Habari za Punde

SIDA watoa msaada wa Vitabu skuli ya msingi Kojani

 MKUTUBI wa Maktaba Kuu ya Pemba Azida Salim Juma, akiwawagawia wanafunzi 60 wa skuli ya kojani msingi Vitabu, katika mikakati ya kuwahamasisha wanafunzi kupenda kusoma vitabu, wakati wa utekelezaji wa mradi wa SIDA.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WANAFUNZI wa Skuli ya Msingi Kojani wakisoma vitabu baada ya kupatiwa na wafanyakazi wa Makatba kuu ya Pemba, katika utekelezaji wa mradi wa kuhamasisha wanafunzi maskulini Pemba kusoma unaofadhiliwa na SIDA.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WANAFUNZI wa skuli ya kojani Msingi wakionesha vitabu vyao walivyopatiwa na wakutubi wa maktaba kuu ya Pemba, kupitia mradi wa SIDA, ambao unahamasisha wanafunzi kupenda kusoma vitabu.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MMOJA wa Wanafunzi wa skuli ya msingi Kojani akisoma kitabu cha hadithi, alichopatiwa na wakutubi wa maktaba kuu ya Pemba, katika utekelezaji wa mradi wa SIDA wenye lengo la kuhamasisha wanafunzi kupenda kusoma vitabu.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WANAFUNZI wa skuli ya Kojani msingi wakichora picha mbali mbali katika utekelezaji wa mradi wa SIDA, wenye lengo la kuhamasisha wanafunzi wa skuli za msingi kupenda kusoma vitabu.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

1 comment:

  1. he! watoto wa skuli wapo kwenye mjamvi kama chuoni, dah masikini Zanzibar

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.