Joseph
Ngilisho,Arusha
BIBI
kizee mwenye umri wa miaka 85,Elishusa Zakaria mkazi wa kijiji
cha
Mfuloni,kata ya Ndohombo wilaya ya Arumeru,mkoani Arusha,amefariki duni kwa
moto nyumbani kwake, akiwa usingizini.
Tukio
hilo
limefahamika mara baada ya kugundulika mwili wa marehemu, jana majira ya saa 5:30
asubuhi baada ya mjukuu wake aliyefahamika kwa jina la Janeth Peterson(16)alipoenda
nyumbani kwa
bibi
yake kumtembelea.
Akizungumzia
tukio hilo,Kamanda
wa polisi mkoa wa Arusha,Liberatus
Sabas
alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza
kuwa chanzo cha tukio hilo
ni kibatali kilichokuwa kikiwaka na baadae kuripuka na moto kusambaa kwenye godoro
alililokuwa amelalia.
“Katika
nyumba hiyo yenye vyumba vitatu marehemu alikuwa amelala
kwenye
chumba kimojawapo na inaonyesha hapa kuwa na mtu mwingine anayeishi naye,”alisema
Kamanda huyo.
Aidha
mbali na kifo cha marehemu, baadhi ya vitu vilivyoko ndani ya
chumba
hicho vikiwemo vyakula,vyombo, kitanda na godoro
viliungua
,huku thamani yake bado haijafahamika ambapo polisi
wanaendelea
na uchunguzi wa tukio hilo.
Mwili
wa marehemu umezikwa baada ya kufanyiwa uchunguzi na daktari na
kuukabidhi
kwa ndugu wa merehemu.
Wakati
huo huo,mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Laray mwenye umri wa miaka 25
mfanyakazi wa kampuni ya ujenzi iitwayo Shereji Construction amefariki dunia baada ya gari alilokuwa akisafiria
kuacha
njia na kupinduka.
Kamanda
wa polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas alisema tukio hilo
lilitokea
Febuari 20 mwaka huu majira ya saa 1:15 jioni katika eneo la chuo kikuu cha
Nelson Mandela wilayani Arumeru.
Alisema
siku ya tukio gari aina ya Toyota Hilux
lenye namba za
usajili
T 732 AEF lililokuwa linaendeshwa na Rajkumar Sharma (24) mkazi wa Kijenge
lilipinduka na kusababisha kifo cha mtu huyo.
Sabas
alisema,ajali hiyo ilitokea wakati gari hilo
likiwa linatokea maeneo ya Usa
river kuelekea mjini na ilipofika karibu na lango kuu la chuo hicho lilianguka
na kusababisha kifo cha abiria
huyo
baada ya kuegemewa na gari hilo.
Aidha
chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana na jeshi la polisi
mkoani
hapa linaendelea na uchunguzi zaidi ili
kujua chanzo halisi na dereva huyo anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakani
pindi upelelezi utakapokamilika.
No comments:
Post a Comment