Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Shirikisho la Somali Nchini Tanzania Ikulu leo

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsalimia Balozi wa Shirikisho la Somali Nchini Tanzania.Mhe.Zahra Ali Hassan,alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa ajili ya mazungumzo na kujitambulisha leo 23-11-2022.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Shirikisho la Somali Nchini Tanzania Mhe. Zahra Ali Hassan, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha leo 23-11-2022, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na mgeni wake Balozi wa Shirikisho la Somali Nchini Tanzania Mhe. Zahra Ali Hassan, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha leo 23-11-2022, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mgeni wake Balozi wa Shirikisho la Somali Nchini Tanzania Mhe. Zahra Ali Hassan, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 23-11-2022,alipofika kujitambulisha.(Picha na Ikulu)  

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amezungumza Balozi wa Shirikisho la Somali nchini Tanzania, Ikulu Zanzibar aliefika kwa ajili ya kujitambulisha.                                                                               

Dk. Mwinyi amewaomba wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Somalia kuja Zanzibar kwa ajili ya kuwekeza katika sekta mbali mbali, ikiwemo uanzishaji wa  Nyumba za makaazi.

Alisema Zanzibar ina fursa nyingi za Uwekezaji, huku akibainisha  miradi ya uanzishaji wa nyumba za makaazi kuwa ni eneo lenye fursa pana kwa ajili ya kuwekeza.

Aidha, alipongeza uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya Somalia na Zanzibar na Tanzania kwa ujumla, ambapo wananchi wa nchi hizo wamekuwa na maingiliano ya muda mrefu pamoja na kushirikiana katika nyanja mbali mbali za kijamii pamoja na kibiashara.

Nae, Balozi wa Shirikisho la Somalia nchi Tanzania Zahra Ali Hassan alishukuru mashirikiano makubwa yaliopo kati ya wananchi wa nchi mbili hizo, huku akibainisha azma ya wananchi wa Somali kuendeleza ushirikiano huo kwa kuwekeza katika miradi mbalimbali pamoja na kuimarisha biashara. 

Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano

Ikulu Zanzibar.

 


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.