Na Laylat Khalfan
VIONGOZI wa dini Zanzibar,
wameelezea wasiwasi juu ya vitendo vya mauaji ya viongozi wa dini vinavyotokea
siku hadi siku nchini.
Hayo yalielezwa na Mufti Mkuu
wa Zanzibar, Sheikh Saleh Omar Kaabi,alipozungumza na mwandishi wa habari hizi
ofisini kwake Mazizini juu ya tukio la
mauaji ya Padri Evarist Mushi.
Alisema vitendo hivyo ni
matukio ya watu wasioitakia mema Zanzibar
na havina uhusiano wa kidini kwa sababu dini zote zimekataza binadamu
kuchukua hatua ya kumuua mwenzake.
Sheikh Kabi alisema tukio la
kuuliwa kwa Padri Mushi limewahuzunisha wanachi na waumini wa dini ya kiislamu
kwani wote wanaishi kwa amani na upendo.
Aidha aliwataka wananchi kuachana
na vitendo vya uhalifu vinavyosababisha uvunjifu wa amani na kuwaomba viongozi
wa dini kuwaelimisha waumini wao kuwa watu wema wanaopendana.
Alifahamisha kuwa ni vyema kwa
vyombo vya ulinzi kufanyakazi kwa uhakika ili kudhibiti mtandao unaohatarisha
amani iliyodumu kwa muda mrefu Zanzibar.
Nae Mwalimu wa Idara ya Vijana
wa Waumini ya dini ya Kikiristo Zanzibar, David Vikta Suna, alisisitiza kuwepo
kwa ushirikiano kati ya serikali na wananchi ili kuona vitendo hivyo
vinadhibitiwa na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
No comments:
Post a Comment