Habari za Punde

Kumuomba Mwenyenzi Mungu Azidi Kuiletea Zanzibar Amani na Maendfeleo Makubwa.-Alhaj Dk. Hussein Mwinyi.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia Wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja baada ya kumaliza kwa Futari Maalum aliyowaandalia Wananchi wa Mkoa wa Kusini katika ukumbi wa Dk.Ali Mohamed Shein,(SUZA) Tunguu Wilaya ya Kati Unguja


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi amefutari pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja na kumuomba Mwenyezi Mungu azidi kuieletea Zanzibar amani na maendeleo makubwa.

Hafla hiyo ya futari iliyoandaliwa na Rais Dk. Mwinyi kwa ajili ya wananchi wa Mkoa huo wa Kusini Unguja ilifanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein uliopo katika Kampasi ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), Tunguu, Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja ambayo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali, dini, vyama vya siasa pamoja na wananchi wa Mkoa huo.

Akitoa shukurani zake kwa wananchi waliohudhuria futari hiyo, Alhaj Dk. Mwinyi alisisitiza haja ya kuendeleza amani na maendeleo ili Zanzibar izidi kupiga hatua.

Alhaj Dk. Mwinyi alitoa shukurani kwa wananchi wote waliohudhuria futari hiyo aliyowaandalia na kutoa shukurani kwa kukubali na kuhudhuria muwaliko wake huo.

Aidha, Alhaj Dk. Miwnyi alieleza kwamba ameona haja ya kuandaa furati hiyo ili aweze kuungana na wananchi wa Mkoa huo katika mwezi huu mtufu wa Ramadhani.

Katika shukrani zak hizo, Alhaj Dk. Mwinyi alieleza utaratibu wake ambao ameuanza wa kufutari na wananchi wa  mikoa ya Unguja na Pemba ambapo kesho Jumaatatu ya Machi 03.2021 anatarajia  kufutari na wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Wakati huohuo, nae Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi kwa upande wake aliungana na viongozi wanawake wa kitaifa pamoja na wananchi wa Mkoa huo wa Kusini Unguja katika futari hiyo maalum aliyoianda  Dk. Mwinyi katika ukumbi huo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.