Habari za Punde

Mama Maryam Mwinyi arejea Zanzibar



Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mhe. Mama Mariam Mwinyi ameagwa rasmi na mwenyeji wake Mke wa Rais wa Burundi Mhe.Mama Angeline Ndaishimiye baada ya kukamilisha ziara yake ya siku 3 ya kushiriki Mkutano wa viongozi Wanawake uliofanyika Burundi.
Mama Mariam amerejea Zanzibar leo tarehe 12 Oktoba 2023.
Aliagwa na Balozi wa Tanzania Nchini Burundi Mhe.Gelasius Gaspar Byakanwa.
Mke wa Rais wa Zanzibar,  Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF)Mhe. Mama Mariam Mwinyi amefanya Ziara kutembelea  benki ya CRDB  tawi la Burundi, Bujumbura.

Katika nasaha zake Mhe. Mama Mariam   ametoa wito kwa Uongozi na
Wafanyakazi wa Benki hiyo kuendelea kufanyakazi vizuri zaidi kama
viashiria vinavyoonesha ufanisi mkubwa mbele yao ili waweze kufungua
fursa zaidi kwa wawekezaji kuwekeza katika sekta ya uchumi na fedha kwa
maslahi ya pande zote mbili.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB tawi la Burundi amesema crdb tawi la Bujumbura wanaaendelea kufanya kazi vizuri na wanaendelea kufanya kazi ya kuutangaza mwana Pamoja na kuendelea kutoa mashirikiano na Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF).
Wakati huo huo Mhe. Mama Mariam Mwinyi amefanya Ziara kutembelea  Ofisi ya Mke wa Rais wa Burundi na Mwenyekiti wa Taasisi inayoshugulikia  Maendeleo Nchini Burundi; Mama Angeline Ndaishimiye iliopo Bujumbura, Alishiriki zoezi la upandaji mti  kuashiria umoja na mashirikiano yao wakiwa viongozi  wanawake ndani ya Nchi za Bara la Africa.

Katika zoezi hilo alishiriki pia Muwakilishi wa Shirika la Maendeleo ya wanawake  UN WOMEN kikanda - Afrika Ms. Awa Ndiaye Seck.

IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.