Habari za Punde

Maadhimisho ya Siku ya Haki za Watoto Duniani

Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi (katikati), akifurahia jambo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndungulile (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Ally Possi, mara baada ya kuwasili katika Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.

Mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala mwaka wa Tatu, Rose Mweleka, akiwasilisha mada kuhusu jinsi ya kutekeleza haki za watoto wa kike ikiwemo kuwafundisha hatua za makuzi ili kuwawezesha kukabiliana na hali wakifikia umri husika, Mada hiyo iliwasilishwa kwenye Maadhimisho ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi (kulia), akiteta jambo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndungulile, baada ya kuwasili katika Sherehe za Kuadhimisha ya Siku ya Haki ya Mtoto Duniani iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere, leo Novemba 20, 2019, ambako alialikwa kuwa mgeni Rasmi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.