Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita akizungumza na Waumini wa Dini ya Kikiristo mara baada ya kukabidhi msaada wa vyakula Mbali Mbali na fedha taslim katika Kanisa la Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu, Mpendae. Wilaya ya Mjini.
Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita ametoa Sadaka ya Vyakula mbali mbali na pesa Taslim kwa waumini ya Dini ya Kikiristo ili kuwasaidia katika Skukuu ya Pasaka .
Akitoa Sadaka hiyo Katika Kanisa la
Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu , Mpendae, Wilaya ya Mjini amesema Serikali inawathamini na kuwapenda waumini wa Dini zote hivyo ni vyema kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum ikiwemo watoto yatima na wajane ili waweze kufurahia sikukuu
Aidha amesema ipo haja ya Mashirika na Watu wenye uwezo kuwasaidia waumini hao kutokana kuwa wengine wanaishi Katika mazingita magumu jambo ambalo litawasaidia kujikwamua kimaisha
Waziri Tabia alisema ataendelea kushirikiana na waumini hao kwa kuwapatia misaada mbalimbali ili waweze kuendesha shughuli zao.
Baadhi ya Masister na Waumini mbali mbali wa Dini ya Kikiristo wakimsikiliza Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita (hayupo pichani) katika Kanisa la Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu, Mpendae. Wilaya ya Mjini.
Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita (wa pili kushoto) akikabidhi fedha taslim kwa Paroko Padre Antony Kantu (wa kwanza kushoto) na Waumini wa Dini ya kikiristo katika Kanisa la Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu, Mpendae. Wilaya ya Mjini.
Diwani wa Viti Maalum Wilaya ya Mjini Asteria Moris Ambros akitoa shukrani kwa Viongozi Wakuu kwa kuonesha mashirikiano yao huko katika Kanisa la Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu, Mpendae. Wilaya ya Mjini.
Baadhi ya Masister na Waumini mbali mbali wa Dini ya Kikiristo wakimsikiliza Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita (hayupo pichani) katika Kanisa la Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu, Mpendae. Wilaya ya Mjini.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Amani Kichama Fransisca Camilius Clement akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita katika Kanisa la Parokia ya MT Mikaeli Malaika Mkuu, Mpendae. Wilaya ya Mjini.
Amesema anaamini kwamba Serikali haina Dini,Ukanda Wala ukabila hivyo ni vyema kuwasaidia watu wa makundi Mbali Mbali ya mahitaji ikiwemo watoto yatima na wajane .
Kwa Upande wa Diwani wa Viti Maalum Wilaya ya Mjini Asteria Moris Ambros amemshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk Hussein Mwinyi kupitia Waziri Tabia Kwa kutoa Sikukuu katika Kanisa la Mtakatifu Mikaeli ili kusherehekea vizuri Pasaka .
Akizungumza Kwa niaba ya Wajane na watu wenye mahitaji Maalum Mkuu wa Kanisa,Paroko Padre Antony Kantu amesema wamefarijika Kwa msaada huo na kuwaombea wazidishe juhudi kuendeleza kuwasaidia.
No comments:
Post a Comment