Kocha Mkuu wa Timu ya Malindi Sports Club Zanzibar Abdulghani Msoma akiwa katika mazoezi ya Timu yake mpya akiinoa kwa ajili ya Michuano ya FA katika mchezo wa Nusu Fainali na Ligi Kuu ya Zanzibar Msimu wa mwaka 2018/2019, inayotarajiwa kuanza mwezi ujao. Timu ya Malindi imefanikiwa kurudi Daraja la Kwanza Taifa baada ya kupanda na Timu ya Malandege.
Viongozi wa Timu ya Malindi wakitowa nasaha kwa wachazaji wao baada ya mazoezi ya asubuhi yanayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar.
Kocha Mkuu wa Timu ya Malindu Abdulhani Msoma akisoma dua baada ya kumaliza mazoezi ya asubuhi katika uwanja wao wa mnazi mmoja Zanzibar.
No comments:
Post a Comment