Habari za Punde

Alhaj Dk. Mwinyi amewanasihi Vijana kuwathamini wazazi wao na kuwatendea mema ili kupata baraka za Mwenyezi Mungu.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mtoto Hassan Saleh alipowasili katika Msikiti wa Maungani kwa Hafidh Ali Wilaya ya Magharibi “B” Unguja, kujumuika na Waumini wa Dini ya Kiislam katika Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika leo 15-11-2024 katika msikiti huo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Waumini wa Dini ya Kiislam, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika leo 15-11-2024 katika Msikiti wa Ijumaa Maungani kwa Hafidh Ali, Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika kuitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kabi (kulia kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika leo 15-11-2024, Msikiti wa Ijumaa Maungani kwa Hafidh Ali Wilaya ya Magharibi “B” Unguja, na (kushoto kwa Rais) Imamu Mkuu Sheikh. Suleiman Mwinyichum Suleiman.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wananchi, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Maungani kwa Hafidh Ali Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 15-11-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wananchi, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Maungani kwa Hafidh Ali Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 15-11-2024.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na Waumini wa dini ya Kiislamu katika ibada ya sala ya Ijumaa Msikiti wa Maungani, Wilaya ya Magharibi B.

Akitoa salamu kwa Waumini, Alhaj Dk. Mwinyi amewanasihi Vijana kuwathamini wazazi wao na kuwatendea mema ili kupata baraka za Mwenyezi Mungu.

Alhaj Dk. Mwinyi amefahamisha ni wajibu na ni jambo jema  kwa vijana ambao wazazi wao wako hai  kuishi nao kwa huruma na upendo na kuwaombea dua wale waliotangulia mbele ya haki kwani kuna fadhila nyingi kwa kutekeleza jambo hilo.

Akitoa hotuba ya Ijumaa Khatibu wa Msikiti wa Ijumaa wa Maungani, Sheikh Suleiman Mwinchumu Suleiman amewasisitiza Waumini hao kuwa karibu na wazazi wao pamoja na kuzungumza nao kwa maneno mazuri na kuacha hasira juu yao kama ilivyoamrishwa na miongozo ya dini ya kiislamu.

Katibu Mtendaji wa Afisi ya Mufti, Sheikh Khalid Ali Mfaume amesema ni vyema kwa Waumini wa kiislamu kufahamu du'a ya kuwaombea wazee na kuitekeleza kila wanapopata fursa ya kufanya hivyo, Ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu.

Wakati huohuo, Alhaj Dk. Mwinyi baada ya sala ya Ijumaa aliendeleza utaratibu wake wa kuwatembelea Wananchi na kuwajulia hali Wagonjwa katika maeneo mbalimbali.

Aliowatembelea leo ni aliekuwa Mbunge na Naibu Waziri Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mshauri wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi wa Awamu ya Saba, Dk. Maua Abeid Daftari anaeishi Beit Ras Wilaya ya Magharibi A.

Msanii Mkongwe wa sanaa za Filamu na Maigizo Zanzibar Bibi Mwanamwema Khamis Juma, maarufu Bi Njiwa.

Mwengine ni Bi. Halima Muhamed, Mjane wa aliekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Kichama, Marehemu Borafya Silima wanaoishi Mwera Mtofaani.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.