Habari za Punde

Rais Magufuli akutana na baadhi ya viongozi wastaafu Ikulu leo

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza Viongozi Wakuu mbalimbali wakiwemo, Marais Wastaafu, Makamu wa Rais Wastaafu, Mawaziri Wakuu Wastaafu, Maspika Wastaafu na Majaji Wakuu Wastaafu wakati wa Kikao chake Ikulu jijini Dar es Salaam.
 . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Wakuu mbalimbali wakiwemo, Marais Wastaafu, Makamu wa Rais Wastaafu, Mawaziri Wakuu Wastaafu, Maspika Wastaafu na Majaji Wakuu Wastaafu mara baada ya kuzungumza nao Ikulu jijini Dar es Salaam. Waliokaa mstari wa mbele ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Ali Hassan Mwinyi,(watatu kutoka kushoto), Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamini Mkapa(watatu kutoka kulia) Waziri Mkuu Msaafu Cleopa David Msuya wapili kutoka kulia, Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume wapili kutoka kushoto, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Spika wa Bunge Job Ndugai. Waliosimama mstari wa nyuma kutoka kulia kuja kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Jaji Mkuu Mstaafu Agustino Ramadhan, Spika Mstaafu Mama Anna Makinda, Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela, Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta, Spika wa Bunge mstaafu Pius Msekwa, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowwasa, Makamu wa Rais Mstaafu Mohamed Gharib Bilal, Waziri Mkuu mstaafu Joseph Sinde Warioba, Waziri Mkuu Msatafu Mizendo Pinda pamoja na  Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Othman Chande.

 Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamini Mkapa akizungumza katika mkutano huo Ikulu jijini Dar es Salaam
 Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa akizungumza katika mkutano huo Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Waziri Mkuu Mstaafu John Samwel Malecela akizungumza katika mkutano huo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye akizungumza katika mkutano huo Ikulu jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.