Habari za Punde

Mkoa wa Arusha na Manyara Mabingwa wa Mchezo wa Riadha Mita 1500 Michuano ya UMISSETA 2021 Mkoani Mtwara.

 
Mikoa ya Arusha na Manyara imeongoza kwenye mchezo wa Riadha mita 1500 katika Mashindano ya Taaluma na Michezo kwa Shule za Sekondari (UMISSETA) kwenye fainali zilizofanyika leo Juni 29, 2021 mjini Mtwara.

Msemaji wa UMISSETA 2021, John Mapepele amesema kwa upande wa wavulana Daniel Patric kutoka Arusha ameibuka mshindi wa kwanza baada ya kumaliza mbio hizo kwa kutumia muda wa dakika 4:07:16 akifuatiwa na Paul Ndege kutoka mkoa wa Mara aliyetumia dakika 4:11:06 wakati nafasi ya tatu imechukuliwa na Agustino Leonard kutoka Mkoa wa Manyara aliyemaliza mbio hizo kwa dakika 4:12:44.

 Kwa upande wa wasichana Leoma Awaki kutoka Manyara ameibuka mshindi wa kwanza baada ya kumaliza mbio hizo kwa kutumia muda wa dakika 4:44:50 akifuatiwa na Esther Martin kutoka mkoa wa Pwani aliyetumia dakika 4:46:80 wakati nafasi ya tatu imechukuliwa na Nyanzobe Mbahi kutoka Mkoa wa Mara aliyemaliza mbio hizo kwa dakika 4:49:66.

Wakati huo huo Mkoa wa Unguja kwa upande wa wavulana umeibuka mshindi wa kwanza katika mbio za kupokezana vijiti mita 4x100 (relay) kwa kutumia dakika (0:45:53), wakifuatiwa na mkoa wa Shinyanga (0:47:10), mkoa wa Tabora umeshika nafasi ya tatu (0:47:20), mkoa wa Pwani nafasi ya nne (0:48:53), mkoa wa Mara nafasi ya tano (0:50:91), na mkoa wa Dodoma umeshika mkia 0:51.09

Kwa upande wa wasichana mkoa wa Njombe umeibuka mshindi wa kwanza katika mbio za kupokezana vijiti mita 4x100 (relay) kwa kutumia dakika (0:55:66), wakifuatiwa na mkoa wa Mara (B 0:56:16), mkoa wa Tabora umeshika nafasi ya tatu (0:56:19), mkoa wa Pwani nafasi ya nne (0:57:10) mkoa wa Simiyu nafasi ya tano (0:57:20) na mkoa wa Dodoma umeshika mkia (0:57:51)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.