TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amemteuwa Dk. Ahmada Hamad Khatib kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kamisheni ya Utalii, Zanzibar.
Kabla ya uteuzi huo Issa Ahmed Othman ndie aliekuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambapo sasa amekuwa Mshauri wa Rais wa mambo ya Utalii.
Rais amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 5(1)(a) cha Sheria ya Kamisheni ya Utalii Namba 7ya 2012
Taarifa iliotolewa na Kaimu Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Salum Maulid Salum imezidi kueleza kuwa Rais pia amemteuwa Shafi Mussa Haji kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Umeme, Zanzibar.
Kabla ya uteuzi huo Mohamed Hashim Ismail ndie aliekuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo.
DKT Shein amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 6(1)(a) cha Sheria ya Shirika la Umeme la Zanzibar.
Uteuzi huo unaanza leo tarehe 5/9/2012
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
5/9/2012
Ufungaji wa Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Chumbuni Zanzibar
Viwanja vya Avenja
-
Shamrashamra za ufungaji wa mkutano ya Kampeni wa Chama Cha Mapiduzi (CCM)
za Ubunge,Uwakilishi na Udiwani Jimbo la Chumbuni Zanzibar , kwa onesho la
Uta...
7 hours ago

No comments:
Post a Comment