Habari za Punde

ZMBF Inatekeleza kwa Vitendo Sera ya Uchumi wa Buluu

Mke wa Rais wa Zanzibar pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation Mhe,Mama Mariam Mwinyi (kulia) akisikiliza Makamo Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndg.Rehema Omary Sombi,(wa pili kulia) alipokuwa akitoa shukurani baada ya mazungumza na Viongozi wa Ngazi ya Taifa UVCCM waliofika kujitambulisha katika Ofisi ya Taasisi hiyo Migombani Jijiji Zanzibar
Mke wa Rais wa Zanzibar pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation Mhe,Mama Mariam Mwinyi (katikati) alipokuwa aki zungumza na Viongozi wa Ngazi ya Taifa UVCCM waliofika kujitambulisha katika Ofisi ya Taasisi hiyo Migombani Jijiji Zanzibar  wakiongozwa na Makamo Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndg.Rehema Omary Sombi,(wa pili kulia)
Mke wa Rais wa Zanzibar pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation Mhe,Mama Mariam Mwinyi (kulia) akisikiliza Makamo Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndg.Rehema Omary Sombi,(wa pili kulia) alipokuwa akitoa shukurani baada ya mazungumza na Viongozi wa Ngazi ya Taifa UVCCM waliofika kujitambulisha katika Ofisi ya Taasisi hiyo Migombani Jijiji Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation Mhe,Mama Mariam Mwinyi alipokuwa akisisitiza jambo wakati wa  mazungumzo na Viongozi wa Ngazi ya Taifa UVCCM waliofika kujitambulisha katika Ofisi ya Taasisi hiyo Migombani Jijiji Zanzibar  wakiongozwa na Makamo Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndg.Rehema Omary Sombi (hawapo pichani).

Na Mwashamba Juma.                                                                                                            

MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mama Mariam Mwinyi amesema taasisi hiyo inatekeleza kwa vitendo Sera ya Uchumi wa Buluu ya Serikali ya awamu ya nane ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mama Mariam Mwinyi aliyasema hayo kwenye ofisi za taasisi hiyo, Migombani Wilaya ya Mjini alipozungumza na ugeni kutoka jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi, UVCCM waliofika kumtembelea.

Alisema tokea kusajiliwa kwa ZMBF Febuari 19 mwaka jana ambayo kwasasa imetimiza mwaka mmoja, wanajivunia mafanikio makubwa ya utekelezaji wa Sera za Serikali kwa vitendo hasa sera ya Uchumi wa Buluu.

Alisema dhana ya Uchumi wa buluu kwa taasisi ya ZMBF imejikita kwenye harakati za kuwasaidia na kuungamkono juhudi za kinamama wanaojitoa kupigania maendeleo ya kiuchumi kupitia matunda ya baharini.

Alisema ZMBF imefanikiwa kuwafikia kinamama wengi Unguja na Pemba wanaujishughulisha na kilimo cha mwani na kueleza asilimia 90 ya ukulima huo hushirikisha kinamama.

Alisema katika jitihada za kuwaungamkono, ZMBF imewasaidia vifaa mbalimbali vya uvuvi kinamama hao ikiwemo boti zenye mashine, viatu vya kuvalia baharini, mashine za kusagia mwani zenye uwezo wa kusaga mwani mwingi kwa wakati hali iliyowasaidia kinamama hao kuongeza ufanisi wa kazi zao na kuwaongezea kipato kwa kukabiliana vyema na soko la bidhaa hiyo.

“Kutokana na mabadiliko ya tabianchi, siku hizi kinamama hufanya shughuli za kilimo cha mwani nje kidogo na usawa wa bahari kutokana na kina cha maji ya bahari wanayolimia tofauti na zamani walilima maeneo karibu hivyo, ZMBF imeona haja ya kuwasaidia vifaa kimama hao, hususani boti zenye mashine kwaajili ya kuvukia na shughuli zao za baharini pamoja na viatu kwa usalama wanapokua baharini” Alifafanua Mama Mariam.

Mama Mariam ambae pia ni Mlezi wa Matembezi ya UVCCM ya Mapinduzi ya Zanzibar aliwaeleza vijana hao kwamba pia ZMBF imejita kwenye harakati za utunzaji mazingira kwa kuishajihisha jamii kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuimarisha usafi.

Alisema katika harakati hizo, ZMBF inajishughulisha na utengenezaji wa taulo za kike za kufua na kuhifadhi baada ya matumizi, ambazo huwasaidia wasichana mashuleni hasa wale wanaotoka kwenye mazingira magumu ambao hawana uwezo wa kuhimili taulo za kawaida.

Aidha, alieleza taulo za kawaida ambazo hutupwa baada ya matumizi huchangia wimbi la uchafuzi wa mazingira na kueleza kwama nyingi husalia kutupwa baharini na kuathiri viumbe vya bahari.

Akizungumzia tatizo la magojwa yasiyoambukiza yanayoendelea kuiathiri jamii, Mama Mariam Mwinyi alieleza ZMBF imekua ikishajihisha jamii kufanya mazoezi na kuambatana nao kwenye makongamano mbalimbali yanayohusisha matembezi ya hiari ambayo husaidia jamii kufanya mazoezi ili kujiepusha na kujinginga na maradhi hayo yakiwemo, presha, kisukari matatizo ya moyo na saratani.

Kuhusu suala la udhalilishaji wa kijinsia, alieleza ZMBF inakerwa zaidi na vitendo hivyo ambavyo huwaathiri zaidi wanawake na Watoto, alisema licha ya harakati nyingi zinazofanya na taasisi hiyo kwa kuwagusa moja kwa moja kinamama, vijana, wasichana na Watoto suala la udhalilishaji wamekua wakilikemea kwa nguvu zote na kulipiga vita.

Katika hatua nyengine Mlezi huyo wa UVCCM aligusia matayarisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuwataka vijana hao kufanya maandalizi ya aina yake kwani vijana ni sauti ya Chama hasa kwenye kuimarisha mustakabali wa maendeleo na mabadiliko kwenye nyanja zote za siasa, uchumi na jamii.

“Kuna haja ya kukaa chini na kufikiria namna kutakavyoadhimisha miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar yawe ya aina yake, muje na fikra tofauti, UVCCM ije na kitu tofauti sababu vijana ndio injini ya Chama” aliwashajihisha vijana hao.

Naye, Makamu Mwenyekiti UVCCM taifa, Ndg. Rehema Sombi Omari (MNEC) kwa niaba ya ugeni alioambatana nao, waliipongeza ZMBF kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa kwa kipindi cha muda mfupi pia waliahidi kuwa balozi wazuri wa kukitangaza Chama na kupaza sauti zao kwa umma kuyasemea mazuri yote yanayofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Dk. Mwinyi na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi imara wa Dk. Samia Suluhu Hassan.

Akilizungumzia jengo la UVCCM, ofisi ya Jimkana, Zanzibar alisema wanatarajia kulifanyia maboresho makubwa ili kueka alama kwa vizazi vijavyo kwamba UVCCM 2022 – 2077 ilifanya makubwa wakati wake. 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.