Habari za Punde

Baraza la Mji Kati Unguja Wapanga Mikakati ya Maendeleo Katika Wilaya Hiyo

Na Fauzia Mussa, Maelezo.

Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Wilaya ya kati Unguja Ndg.Said Hassan Shaaban amesema baraza la mji kati limepanga mikakati mbalimbali ya  kuwaletea maendeleo wananchi wa Wilaya hiyo.

Ameyasema  hayo katika kikao cha madiwani wa wilaya hiyo 

kilichofanyika Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na  ujenzi 

wa vituo vya daladala ambapo tayari  vituo kumi 

vimeshajengwa na vipo katika hatua ya mwisho ili kuanza 

kutumika.


Aidha  ameeleza kuwa Baraza hilo limejipanga kuiendeleza 

miradi ya masoko iliyojengwa katika Wilaya hiyo  pamoja na 

bustani zinazotarajiwa  kutengenezwa  katika maeneo ya 

Hanyegwamchana  na Tunguu.


Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa baraza la mji kati, 

mkuu wa idara ya rasilimali watu, mipango, utawala na 

mtumzaji kumbu kumbu  Rehema Khamis Hassan amesema 

watahakikisha kuwa  wafanyakazi wa baraza hilo 

wanatekeleza majukumu yao ipasavyo ili kufikia malengo 

yaliokusudiwa.


Aidha amesema watahakikisha  ofisi ya baraza la mji kati 

inatekeleza miradi yote ya kimkakati ambayo imewekwa 

sambamba na uimarishaji wa miji katika robo ya mwaka 

inayomalizia  2024_2025.

kikao hicho ni cha tatu Kufanyika katika Baraza la tano la  

madiwani ndani ya Wilaya hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.