Ofisa michezo kutoka idara ya michezo chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Saleh Hashim, akizungumza wakati akizindua ligi ya mchezo ya kabaddi muhula wa kwanza katika viwanja vya New Amaan Compex. (Picha na Mpiga Picha Wetu).
NA FAUZIA MUSSA
Katika kuadhimisha miaka minne ya Dk.
Mwinyi, shirikisho la kabadi Zanzibar limeandaa ligi ya mchezo huo msimu wa
kwanza ambapo kufanyika kwa mashindano hayo kutasaidia kuutangaza mchezo huo ndani
ya jamii.
Hayo yameelezwa na ofisa michezo
kutoka idara ya michezo chini ya Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Saleh Hashim wakati akizindua mashindano
hayo yatakayodumu kwa siku tano katika viwanja vya New Amaani Compex.
Alisema uzowefu unaonesha kuwa mchezo huo bado
ni mgeni kwa jamii hivyo aliwaomba vijana kujifunza kupitia mashindano hayo.
Alieleza kuwa Wizara inafarajika kuona
michezo mbalimbali inaongezeka hali
inayosaidia kuitangaza nchi na kusema kuwa wizara itaendelea kuchukua juhudi za
makusudi kuhakikisha mchezo huo unatambulika na kuendelezwa.
Alifahamisha kuwa hatua hiyo pia inaonesha
wazi maendeleo ya mchezo huo ulioanzishwa miaka miwili iliyopita, na kuwaomba
wadau wa michezo kuongeza nguvu katika mchezo huo ili kuupa thamani na kuutambulisha kwa watu.
Mkurugenzi
wa maendeleo ya michezo wa
shirikisho la chama cha kabadi Zanzibar,
Abdalla Juma Abeid na Makamu Mwenyekiti wa mchezo huo,
Ali Seif Juma, walisema historia inaandikwa kwa kuzindua mashindano hayo
kwani haijawahi kufanyika tangu kuanza kuchezwa kwa mchezo huo visiwani
Zanzibar.
Walieleza kuwa kuimarika na kuongezeka
kwa michezo kunaenda sambamba na juhudi za Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza La Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi
za kuwekeza katika sekta ya michezo, na kusema kuwa ligi hiyo ni maalum
kwaajili ya kumpongeza kiongozi huyo kwa mageuzia makubwa aliyoyafanya katika
sekta ya michezo.
Walifahamisha kuwa timu 12 zitashiriki
katika michuano ya mchezo huo zikiwemo timu nne za wanawake ambapo mara baada
ya ufunguzi timu ya KMKM wanawake watachuana
na Lumumba wanawake, na kwa upande wa wanaume timu ya KMKM na Lumumba
zitapimana nguvu.
Viongozi hao walilishukuru Baraza la
michezo kupitia Wizara ya Habari kwa msaada wao uliyofanikisha michuano hiyo
Kufanyika katika viwanja hivyo na kusema kwao ni fursa ya kuutangaza.
Naifat Ame Hassan na Samir Mubarak Sururu
wa timu ya kabadi KMKM walisema
wanatarajia kupata ubingwa katika ligi hiyo kwani suala hilo sio geni kwao na
wameshafanikiwa katika michezo mingi iliyopita na kupata vikombe.
Aidha wachezaji hao waliahidi
kutomwangusha Dk. Mwinyi kwa kuiwakilisha vyema nchi wanaposhiriki mchezo huo ndani na nje ya nchi.
Adam Makame Hamad na Sina Mussa wa timu ya
kabadi Lumumba walimshukuru Rais wa
Zanziba na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa mchango wake unaosaidia kuitambulisha
michezo mbalimbali ikiwemo kabadi na kuwashauri vijana kujiunga na mchezo huo
kwani utawasiadia kuwatoa kimaisha, na kuimarisha afya zao.
Watazamaji wa michuano hiyo akiwemo Ahlam Khamis walionesha kufurahishwa
na mchezo huo na kusema kuwa wanatamani kujiunga.
Michuano hiyo inakwenda sambamba na kauli mbiu " miaka minne ya Dk. Hussein kabadi inajieleza"
No comments:
Post a Comment