Habari za Punde

Mhe Othman ahimiza uwajibikaji na uadilifu

 


Mkoa wa Kusini Pemba

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT- Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman, amesema uwajibikaji na uadilifu kwa viongozi ni njia sahihi inbavyosaidia Viongozi kutimiza vilivyo matarajio na matumani ya wananchi  katika kukuza maendeleo ya nchi kuichumi na kijamii.

Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ameyasema hayo huko Viwanja vya Tibirinzi Chake Chake Pemba alipozungunza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho ikiwa ni muendelezo wa kutangaza ahadi za Chama hicho kwa wananchi.

Mhe Othman amefahamisha kwamba nchi yoyotoe haiwezi kupiga hatua ya kimaendeleo iwapo viongozi wake hawatoweka mbele  suala la masalahi ya wananchi sambamba na kuzingatia  udilifu katika kuwahudumia wananchi na shughuli za uendeshaji wa nchi na kwamba chama  cha ACT wazalendo kinaswasilia kwa wananchi maono ya mabadiliko ya kimaendeleo katika kipindi cha miaka kumi ijayo.

Amewataka wananchi kuungana pamoja katika kuujenga Zanzibar mpya , yenye umoja  na mamkala kamili itakauoweza kutumia rasilimali zake mbali mbali ikwemo uwezo wa usarifu na upangaji wa kodi mbali mbali katika kuongeza mapato ya wananchi na kukuza jitihada za kimaendeleo.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba katika uendeshaji wa nchi   kunahitajika  viongozi kwa wazalendo wenye kutumia maarifa na uwezo wao ipasavyo wa kuwatumikia wananchi kutimiza malengo mbali mbali wanayojiwekea .

Amesema kwamba hatua hiyo pia ni muhimu katika kujenga amani  kweli nchini  inayotokana na kuwepo matumaini  makubwa ya imani kwa viongozi  katika kuleta mabadiliko yanayotokana na uwezo wa ndani wa rasilimali zilizopo  bila kuwepo  vipingamizi vya namna yoyote.

Amefahamisha wananchi ni vyema wakaunga mkono jitahada za viongozi wa ACT- Wazalendo kwa kuwa viongozi wanaelekeza maono yao katika kupiga hatua za maendeleo kama zilivyofanya nchi nyengene  mbali mbali ambazo mazingara yao ya kijiographia na uchumi yanafanana na Zanzibar.

Naye Mwenyekiti wa Chama hicho Babu Juma Dunia Haji amewataka wananchi wa Zanzibar kuungana ili kuendana na maono na mipango ya fikra za viongozi wa Chama hicho za kuleta mabadiliko ya kisera na uwajiabikaji  utakaosaidia kiuchumi na  na maendeleo bora ya Zanzibar.

Amefahjamisha kwamba viongozi waote wa chama hicho wanasimama  kutetea maslahi ya Zanzibar ikiwemo umoja haki na maridhiano ya kweli ambayo ndio chachu ya kuleta na kudumisha Amani ya kweli katika nchi yoyote duniani.

Naye Katibu Mkuu wa Chama hicho Ado sahib Ado, amesema katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 chama hicho kinahitaji kuwepo katiba Mpya, Mabadiliko katika sheria ya Uchaguzi  kwa kuwa ndio mamabo yanayoweza kuleta haki.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho Ismail Jussa Ladhu amewataka wananchi wa Zanzibar kutokata tamaa  na waendelee kujenga mshikamano na umoja katika kujenga chama hicho ili juhudi za pamoja zitumike kuweza kuleta maendeleo ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.