Na. Grace Semfuko,MAELEZO
Shirika la Reli Tanzania TRC limeanza kukarabati njia ya Reli
ya kati ya kutoka Dar Es Salaam mpaka Isaka iliyopo Wilaya ya Kahama Mkoa wa
Shinyanga takribani kilomita 970 ili kuimarisha reli hiyo yenye kiwango cha
Mitagauge zoezi ambalo lilianza Juni mwaka huu na kutarajia kukamilika mwaka
2020.
Katika Utakabati huo Shirika hilo linatarajia kufunga njia za
reli hiyo kwa saa 72 kwa wiki ikiwa ni sawa na siku tatu kwa Wiki kwa muda wa
miezi mitano kuanzia Julai hadi Novemba 2019, zoezi zoezi ambalo kukamilika kwake kutaingiza faida mara dufu
ya usafiri huo.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Shirika hilo Masanja
Kadogosa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye viwanja vya Maonesho
ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam na kubainisha kuwa
kukamilika kwa Reli hiyo kutaongeza mapato ya usafirishaji wa Reli kwa asilimia
mia moja.
“Waandishi wa Habari na Watanzania kwa ujumla, TRC sasa
tunakuja kuimarisha miundombinu yenu ya Reli, tunafanya hivi kwa kuwa tunafahamu
mnahitaji huduma hizi, tunaomba mtuvumilie kwa siku ambazo tutafunga njia
hizi”alisema Kadogosa.
Alisema kwa treni za kawaida za mjini (Cummuter Train) za
kutoka Kamata kwenda Ubungo na Pugu zitafanya kazi siku za jumatatu hadi Ijumaa
huku Treni za kawaida (Ordinary Train) za kutoka Dar Es Salaam kwenda Kigoma,
Mwanza na Mpanda zitafanya kazi siku za Jumatatu na Jumatano saa tisa alasiri
tu na treni za Deluxe ya kutoka Dar kwenda Kigoma zitakuwepo siku ya Jumanne
pekee.
Alibainisha kuwa ukarabati mwingine wa njia ya Reli kutoka
Tanga kwenda Arusha ulianza mapema mwaka
huu ambapo njia hiyo itaanza kutumika mwezi Desemba mwaka huu.
“Ndugu zangu wa mikoa ya Kaskazini mtaanza kunufaika na usafiri
wa treni ya Abiria kuanzia Desemba mwaka huu, yaani Sikukuu zaKrismas na Mwaka
mpya mtaenda nyumbani na Treni ya Abiria ya TRCälisema Kadogosa.
Akizungumzia ujenzi wa Reli ya Standard Gauge inayoendelea
kujengwa Nchini Kadogosa alisema kwa awamu ya kwanza kutoka Dar Es Salaam
kwenda Morogoro ujenzi huo umefikia asilimia 56.
No comments:
Post a Comment