Na
Husna Mohammed
BODI ya
Mapato Zanzibar (ZRB), imekusanya shilingi bilioni 67.642 sawa na asilimia 82.65 kuanzia mwezi
Julai hadi Disemba 2012 ikiwa ni makusanyo halisi kwa kipindi hicho.
Awali
bodi hiyo ililenga kukusanya shilingi bilioni 81.846 katika kipindi hicho
lakini ilishindwa kufikia makusanyo hayo kutokana na sababu mbalimbali.
Akizungumza
na Zanzibar Leo ofisini kwake Mazizini, Kaimu Meneja, Idara ya Usajili na
Huduma kwa Walipakodi, Safia Is-hak, alizitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na
kupungua kwa idadi ya watalii waliotembelea Zanzibar kutokana na matatizo ya kifedha
yaliyoikumba dunia.
Sababu
nyengine ni pamoja na kutokusambazwa kwa bidhaa ya mafuta ya nishati katika
kiwango kinachokidhi mahitaji jambo ambalo linapelekea kushamiri kwa biashara
ya magendo ya mafuta ya nishati.
Sambamba
na hayo,alisema sababu ya kutokuanza kukusanywa kwa mapato kutoka katika baadhi
ya vianzio vya mapato ya mawizara ni mambo yaliopelekea kutofikia makusanyo
yaliyotakiwa.
Hata
hivyo,alisema licha ya kutofikia lengo
la makusanyo lililolengwa lakini kwa kipindi hicho cha makusanyo kilionekana
kukua ukilinganisha na miezi kama hiyo katika kipindi cha mwaka 2011/2012
ambapo ZRB ilikadiria kukusanya shilingi
59.9 bilioni na kukusanya shilingi 59.6 bilioni sawa na asilimia 99.4
ambapo ni ongezeko la mapato la shilingi
bilioni 8 sawa na asilimia 13.5.
Safia
alisema ili kuona kwamba bodi ya mapato inakusanya mapato kama
ilivyokusuidiwa ni lazima kuwepo kwa mashirikiano makubwa kati ya wananchi hasa
katika suala zima la kudai risiti wakati wa kununua bidhaa mbalimbali.
No comments:
Post a Comment