Habari za Punde

Mhe Othman amuwakilisha Rais Dk Hussein Mwinyi Maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini 2022

 

                13.11.2022

IRINGA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussin Mwinyi ametoa wito kwa washiriki wa Maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini 2022 yaliyofanyika Mkoani Iringa Tanzania Bara kuitumia vyema fursa ya kuwepo maonesho hayo  kupanua wigo wa kibiashara sambamba na kuimarisha ushirikiano katika kukuza sekta hiyo nchini.

Mhe. Dk. Mwinyi ameyasema hayo Mkoani Iringa katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman katika ufungaji rasmi wa Maonesho ya Utalii yaliyopewa jina la Karibu Kusini yaliyofanyika  huko Iringa Tanzania Bara.

Aidha Dk. Mwinyi  amewahimiza viongozi na watendaji katika ngazi mbali mbali na wananchi kwa jumla kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhumuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasan katika kutangaza na kukuza sekta ya utalii hapa nchini na kwengineko duaniani.

Amefahamisha kuwa kupitia program ya Royal Tour Mhe. Rais amewafungulia watanzania fursa kubwa ya kuendeleza sekta ya Utalii nchini sekta ambayo inatoa mchango muhimu katika kukuza uchumi wa Tanzania , ustawi wa jamii pamoja na uhifadhi wa mazingira.

Dk . Mwinyi amewahimiza Watanzania kuvitembelea vivutio vya Utalii vilivyopo kusini mwa Tanzania ili kutekeleza kwa vitendo kauli mbinu ya nchi  ya uhifadhi wa maliasili ambayo ni hazina muhimu isemayo ‘ tumerithishwa tuwarithishe’   

Aidha Mhe. Mwinyi amesema kwamba Tanzania imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vyua Utalii vikiwamo  vya asili na historia, ikiwemo misitu ya asili inayohifadhi na viumbe wasiopatikana mahali popote duniani ispokuwa Tanzania sambamba na tamaduni na hiostoria zenye nguvu sana duniani ikiwemo ile ya Chifu Mkwawa , ngome ya Kolenga , maporomoko  ya maji , maziwa pamoja na milima  yenye muonekano na mandhari za kuvutia kiutalii.

Amesema kwa upande wa Zanzibar kuna fukwe za aina yake , mji mkongwe , maeneo ya historia  viongo na mazao ya aina hiyo  sambamba na kuwepo mandhari bora na tulivu ambapo wageni  mashuhuri na watalii kutoka kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika kwao ni vivutio  vikubwa vya kuja kuvitembelea. 

Mhe. Mwinyi ameeleza kwamba vivutio hivyo vilivyopo Tanzania kabla ya  maradhi ya uviko 19 mapato yatokanayo na sekta ya utalii yalifikia dola za Marekabili bilioni 2.6 na kuchangia wastani wa asilimia 17 ya pato la taifa  ambazo ni sawa na asilimia 25 ya pato la fedha za kigeni  na kuzalisha ajira zaidi ya milioni moja na lakini sita.

Amefahamisha kwamba mafanikio hayo ni matokeo ya juhudi za serikali  kwa kushirikiana na sekta binafsi kuendeleza sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kulifufua shirika la Ndenge Tanzania ATCL  ili kuimarisha sekta ya usafiri kwa  watalii na wageni mbali mbali .

Aidha amesema kwamba Tanzania imefanikiwa kuwa mwenyeji wa mikutano na matukio mbali mbali  ya kimataifa ikiwa ni mafanikio ya zao la kuanzisha  mpan go na program za utalii wa kimkakati  katika sekta ya Utalii ambapo yamesaidia sana katika kuitangaza Tanzania  na kuongeza idadi ya wageni wanaotembelea nchi.

Amesema maonesho ya  utalii ya Karibu Kusini 2022  yatakuwa na manufaa makubwa kwa kukuza utalii na kuongeza idadi ya wataali ambapo mwaka huu wa 2022 kuanzia Januari hadi Septemba  Tanzania imetembelewa na watalii wa kimataifa wapatao  moja elf thelathini nanne na mia na Themanini (1,034180).

Naye waziri  wa Maliasili na  Utaliii wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Balozi Dk. Pindi Chana, amesema kwamba maonesho hayo yatachangia sana katika kuiarisha jitihada kuitangaza Tanzania  katika kukuaza uwekezaji kwenye sekta ya utalii.

Amesema kwamba hatua hiyo inatikana na ukweli kwamba bado Tanzania inahitaji kufanya juhudi za kuionesha duania  maeneo na vivutio mbali mbali vile vya maumbile na vya historia vilivyopo nchini Tanzania kwa lengo la kukuza maendeleo ya biashara ya utalii ikiwa ni hatua ya kuingamkono Jitihada za Rais Samia.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Halima Omari Dendego akitoa salamu za Mkoa huo amasema kwamba kufanikiwa kwa  maonesho hayo muhimu ni maotokeo ya juhudi kubwa za ushirikiano wa viongozi mbali mbali wa Miko kumi ya Kanda ya Kusini katika kuendeleza jitihada za kimarisha utalii nchini. .

 

Maoneyo ya Utalii ya Karibu Kusini 2022 yaliyofanyika katika eneo Keisa Kilolo Iringa kuanzia tarehe tisa hadi 13 mwaka huu 2022 yamewashirikisha waoneshaji  wa sekta ya Utalii wa ndani nanje ya Tanzania na yamefungwa rasmi  leo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Mwinyi.

Mwisho.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha habari leo tarehe 13.11.2022.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.