udhalilishaji katika kipindi kama hiki.
No comments:
Post a Comment