Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.Ndg. Khatib Mwadin, hafla hiyo imefanyika Ikulu Jijini Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali
Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi mbali mbali kushika nyadhifa baada ya
kuwateuwa hivi karibuni.
Katika hafla hiyo iliyofanyika Ikulu mjini hapa na kuhudhuriwa
na viongozi mbali mbali wa Serikali, Dk. Shein amemuapisha Khatib Mwadini
Khatibu kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Ame Burhan
Shadhil kuwa Naibu Mhasibu Mkuu wa Serikali.
Miongoni mwa
waliohudhuria katika hafla hiyo ni pamoja na
Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Katibu wa Baraza la Mapinduzi
na Katibu Mkuu Kiongozi Abdulhamid Yahya
Mzee, Mawaziri, Spika wa Baraza la Wawakilishi,
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi, Washauri wa Rais pamoja na watendaji mbali
mbali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Naibu Mhasibu Mkuu wa Serikali Ndg.Ame Burhan Shadhil, hafla hiyo imefanyika Ikulu Jijini Zanzibar.
No comments:
Post a Comment