Na Masanja Mabula,Pemba
WATU wanaosadikiwa
kuwa majambazi usiku wa kuamkia Jumapili wamevamia nyumbani kwa Juma Haji Kombo (Malengo) mkaazi
wa shehia ya Mzambarautakao wilaya ya Wete na kufanikiwa kupora shilingi
milioni 2.5 pamoja vitu vya dhabhabu na simu nne za mkononi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kaimu Kamanda wa polisi
Mkoa wa Kaskazini Pemba, Juma Sadi alisema katika tukio hilo majambazi hao
walikuwa ni wanane na mara baada ya kutekeleza tukio hilo walikimbia katika
mabonde ya msitu wa Matuuni Mtambwe.
Alisema tukio hilo limetokea usiku wa saa 2 :10
ambapo walipoingia ndani walimlazimisha kutoa pesa huku wakitishia kumuua
ambapo aliwakabidhi fedha kwa hofu ya
usalama wa maisha yake.
Kamanda Sadi amefahamisha jeshi la polisi mkoa huo
lilipata taarifa ya kuwepo na tendo la uhalifu katika shehia ya Mzambarautakao,
hata hivyo hawakuweza kufanikiwa kuwakamata majambazi hao.
Naye
Naibu sheha wa Shehia hiyo, Mwanajuma Mohammed akizungumza na mwandishi wa
habari hizi ameitaka jamii kuimarisha
mpango wa ulinzi wa polisi jamii ili kuweza kusaidia kudhibiti matendo kama hayo.
Alisema
kwamba kuwepo kwa ulinzi shirikishi ndio
njia pekee ya kuweza kuwabana wahalifu kwani itakuwa ni rahisi kufichua
maficho ya wanaojighusisha na vitendo hivyo .
Tukio
hilo ni la pili kutokea katika Wilaya ya Wete katika kipindi cha mwaka huu,
ambapo tukio kama hilo
lilitokea wiki mbili zilizopita kwa
Afisa Mdhamini Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano Pemba kuvamiwa na
majambazi akiwa nyumbani kwake Kifumbikai.
No comments:
Post a Comment