Habari za Punde

Serikali kuunga mkono jitihada za Chuo cha mafunzo kurekebisha tabia kwa watoto

Na Mwashungi Tahir    Maelezo. 
Waziri wa Kazi , Uwezeshaji ,Wazee, Wanawake na Watoto Moudline Cyrus Castico  amesema Serikali   ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea  kuunga mkono jitihada zinazo fanywa na chuo cha mafunzo kwa  kuweka mazingira mazuri katika ujenzi wa kukerebisha tabia kwa watoto
Amesema ujenzi wa jengo la kurekebisha watoto kutapelekea  kurahisisha utekelezaji wa sheria ya mtoto na 6 ya mwaka 2011 ya Zanzibar  inayo wataka watoto kujengewa mazingira rafiki ili kuimarisha ustawi wao.
Akizungumza kwa niaba yake Naibu Waziri wa Wizara hiyo Shadya Mohamed   Suleiman wakati alipokua katika hafla ya  uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa Ujenzi wa Chuo cha kurekebisha watoto huko Hanyegwa Mchana ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za kusherehekea Miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Amesema  kuwepo kwa changamoto ya  mlimbukano wa watoto wengi wanao letwa katika vyuo vya mafunzo  kumepelekea Serikali kujenga jengo hilo ambalo litasadia kuwaekea mazingira mazuri watoto hao katika kipindi chote cha mafunzo ya kurekebisha tabia .
Aidha alisema  hakuna jambo zuri kama kumpa mtoto malezi bora mapema samaki mkunje bado mbichi kwani watoto watapofundishwa maadili mazuri mapema kutasaidia makuzi yao kupatikana Taifa lililo bora.
“hakuna jambo zuri kama kumkerebisha mtoto mapema kwani samaki  angali mbichi akiwa mkavu hakunjiki bali anavunjika “ , alisema Naibu Waziri huyo.
Aidha amesema Serikali ya M apinduzi ya Zanzibar imeona  kuwepo kwa  chuo  cha mafunzo cha la kurekebish tabia za watoto wanaokingana na sheria kutasaidia  kupunguza idadi  nyingi ya wahalifu kwa watoto na watu wazima.

Aidha alisema malengo ya Serikali ni kuona wakufunzi wanasimamia vyema watoto hao ili kuwa wanakaa mbali wanawake na wanaume  na kuepuka vitendo vya udhalilishaji pindi litakapokamilika ujenzi wa jengo hilo .
Mapema Naibu Waziri wa Nchi , Ofisi ya  Rais Tawala za Mikoa , Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Shamata Shaame Khamis  amesema kazi kubwa ilio fanywa na mzee Karume wakishirikiana na wenzake kuhakikisha walipambana na kujitawala wenyewe .
Aidha amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechukua  uwamuzi wa kuweka miundombinu imara  na ilio bora  kuhakikisha wanawaekea mazingira sawa wale wote watakao ingia kwenye magereza kwa kukiuka sheria .

Hata hivyo   amewapongeza mafundi walio jitolea katika Chuo hicho kujenga jengo  bila ya kutafuta mafundi wengine na kuweza kuokoa fedha za serikali katika ujenzii huo
Akitoa taarifa kwa niaba ya katibu mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya  Rais Tawala za Mikoa , Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Sida Himid amempongeza Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa usimamizi mzuri wa jengo hilo kwani kutasaidia kuondosha changamoto ya mlimbikano wa wanafunzi .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.