Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akimsikiliza mgeni wake Mwakilishi wa UNFPA Nchini Tanzania Ms.Jacqueline Mahon wakati wa mazungumzo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kwa ajili ya kumsalimia Rais
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dk. Ali Mohamed Shein, alifanya
mazungumzo na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu
Duniani (UNFPA) Bibi Jacqueline Mahol aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili
ya kuzungumza na Rais.
Katika maelezo yake Rais
Dk. Shein alilipongeza Shirika hilo la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu
Duniani (UNFPA), kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuhakikisha huduma
za jamii zinaimarika zikiwemo huduma za afya.
Katika maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa Shirika
la UNFPA limekuwa na uhusiano na ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kwa muda mrefu na tokea wakati huo limekuwa likifanya juhudi katika kusaidia
miradi mbali mbali ya maendeleo.
Alieleza kuwa juhudi kubwa zimechukuliwa na
mafanikio yanaonekana katika kupunguza vifo vya akina mama na watoto kwa
mashirikiano ya pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika
wa maendeleo likiwemo Shirika hilo la UNFPA.
Nae Mwakilishi
huyo wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Bibi
Jacqueline Mohan alitoa pongezi kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya
uongozi wa Dk. Shein katika kuimarisha miradi ya maendeleo pamoja na kuwapatia
huduma wanawake na watoto.
Mwakilishi huyo aliahidi
kuwa Shirika lake litaendelea kuziunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar za kupambana na umasikini, kuwaletea maendeleo wananchi wake sambamba
na kutekeleza Malengo na Mikakati yake iliyoiweka kwenye MKUZA III.
Katika maelezo yake,
Mwakilishi huyo alitumia fursa hiyo kuipongeza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kwa kufanikisha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC) pamoja na kupelekea lugha ya Kiswahili kupitishwa kwua lugha rasmi ya nne
itakayotumika katika Jumuiya hiyo.
Aidha, Mwakilishi huyo
alitumia fursa hiyo kutoka pole kwa ajali ya gari la mafuta iliyotokea hivi
karibuni huko Morogoro na kusabisha vifo pamoja na majeruhi kadhaa.
Pia, kiongozi huyo
alipongeza juhudi za Zanzibar katika kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2020
sambamba na mafanikio makubwa yaliopatikana katika usajili wa vizazi kwa
asilimi 71 na kueleza kwua (UNFPA), inajivunia mafanikio hayo yaliopatikana
hapa Zanzibar.
Hivyo, Shirika hilo
limmeahidi kuendelea kuiunga mkono Zanzibar na kutoa misaada yake zaidi kwa
kuendeleza miradi mbali mbali ambapo pia, Shirika hilo limeahidi kutoa msaada
wa gari za mbili za kubebea wagonjwa (ambulances).
Pia, Shirika hilo
limeeleza azma yake ya kuanzisha kampeni juu ya kukinga vifo vya watoto
wachanga na wazazi na kuahidi kuzidisha mashirikiano katika sekta mbali mbali
za maendeleo na huduma za kijamii ikiwemo sekta ya afya, elimu na nyenginezo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment