Habari za Punde

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Tanzania Mhe.Luhaga Mpina Awamwagia Mabilioni Wavuvi Nchi Nzima.



Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina, akizungumza wakati wa mkutano wake na  watendaji wa Wizara yake.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya  Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji, Mahmoud Mgimwa(Aliyesimama) akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina na Mjumbe wa Kamati hiyo Calist Komu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina wa pili kutoka kushoto akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali waliohudhuria kikao hicho mara baada ya kumalizika

Na.John Mapepele -Mwanza.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ametoa muda usiozidi mwezi mmoja kwa watendaji wa Wizara yake kufanya marekebisho ya Kanuni Uvuvi ya Mwaka 2009 ili kuruhusu kuvuliwa kwa samaki aina ya Sangara kuanzia sentimita 50 na kuendelea ili kudhibiti utoroshwaji wa samaki hao kwenda nchi jirani na kuifanya Serikali na wadau wa uvuvi kupata mapato makubwa zaidi kutokana na  uhifadhi unaofanywa katika Ziwa Victoria.

Akizungumza kwa katika kikao cha pamoja baina ya Kamati ya Bunge ya kudumu  ya kilimo mifugo na maji  na makundi ya wadau wa sekta uvuvi katika ukumbi wa mkutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza mwishoni mwa wiki,Mpina amesema kanuni ya sasa ya uvuvi inaruhusu kuvuliwa kwa Samaki Sangara kuanzia sentimeta 50 hadi 85 hali ambayo inawafanya samaki wakubwa zaidi ya sentimita 85 kuuzwa katika nchi jirani kwa kuwa nchi nyingine zinaruhusu kuvuliwa kwa samaki hao na Tanzania kubakia kuwa eneo la mazalia na malisho ya samaki hao.

“Wizara yangu haitalala itahakikisha kwamba wananchi wananufaika na biashara ya samaki na mazao yake, lishe bora na ajira zaidi zinazotokana na uhifadhi, sisi akina Mpina ni vibarua tu wa kulinda raslimali za uvuvi kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye kwa hiyo tuendelee kudhibiti uvuvi haramu ili uvuvi ututajirishe” alisisitiza Mpina

Aidha ametoa muda wa wiki mbili kwa Taasisi ya Utafiti wa Samaki nchini(TAFIRI) kushirikiana na wavuvi wa  Bahari ya Hindi kufanya utafiti wa vyavu za kuvulia dagaa mchele ili kupata majibu ya kisayansi yatakayosaidia kutoa uamuzi wa kutumia nyavu  za kutoka sentimeta 10 hadi sentimeta 8.

Waziri Mpina alisema  kutokana na udhibiti wa uvuvi haramu  uliofanywa na wizara yake katika kipindi cha mwaka mmoja sasa ripoti iliyowasilishwa katika kikao cha Mawaziri wa sekta uvuvi kwa  nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanazunguka ziwa Victoria jijini Arusha mwanzoni mwa mwezi Machi mwaka  huu inaonyesha kuwa  samaki wazazi aina ya Sangara wameongezeka katika ziwa Victoria kutoa asilimia o.4 ya awali hadi kufika  asilimia 5.2  ambapo kwa kawaida  inatakiwa kufikia kiwango cha alisimia 3.3 huku  samaki waliokuwa wanaruhusiwa kuvuliwa (ambao ni sentimita  50-85) kuongezeka kutoka asilimia 3 hadi 32 na samaki wachanga kupungua kutoka asilimia 96.6 hadi 63.

Alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kusimamia kikamilifu Sheria ya Uvuvi Namba 22 ya Mwaka 2003 pamoja na Kanuni zake za Mwaka 2009 ambapo aliongeza kuwa njia pekee kwa wavuvi ni kuzingatia sheria badala ya kutaka kuonewa huruma  na vyombo vya Serikali huku wakiendelea kufanya uvuvi haramu.

Katika hatua nyingine Mpina ametoa onyo kali kwa wamiliki wa viwanda vya kuchakata samaki kuacha mara moja kupuuza maagizo ya Serikali ya kuwataka kuzingatia bei elekezi ya kuanzia shilingi 5500 kwa samaki aina ya Sangara kutoka kwa wavuvi ambapo amesisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yoyote atakayebainika.

Alisema ni kosa kwa wamiliki wa viwanda vya samaki kupunguza  bei za kununua Sangara kwa wavuvi kwa visingizio  kuwa bei imeshuka katika masoko ya kimataifa bila kutoa uthibitisho wowote.

Akitolea ufafanuzi juu ya hoja mbalimbali zilizowasilishwa kwa Serikali na wadau wa uvuvi Mpina alisema Wizara yake inatambua kumekuwa na changamoto  na mapungufu katika sekta ya uvuvi nchini ndiyo  maana Wizara imeamua kuifumua Sheria ya Uvuvi ili ifanyiwe marekebisho na kutunga Sheria nyingine ya utunzaji wa viumbe kwenye maji ili wadau wote waweze kuchangia  mawazo yao  na kuboresha ili iendane na mazingira ya sasa.

Pia Mpina alisema  Serikali imeamua kuruhusu taa za mwanga wa jua na majenereta kwa wavuvi ambapo amesisitiza kuwa serikali inaendelea na utafiti ili kuona teknolojia
Kuhusu suala la kusafirisha samaki kwa kutumia gari  maalum  na serikali kutoruhusu  kuchukua  samaki kilo 20 hadi zilipiwe alisema kwamba tayari Serikali ilishalitolea ufafanuzi kwamba  wananchi hawazuiliwi kubeba kiasi hicho cha samaki pia gari yoyote inayozingatia usafi inaruhusiwa kubeba samaki.

Alionya watanzania kuendelea kutumika kama madalali wa wafanyabiashara wa dagaa kutoka nchi jirani na kujifanya kuwa ndiyo wanunuzi ilhali wanafanya hivyo kukweka  kulipa kodi za Serikali.

Akichangia katika mkutano huo mbunge Mheshimiwa Emanuel Papiani alipongeza juhudi zinazofanywa na Wizara ambapo aliwataka wamiliki wa viwanda vya kuchakata samaki kufanya  biashara kwa uaminifu na kufanya  biashara zao kwa uwazi na kushirikiana na serikali tofauti na ilivyo sasa ambapo wamekuwa wanashusha bei za samaki bila kuishirikisha Serikali na wadau wengine wa sekta ya hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya  Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji, Mahmoud Mgimwa aliipongeza Wizara kwa jitihada  na mikakati mbalimbali inayoibuni kwa wavuvi ili kuwasaidia  waweze kupata manufaa na shughuli za uvuvi

Mgimwa alisema  katika kipindi cha muda mfupi Wizara imeanzisha Dawati maalum linaloshughulikia  sekta  binafsi katika  kuwaunganisha  na fursa mbalimbali ambapo pia Wizara imesaidia kuwashawishi  benki ya kilimo kuanzisha  benki hiyo katika jiji la mwanza ili kutoa mikopo kwa wavuvi.

Alisema kamati yake imekuwa ikifanya kazi kwa  karibu na Wizara  na itaendelea  kuisimamia na kutoa maelekezo mbalimbali kwa niaba ya wananchi ili kuweka daraja baina ya serikali na wananchi.

Alisema alifarijika kuona kuwa maelekezo yote yanayotolewa na Kamati yake kwa Wizara yanafanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na marekebisho ya Sheria ya Uvuvi na 22 ya Mwaka 2003 ambapo aliwahakikishia wa wavuvi kuwa maoni yao yatazingatiwa katika sheria  mpya na kwamba wana fursa mbili  za kushiriki  katika utoaji wa maoni  hayo  yakifikishwa bungeni na kabla ya kufika bungeni.

Naye mvuvi na mfanyabiashara wa mabondo onesmo Nzagamba  amepongeza  juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya Tano za kuwasilikiliza wadau wa sekta ya uvuvi ambapo amesema  maamuzi na maelekezo ya Waziri Mpina yatawanufaisha siyo tu wavuvi bali wananchi wengi masikini.

“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufuli na Serikali yake kwa kuendelea kutujali sisi wanyonge” alisisitiza Nzagamba

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.