Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika,
akifuatilia mada mbalimbali kwenye kongamano la siku maalum dhidi ya Rushwa
iliyofanyika katika Maonesho ya 43 ya Kimataifa
ya Biashara Sabasaba yanayoendelea
katika viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Katibu Mkuu
wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Dkt.Bashiru Ally na kulia ni Mkurugenzi Mkuu Takukuru,
Diwani Athuman.
Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika,
akifurahia jambo katika kongamano la siku maalum dhidi ya Rushwa iliyofanyika
katika Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya
Biashara Sabasaba yanayoendelea katika
viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Musa Assad, Katibu Mkuu wa Chama Cha
Mapinduzi(CCM), Dkt.Bashiru Ally.
Katibu Mkuu wa Chama
Cha Mapinduzi(CCM), Dkt.Bashiru Ally, akiteta Jambo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
Prof. Musa Assad, kwenye kongamano la siku maalum dhidi ya Rushwa iliyofanyika
katika Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya
Biashara Sabasaba yanayoendelea katika
viwanja vya Julius NyerereJijini Dar es Salaam,
Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika akufuatilia
mijadala mbalimbali kwenye kongamano la siku maalum dhidi ya Rushwa
iliyofanyika katika Maonesho ya 43 ya
Kimataifa ya Biashara Sabasaba
yanayoendelea katika viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam,
kushoto ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Musa Assad (wa
kwanza kushoto), Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Dkt.Bashiru Ally.
Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Takukuru, Diwani Athuman akisisitiza
jambo wakati wa kuwasilisha Mada yake kuhusu Mwelekeo wa Taasisi hiyo katika
mapambano dhidi ya Rushwa, katika kongamano la siku maalum dhidi ya Rushwa
iliyofanyika katika Maonesho ya 43 ya
Kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea
katika viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa
kongamano la siku maalum dhidi ya Rushwa lililofanyika katika Maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Julius
Nyerere Jijini Dar es Salaam wakifuatilia kwa makini kongamano hilo.
Na Mwandishi Wetu, MAELEZO DAR ES SALAAM 3.JULAI, 2019
WAZIRI wa nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora), George Mkuchika amesema Tanzania inaendelea kupata
heshima kubwa katika Jumuiya ya Kimataifa katika vita vya mapambano dhidi ya
rushwa kutokana na mshikamano na nguvu ya pamoja iliyopo katika vyombo na
taasisi zinazosimamia utawala bora nchini.
Akizungumza katika kongamano la siku maalum dhidi ya
rushwa katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea Jijini Dar es
Salaam leo Jumatano (Julai 3, 2019) Waziri Mkuchika alisema utafiti uliofanywa
na taasisi hizo zimesifu juhudi za zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano na
kuitaja Tanzania kuwa ni nchi ya mfano katika vita vya mapambano dhidi ya
rushwa.
Mkuchika aliasema taasisi hizo zikiwemo MO Ibrahim,
Transparency International, APRM na taasisi nyingine kubwa duniani
zinazosimamia masuala ya utawala bora zimefanya utafiti na kusifu juhudi kubwa
zinazofanywa na serikali ya Tanzania
chini ya Rais Dkt. John Magufuli katika mapambano dhidi ya rushwa ambapo tafiti
mbalimbali zimeifanya Tanzania kushika nafasi ya pili nyuma ya nchi ya Rwanda.
Waziri Mkuchika alisema Serikali ya Awamu ya tano imeendelea
kuweka mkazo na msukumo katika mapambano
dhidi ya rushwa ambapo taasisi zote zinazosimamia masuala ya utawala bora zimekuwa
zikiunganisha nguvu ya pamoja na kulifanya suala la rushwa sasa kuwa na nguvu
na msukumo mpya wa mapambano katika jamii.
“Kwa sasa vyombo vyetu vyote serikalini si TAKUKURU
pekee bali pia polisi, tiss (usalama wa taifa), Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali ICAG) na vingine vyote, vimeendelea kuunga katika
kusimamia masuala ya utawala bora na hili limeleta msukumo na hamasa mpya katika
vita dhidi ya rushwa hapa nchini” alisema Waziri Mkuchika
Akizungumzia rushwa katika sekta ya viwanda na
biashara, Waziri Mkuchika alisema Serikali imeendelea kuweka mikakati
mbalimbali katika kupunguza tatizo hilo ambalo limekuwa likiathiri sekta
binafsi ambayo imekuwa mshirika wa karibu wa serikali katika kutekeleza miradi
mbalimbali ya maendeleo nchini.
Kwa mujibu wa Waziri Mkuchika alisema rushwa katika
sekta biashara imekuwa ikiathiri sana masuala ya uwekezaji wa kigeni, ambapo
eneo lililonyesha kutawala kwa rushwa ni katika eneo la utoaji wa vibali na
leseni kutoka katika taasisi na idara muhimu za serikalini na hivyo serikali
imeendelea kulifanyia kazi ili kuhakikisha kuwa vikwazo hivyo vinaondolewa kwa
wawekezaji na hivyo kuharakisha ukuaji wa uchumi.
Akifafanua zaidi Mkuchika anasema kutokana na serikali
kutambua mchango wa sekta ya viwanda na biashara katika kukuza uchumi na
uzalishaji wa ajira nchini ili kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, Serikali
imekuwa ikifanya marekebisho mbalimbali ya sheria na sera mbalimbali ambazo
zimekuwa ni sehemu ya mianya ya rushwa nchini ikiwemo eneo la kodi.
“Kutokana na kudhibiti rushwa kwa sasa kiwango cha
ukusanyaji wa mapato ya mwezi yameweza kuongezeka kutoka Tsh Bilioni 800 kwa
mwezi hadi kufikia Tsh trilioni 1.3 hii inaoyesha kuwa kulikuwa na maeneo
ambayo kulikuwa na uvujaji wa mapato ya serikali kulikochangiwa na sababu
mbalimbali ikiwemo rushwa”
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Diwani Athumani alisema serikali imeendelea
kushirikiana na wadau wa sekta binafsi kupitia Mpango Mkakati dhidi ya
mapambano ya rushwa (NASCAP III) ili kuhakikisha kuwa mapambano na vita dhidi
ya rushwa yanapata mafanikio nchini.
Anaongeza kuwa kupitia NASCAP III, ofisi yake
imeendelea kutekeleza masuala mbalimbaliu ikiwemo kufanya tafiti kubaini ukubwa
na kiwango cha rushwa nchini, kupokea maoni, kutoa elimu kwa umma kupitia
makongamano, rushwa pamoja na kufanya uchunguzi na kufungua mashtaka kwa watu
mbalimbali wanaopatikana na hatia dhidi ya rushwa.
No comments:
Post a Comment