Habari za Punde

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dkt. Haruni Kondo, akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya mafanikio na matarajio ya shirika hilo, kwa mwaka 2019/2020, mara baada ya Mkutano Mkuu wa Pili wa Mwaka, (2nd Annual General Meeting), jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Elia Madulesi, akizungumza wakati akimkaribisha Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe (picha ya chini), kabla ya Mwenyekiti wa shirika hilo, Kanali Mstaafu, Dkt. Haruni Kondo (hayupo pichani), kutoa taarifa ya mafanikio na matarajio ya shirika kwa mwaka 2019/2020, jijini Dar es Salaam leo.
Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe, akizungumza na waandishi katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dkt. Haruni Kondo, akitoa taarifa hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu Dkt. Haruni Kondo, akifafanua jambo kwa  waandishi wa habari katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dkt. Haruni Kondo, akisisitiza jambo.
Baadhi ya wa Wajumbe ya Bodi ya Shirika wakiwa katika mkutano huo. 
Mjumbe wa Bodi Bibi Fatma  Juma na Postamasta Mkuu Hassan Mwang'ombe, wakifuatilia taarifa iliyokuwa ikitolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika hilo, Kanali Mstaafu Dkt. Haruni Kondo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dkt. Haruni Kondo, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania, mara baada ya mkutano huo. Kulia waliokaa ni Mwakilishi wa Katibu Mkuu (Mawasiliano), Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Bibi Kitolina Kippa na Mwakilishi wa Msajili wa Hazina, Bw. Elikana Mtumweni. Aliyesimama kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu (TCRA), Bw. Wilfred Maro.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Kanali Mstaafu, Dkt. Haruni Kondo, katika picha ya pamoja na menejimenti ya Shirika la Posta Tanzania.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.