Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar Mhe. Maudline Castico, akizungumza na kutowa neno la shukrani kwa Niaba ya Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, baada ya kumalizika kwa futari maalum aliyowaandalia Watoto wa Nyumba ya Watoto Yatima Maziziniu Zanzibar.
WAZIRI wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto Moudline
Castico ameipongeza jamii ya Wazanzibar kwa juhudi inazozichukuwa katika
utunzaji wa familia, na hivyo kupunguza tatizo la utupaji wa watoto ovyo.
Ametowa
pongezi hizo kituo cha kulelea watoto
Mazizini, wakati akitowa neno la shukrani baada ya hafla ya Futari
iliyoandaliwa kwa pamoja kati ya Mke wa
Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Mke wa Makamo wa Pili wa Rais wa
Zanzibar, Mama Asha Suleiman Idd, kwa ajili ya watoto wa kituo hicho.
Alisema
ni jambo la faraja kuona katika siku za hivi karibuni vitendo ya utupaji wa
watoto vimepungua, hatua aliyobainisha inatokana na juhudi za wananchi katika
utunzaji wa familia zao.
Aliiomba
jamii kuendelea na juhudi hizo zinazotokana na ushirikiano wa pamoja kati ya
jamii hiyo na Serikali.
Aidha,
Waziri Castico alitumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi hao kutokana na mchango
mkubwa wanaouonyeha katika kuleta maendeleo na ustawi bora wa watoto hapa
nchini, ikiwemo wale wanaoishi katika mazingira magumu.
Alisema
hafla hiyo iliyowahusisha watoto wanaolelewa katika kijiji hicho inadhihirisha
imani na mapenzi makubwa waliyonayo viongozi hao kwa watoto hao, hivyo
akawaomba kuendelea kuwa karibu nao katika vipindi vyote.
Katika
hatua nyengine, Waziri Castico aliutaka uongozi wa kituo hicho kuendelea
kuwatunza vyema watoto hao, sambamba na kutoa indhari ya kuwepo umakini wa kiusalama katika kipindi
cha sherehe ya sikukuu ya Idd el Fitri.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail:
abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment