Timu ya Daraja la pili ya Mwembeladu mjini Unguja inaendelea vizuri katika mashindano ya nane bora kutafuta timu mbili zitakazopanda daraja baada ya kupata ushindi wa pili mfululizo.
Mechi ya kwanza waliwafunga Majirani wao Timu ya Kundemba 2-0 na jana usiku waliweza kuwafunga timu ya Vikokotoni 3-0.
Hongera Kocha Masoud Chile kwa ushindi wapili mfululizo katika nanebora ligi daraja la pili Zanzibar ambapo timu ilionesha kandanda safi la kutoka kitabuni lililofundishwa na Kocha Chile.
No comments:
Post a Comment