Habari za Punde

Mamlaka zazungumzia kuzama kwa daladala Ziwa Victoria Mkoani Mwanza

Watu 12 wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa baada ya daladala waliyokuwa wakisafiria, kutumbukia katika fukwe za Ziwa Victoria katika eneo la Kingo Feri wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa tano asubuhi baada ya daladala hiyo yenye nambari za usajili T.229 DDW Toyota Hiace iliyokuwa ikitokea Buhongwa Jijini Mwanza kwenda kivukoni hapo kudaiwa kukatika breki ikiwa kwenye mwendo kasi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.