Habari za Punde

RC Kusini Unguja apongeza zoezi la kurejewa kazi ya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za wapiga kura


Na Jaala Haji Makame, ZEC


Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud alisema kurejewa kwa kazi ya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za Wapiga Kura kwa Mikoa yote ya Zanzibar ni ishara moja wapo ya mafanikio makubwa kwa nchi yenye nia ya kuimarisha demokrasia nchini.

Akizungumza katika kituo cha Uandikishaji cha Bungi wakati akifanya ziara katika vituo vya Uandikishaji alisema hatua hiyo imewajengea imani wananchi na kuondosha malalamiko ambayo yangeweza kujitokeza katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu.

Mhe. Ayoub aliendelea kuwasisitiza wananchi ambao bado whawajaandikishwa na kuhakikiwa taarifa zaao kushiriki kikamilifu katika kazi hiyo kwa salama na utulivu wa hali ya juu.

Aliendelea kusema kuwa  ni jukumu la viongozi wa vyama vya siasa kuhakikisha wanaendesha siasa za kistaarabu  na kufuata Sheria, Kanuni, Miongozo na taratibu zinazotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ili kufikia dhamira ya kuendesha Uchaguzi Mkuu na kuufanya Uchaguzi huo kuwa huru na wa haki.

Aidha, alisisitiza kuwa  Viongozi wa Mikoa na Wilaya wanajukumu la kuwahamasiha wananchi ili wajitokeze kwenda kujiandkisha na kuhakikisha hali ya utulivu na Amani inakuwepo katika maeneo ya vituo vya kujiandikisha.

“ sisi viongozi wa Mikoa na Wilaya tunajukumu la kuwahamasisha wananchi waendelee kujitokeza kujiandikisha…………” alisema.

Nao Mawakala wa vyama mbali mbali vya siasa katika vituo vya uandikishaji walitoa ushauri kwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuendelea kutoa mafunzo kwa Wapiga Kura licha ya mafanikio yanayopatikana hivi sasa katika vituo vya uandikishaji na uhakiki wa taarifa za Wapiga kura ili wananchi waendelee kujitokeza zaidi.

Kazi ya Uandkishaji na uhakiki wa taarifa za Wapiga Kura imekamilika kwa mikoa yote ya Pemba na Mkoa wa Kaskazini na Kusini kwa Upande wa Unguja ambapo kazi hiyo itaendelea tarehe 9 na 10/6/2020 Wilaya ya Magharibi “A” na Wilaya ya Magharib “B” na kukamilisha mzunguuko wa raatiba ya uandikishaji katika Wilaya ya Mjini tarehe 11 na 12/6/2020


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.