Mdau katika matembezi yangu ya hapa na pale mitaani ili kutafuta matukio kwa ajili ya jamii sehemu za mitaa ya uswahili, nilikutana na kijana huyu akiwa katika mchezo na kuku wake aina ya jogoo likiwa na afya njema mashaaAllah.
Ilibidi nisimame na kujuwa kulikoni mambo haya ya Mtu kucheza na kuku na kuku huyu kufuata amri ya mfugaji wake kijana Khalid Abdalla, na kufahamu jina lake na kulijua anapoitwa Chicken huja mbio na kucheza nae, ilibidi kumuuliza kulikoni mambo haya, na kueleza haya mafunzo nimemfunza sasa karibu miaka miwili sasa.
hapa nimeona show ambayo sikufikiria baada ya muda Khalid atakuwa msanii.
ReplyDeleteDuuu hii kali mdau si bora awe anafanya show kama vile Chicken George
ReplyDeleteKabla hujapost tafadhali ufanye review, makosa mengi ya spelling.
ReplyDeleteKuna habari muhimu kwa ZNZ wiki nzima sasa, kuna wanahabari from Dar na kwengine wanafuatilia kwa ukaribu. Kwako wewe sio issue! Then unapita mitaani kwa story za jogoo.
Wadau majority ni wa nje ya nchi, wanapenda kujua mambo muhimu ya nyumbani.
Badilika tafadhali.