Habari za Punde

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Jeshi la Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan Aongoza Viongozi Mbalimbaliu katika Uwekaji wa Mashada ya Maua Katika Kaburi la Hayati Dkt. John [Pombe Magufuli Chato.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiweka Shada la Maua kwenye Kaburi la aliyekuwa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Mazishi yake yaliyofanyika leo March 26,2021 katika Makaburi ya Familia Kijijini kwake Chato Kilimani Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitia Udongo kwenye Kaburi wakati wa Mazishi ya aliyekuwa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Hayati Dkt. John Pombe Magufuli yaliyofanyika leo March 26,2021 katika Makaburi ya Familia Kijijini kwake Chato Kilimani Mkoani Geita.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.Mhe Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua katika kaburi la Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania yaliofanyika Kijiji kwao Chato Mkoa wa Geita leo 26-3-2021. 
Mjane wa Hayati Dkt.John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiweka shada la maua katika kaburi la marehemu wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijijini kwao Chato Mkoani Geita leo.
Watoto wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wakiweka Shada la Maua katika kaburi la baba yao wakati wa maziko yaliofanyika Kijiji kao Chato Mkoa wa Geita leo.  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiweka Shada la Maua katika kaburi la Hayati Dkt.John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yaliofanyika Kijiji kwao Chato Mkoa wa Geita.  
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akiwa na Mkewe Mama Mary Majaliwa wakiweka Shada la Maua katika kaburi la Hayati Dkt.John Pombe Magufuli yaliofanyika leo Kijijini Kwao Chato Mkoa wa Geita.
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akiwa na Mkewe Mama Mary Majaliwa wakitowa heshima za mwisho katika kaburi la Hayati Dkt.John Pombe Magufuli yaliofanyika leo Kijijini Kwao Chato Mkoa wa Geita. baada ya kuweka shada la maua.
Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai akiwa na Mkewe wakiweka shada la maua katika kaburi la Hayati Dkt.John Pombe Magufuli aliyekiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yaliofanyika kijijini kwao Chato Mkoani Geita leo. 
Rais Mstaaf wa Tanzania Awamu ya Pili Mhe.Ali Hassan Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Siti Mwinyi  wakiwa shada la maua katika kaburi la Hayati Dkt.John Pombe Magufuli yaliofanyika Kijijini Kwao Chato Mkoani Geita  yaliofanyika leo. 
Rais Mstaaf wa Awamu ya Nne Tanzania Mhe.Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa shada la maua katika kaburi la Hayati Dkt.John Pombe Magufuli yaliofanyika Kijijini Kwao Chato Mkoani Geita  yaliofanyika leo.







 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.