Habari za Punde

Balozi Seif apiga kura Kitope

 Mgombea nafasi ya Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa Tiketi ya CCM Jimbo la Mahonda ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika foleni ya kusubiri kupiga kura kwenye Kituo chake kiliopo Skuli ya sekondari ya Kitope.
 Balozi Seif akipiga kura ya Kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Bunge ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Kituo chake hapo Skuli ya Sekondari ya Kitope.
 Karani wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ambae jina lake halikupatikana akimueka alama Balozi Seif kuashiria kwamba ameshakamilisha zoezi la Kupiga kura ya kumchagua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, Mbunge, Mwakilishi na Diwani.

Balozi Seif akizungumza na vyombo vya Habari mara tuu bada ya kumaliza kutumia haki yake ya kupiga kura hapo Skuli ya Sekondari ya Kitope ambapo ndio kwenye kituo chake cha uchaguzi.

Picha na –OMPR – ZNZ.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.