Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi amtumia salamu Rais wa Tanzania Mhe Samia katika siku yake ya kuzaliwa


 

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

Zanzibar                                                                    27.01.2022

---

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amemtakia  kila la heri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika siku yake ya kuzaliwa hivi leo.

 

Katika salamu hizo, Rais Dk. Mwinyi amemuombea kwa MwenyeziMungu Mama Samia Suluhu Hassan kuwa na maisha marefu na yenye afya njema ili azidi kuendelea kuijenga Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na watu wake wote, ambapo haya ni maadhimisho yake ya kwanza ya siku ya kuzaliwa tokea ashike madaraka ya kuiongoza nchi.

 

Imetayarishwa na Kitengo cha Habari,

Ikulu Zanzibar

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.