TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
|
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya
uteuzi wa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:
1.
UTEUZI WA WAKUU
WA MIKOA
Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 61(1)
cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed
Shein amefanya uteuzi wa Wakuu wa Mikoa kama ifuatavyo:
i.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini na Magharibi –
Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahmoud
ii.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, Unguja –
Mheshimiwa Vuai Mwinyi Mohamed
Aidha Wakuu wa Mikoa ambao
Mikoa yao haikutajwa katika taarifa hii
wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Uteuzi
huo umeanza leo tarehe 23 Mei 2016.
2.
UTEUZI WA WAKUU
WA WILAYA
Kwa
mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 61(2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka
1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya
uteuzi wa Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:
i. Mkuu wa Wilaya ya Mjini – Mheshimiwa
Marina Joel Thomas.
ii. Mkuu wa Wilaya ya Magharibi “B” – Mheshimiwa
Silima Haji Haji
iii. Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “A”– Mheshimiwa
Hassan Ali Kombo
iv. Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “B” –
Mheshimiwa Issa Juma Ali
v. Mkuu wa Wilaya ya Kati – Mheshimiwa Mashavu Sukwa Said
vi. Mkuu wa Wilaya ya Kusini – Mheshimiwa
Idrissa Kitwana Mustafa
vii. Mkuu wa Wilaya ya Chakechake –
Mheshimiwa Salama Mbarouk Khatib
Aidha
Wakuu wa Wilaya ambao Wilaya zao hazikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Uteuzi
huo umeanza leo tarehe 23 Mei 2016.
Viongozi
wote waliotajwa wanatakiwa waripoti Ikulu, Mjini – Unguja, siku ya Jumanne tarehe
24 Mei 2016 saa 8 za mchana tayari kwa kuapishwa.
(DKT.
ABDULHAMID Y. MZEE)
KATIBU WA BARAZA LA MAPINDUZI
NA
KATIBU MKUU KIONGOZI,
ZANZIBAR.
23
MEI, 2016
No comments:
Post a Comment