HOTUBA YA
WAZIRI WA BIASHARA NA VIWANDA
KUHUSU
MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2020/2021

MHESHIMIWA: BALOZI AMINA SALUM ALI (MBM)
i
MHESHIMIWA BALOZI
AMINA SALUM ALI,
KATIKA BARAZA LA
WAWAKILISHI LA ZANZIBAR
KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA
MWAKA WA FEDHA 2020/2021:
1
UTANGULIZI :
1. Mheshimiwa Spika, Naomba kutoa hoja
kwamba
Baraza lako
Tukufu sasa likae kama Kamati ya Mapato na Matumizi kwa madhumuni ya kupokea,
kuzingatia, kujadili na hatimae kuidhinisha makadirio ya mapato na matumizi ya
Wizara ya Biashara na Viwanda kwa kazi za kawaida na maendeleo kwa mwaka wa
fedha 2020/2021.
2. Mheshimiwa Spika, Kwanza kabisa naomba
kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutuwezesha kufika katika ukumbi huu hii
leo tukiwa wazima na afya njema na pia kutuwezesha kuendelea kutekeleza
majukumu ya kujenga nchi yetu kwa usalama, amani na ufanisi mkubwa katika
kipindi chote cha miaka 10 ya awamu ya saba ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Ali
Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
3. Mheshimiwa Spika, Naomba kuchukua fursa
hii adhimu kumshukuru kwa dhati Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi kwa kusimamia kwa umakini
mkubwa utekelezaji
wa mipango ya
kitaifa na kimataifa, hususan uendelezaji wa Sekta ya Biashara na Viwanda, Dira
ya Maendeleo 2020, pamoja na utekelezaji wa malengo ya Ilani ya CCM ya mwaka
2010 – 2020.
4. Mheshimiwa Spika, Pia nachukua fursa
hii kumpongeza Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar kwa jitihada zake za dhati anazozichukua za kumsaidia Mheshimiwa Rais
wetu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika kuwatumikia
wananchi wa Zanzibar. Vile vile kwa kutupatia miongozo, maelekezo na maagizo
yake katika maendeleo ya nchi yetu.
5. Mheshimiwa Spika, Nathubutu kutamka
kwamba katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Saba, mafanikio makubwa
yamepatikana katika Sekta mbali mbali ikiwemo Sekta ya Biashara na Viwanda.
Aidha, kama nitakavyoeleza katika Hotuba yangu huko mbele, Serikali ya Awamu ya
Saba imeweka msingi imara wa maendeleo endelevu ya Sekta za Biashara na Viwanda
na nchi yetu kwa ujumla.
Hivyo, sina budi
kumshukuru kwa namna ya kipekee kabisa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa imani yake kubwa kwangu kwa kunikabidhi
dhamana ya kuiongoza Wizara ya Biashara na Viwanda ambayo ndio sekta kiongozi
katika kuleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii katika Taifa letu.
6. Mheshimiwa Spika, Nina hakika kuwa
nimetumia juhudi na uwezo wangu wote alionipa Mwenyezi Mungu kutekeleza kazi na
dhamana hii niliyopewa na Mheshimiwa Rais, na ni matumaini yangu kuwa mafanikio
tuliyofikia yataendelezwa kwa nguvu na msukumo wa ziada katika uongozi wa
Serikali ya Awamu inayokuja.
7. Mheshimiwa Spika, Naomba kuchukua fursa
hii pia kukushukuru wewe binafsi pamoja na Naibu Spika wa Baraza la
Wawakilishi, Wenyeviti wa Kamati za kudumu za Baraza bila kuwasahau wajumbe wa
Baraza lako tukufu kwa mashirikiano makubwa na michango na ushauri mliotupatia
kwa lengo la kufanikisha utekelezaji wa malengo ya Wizara, kwa mwaka wa fedha
2019/2020 na pia kwa ushauri na maelekezo yenu kuhusiana na utekelezaji wa
malengo ya Wizara hii kwa mwaka ujao wa 2020/2021.
8. Mheshimiwa Spika, Naomba kuchukua fursa
hii kumpa pole za dhati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
kwa kukabiliana na janga la Ugonjwa wa COVID19 unaosababishwa na Virusi vya
KORONA. Aidha, nawapa pole viongozi na Wananchi wote kwa ujumla kwa kuathirika
kutokana na ugonjwa huu thakili. Salamu maalum za rambi rambi ziwaendee
Wananchi wote waliopoteza ndugu zao na wale waliopoteza ajira kutokana na janga
hili ambalo limeathiri sana Sekta mbali mbali za Kiuchumi na Kijamii.
9. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Biashara na
Viwanda katika juhudi za kukabiliana na kuenea kwa maradhi
ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na
virusi vya CORONA (COVID – 19), iliamua kufanya tathmini juu ya upatikanaji wa
vifaa kinga vya maradhi hayo. Matokeo ya tathmini hiyo imeonesha
kutokuridhishwa kwa vifaa hivyo na upandishwaji wa bei na vyengine havikidhi
viwango au havifai kabisa.
10. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa
kushirikiana na Wakala wa Chakula na Dawa (ZFDA) pamoja na Mkemia Mkuu wa
Serikali (CGCLA) iliandaa na kutoa mafunzo ya kutengeneza vifaa kinga kwa
wajasiriamali 25 pamoja na wahitimu wa vyuo 3 ambao wameshirikiana na
wajasiriamali kuzalisha vitakasa mikono (sanitizer). Kwa upande wa barakoa
(mask), Wizara imeshirikiana na kiwanda cha Serikali kilichopo Amani (ZQTL) kwa
kukipatia aina (sample) na malighafi na wameweza kutengeneza. Lengo ni vifaa hivi
viweze kupatikana kwa uhakika na kwa bei nafuu na kila mwananchi amudu
kuvitumia.
11. Mheshimiwa Spika, Bila shaka ugonjwa
huu utakuwa na athari kubwa kwenye pato la mtu mmoja mmoja na kupunguza kasi ya
ukuaji wa pato la Taifa. Hata hivyo, “Wahenga wanasema mwisho wa dhiki ni
faraja” naamini tutavuka katika kipindi hiki kigumu tukiwa washindi kama
tulivyovuka majanga mengine yaliyotokea miaka ya nyuma kama Kipindupindu,
Ukimwi (HIV) na Malaria. Tumuamini Mwenyezi Mungu na tuongeze juhudi za
kupambana na Ugonjwa wa COVID-19, bila ya shaka kwa kufuata masharti ya
Wataalamu wa Afya na maelezo yanayotolewa na Serikali ugonjwa huu tutaushinda.
12. Mheshimiwa Spika, Mapendekezo ya bajeti
hii yamepitia katika hatua na ngazi mbali mbali za awali ikiwemo Kamati ya Uongozi
ya Wizara na Kamati ya Kudumu ya Fedha, Biashara na Kilimo ya Baraza la
Wawakilishi. Naomba kuchukua fursa hii kuishukuru sana Kamati hii inayoongozwa
na Mheshimiwa Mwinyihaji Makame Mwadini, Mwakilishi wa Jimbo la Dimani kwa
kuchambua mapendekezo ya awali ya bajeti hii na hatimae kuridhia kuwasilishwa
mbele ya Baraza lako Tukufu kwa kujadiliwa na kuidhinishwa.
13. Mheshimiwa Spika, Aidha, shukurani
zangu za pekee zimwendee Naibu Waziri wa Wizara hii Mheshimiwa Hassan Khamis
Hafidh kwa mashirikiano yake makubwa anayonipatia katika kuhakikisha malengo ya
Wizara yanafikiwa. Pia nawashukuru kwa dhati ndugu Juma Hassan Reli, Katibu
Mkuu na ndugu Khadija Khamis Rajab, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hii,
Wakurugenzi na viongozi wote wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Wizara ya
Biashara na Viwanda pamoja na Wafanyakazi wote wa Wizara kwa juhudi zao kubwa
za kuchapa kazi pamoja na mashirikiano makubwa wanayonipatia yaliyosaidia
katika utekelezaji mzuri wa majukumu yangu.
14. Mheshimiwa Spika, Matayarisho ya bajeti hii yamezingatia miongozo mbalimbali
iliyowekwa na Serikali ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020, Mpango wa
Ukuzaji Uchumi na Kuondoa Umasikini Zanzibar (MKUZA III), Ilani ya CCM ya mwaka
2010 -2020, Sera za Biashara na Viwanda, maagizo yanayotolewa na viongozi wakuu
wa
nchi pamoja na
Ukomo wa Rasilimali Fedha uliopangiwa kwa Wizara.
15. Mheshimiwa Spika, Pamoja na mazingatio
ya hapo juu, utayarishaji wa mapendekezo haya ulizingatia pia matukio mbali
mbali yaliyojitokeza ulimwenguni ambayo yamekuwa na athari za moja kwa moja
katika mwenendo wa biashara, viwanda na uchumi duniani. Matukio hayo ni kama
vile janga la Dunia lililojitokeza hivi karibuni la maradhi ya COVID–19
yanayosabishwa na virusi vya KORONA, kushuka kwa bei ya mafuta Duniani,
kupungua kwa mwenendo wa uwekezaji duniani, kuathirika kwa mwenendo wa biashara
na fedha pamoja na masuala ya kisiasa katika baadhi ya maeneo ya Dunia.
16. Mheshimiwa Spika, Katika hotuba yangu
hii, nitaanza kwa kufanya mapitio ya jumla kuhusu mwenendo wa biashara na hali
ya viwanda, utekelezaji wa malengo ya bajeti ya Wizara kwa mwaka 2019/2020, na
hatimae nitawasilisha mapendekezo ya bajeti kwa programu za Wizara kwa mwaka ujao
2020/2021.
2
MWENENDO WA BIASHARA :
17. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
awamu ya Saba, sekta ya Biashara imepata mafanikio makubwa kutokana na juhudi
za Serikali za kuimarisha mazingira mazuri ya biashara na kurahisisha ufanyaji
wa biashara hapa Zanzibar. Juhudi hizo zimepelekea kupitisha sheria mbali
mbali, kuanzisha taasisi na kuziimarisha baadhi ya taasisi nyengine.
18. Mheshimiwa Spika, Serikali katika
juhudi zake za kulinda afya na usalama kwa watumiaji wa bidhaa, huduma na
kuhifadhi mazingira nchini, ilitunga Sheria
Namba 1 ya mwaka
2011 ya Viwango, Zanzibar.
Sheria hii
ilianzisha Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) yenye malengo ya kuweka viwango na
kusimamia ubora wa bidhaa zinazozalishwa au kuingizwa nchini kutoka nje ya
nchi. Mpaka sasa ZBS imeanzisha maabara 3 (Kemikali, Vifaa vya umeme na
Chakula) zinazofanya kazi, ujenzi wa Ofisi na maabara za ziada unaendelea
katika eneo la Maruhubi.
19. Mheshimiwa Spika, Serikali katika lengo
la kurahisisha na kuendeleza Biashara Zanzibar imetunga Sheria Namba 13 ya Mwaka 2012, inayosimamiwa na Wakala wa Usajili
wa Biashara na Mali Zanzibar (BPRA). Taasisi hii imepewa jukumu la kufanya
usajili wa Biashara na Mali, ikijumuisha usajili wa taasisi za Biashara, Mali
za Ubunifu pamoja na Usajili wa Nyaraka mbali mbali zinazowahusu wananchi na
wageni wanaoishi au wanaofanya shughuli zao Zanzibar. Tangu kuanzishwa BPRA,
imerahisisha masuala ya usajili kwa kufanya marekebisho na mageuzi ya mifumo ya
usajili wa Biashara na mali kwa kuandaa mifumo mipya ya usajili kwa kutumia
mfumo wa kielektroniki.
20. Mheshimiwa Spika, Katika kurahisisha na
kuendeleza Biashara, Serikali imetunga Sheria ya Kusimamia Mfumo wa Utoaji
Leseni za Biashara ya mwaka 2013 (The
Business Licensing Regulatory Act No. 13 of 20I3). Lengo kuu la sheria hiyo
ni kuondosha changamoto zote zinazoukabili mfumo wa utoaji leseni za Biashara
uliokuwa ukiendelea kutumika. Sheria hiyo imeanzisha Baraza la Kusimamia
Mageuzi ya Mfumo wa Utoaji Leseni za Biashara (BLRC) ili kuweza kusimamia
mageuzi kwa taasisi zinazotoa leseni. Tangu kuanzishwa kwa BLRC, hatua za
upatikanaji wa leseni zimepungua sana, malipo ya leseni kufanyika kupitia benki
na taarifa za leseni zinapatikana wa njia ya kielektoniki.
21. Mheshimiwa Spika, Serikali katika
kuhakikisha jukwaa la majadiliano ya Biashara baina ya sekta ya umma na sekta
binafsi yanatekelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu imetunga Sheria Namba 10 ya mwaka 2017 inayosimamiwa na Baraza la Taifa la Biashara (ZNBC). Madhumuni
ya majadiliano haya ni kuwashirikisha sekta binafsi katika maendeleo ya nchi
pamoja na kutatua kero mbalimbali za wafanyabiashara.
22. Mheshimiwa Spika, Katika kusimamia
ushindani halali wa kibiashara na kumlinda Mtumiaji, Serikali imetunga Sheria Namba 5 ya mwaka 2018
inayosimamiwa na Tume ya Ushindani Halali wa Biashara na Kumlinda Mtumiaji
(ZFCC). Taasisi hii ina lengo la kuhakikisha kuwa inaimarisha na kushajihisha
ushindani halali wa biashara na kumlinda mtumiaji wa bidhaa na huduma Zanzibar.
23. Mheshimiwa Spika, Katika kuendeleza
Wajasiriamali wadogo wadogo, wadogo na wa kati Serikali imetunga Sheria Namba 2 ya mwaka 2018(Micro, Small
and Medium Enterprises Act) inayosimamiwa na Wakala wa Maendeleo ya Viwanda
Vidogo vidogo, Vidogo na vya kati (SMIDA). Madhumuni ya Wakala ni kuwaendeleza
na kuimarisha sekta ya uzalishaji viwanda kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa
zinakidhi viwango vinavyokubalika Kitaifa na Kimataifa kwa lengo la kuleta tija
na manufaa kwa Taifa. Tangu kuanzishwa kwa Wakala changamoto ya upatikanaji wa
mikopo kwa Wajasiriamali imepungua pamoja na kuimarika kwa uzalishaji wa bidhaa
wanazozalisha na kukidhi soko linalohitajika.
24. Mheshimiwa Spika, Katika kuwatafutia
masoko wajasiriamali wetu pamoja na kuhamasisha uzalishaji nchini, Wizara
imekuwa ikiandaa matamasha ya biashara pamoja na kuratibu ushiriki wa
wajasiriamali katika maonesho mbali mbali nchini, kikanda na kimataifa. Mheshimiwa Spika haya yote ni mafanikio
katika sekta ya biashara yaliyopatikana katika awamu ya saba.
2.1
Hali ya Uchumi na Biashara Duniani :
25. Mheshimiwa Spika, Katika hotuba yangu
ya bajeti ya mwaka 2019/2020, nililiarifu Baraza lako Tukufu juu ya kuyumba kwa
mwenendo wa uchumi na biashara duniani na jinsi mwenendo huo ulivyoathiri
biashara kwa nchi mbali mbali ikiwemo Zanzibar. Naomba kuliarifu Baraza
lako Tukufu kuwa
hali ya uchumi na biashara duniani bado haijatengemaa na inaendelea kutishia
kasi ya ukuaji biashara Duniani na kuathiri mchango wa sekta hii katika uchumi
wa dunia (World Merchandise Trade
Percentage of GDP) ambao unatarajiwa kupungua kwa asilimia 2.6 mwaka 2019 kutoka asilimia
3.0 mwaka 2018. Vile vile, kutokana na kulipuka kwa maradhi ya COVID19
yanayosababishwa na virusi vya KORONA ambayo yameikumba Dunia nzima tunatarajia
kuendelea kushuka zaidi kwa mchango wa sekta ya biashara kwa mwaka huu wa 2020.
Mchoro namba 1 unaonesha asilimia ya
mchango wa biashara katika uchumi wa dunia.
Mchoro Namba 1:
Mchango wa Sekta ya
Biashara katika Uchumi wa
Dunia 2016-2019

Chanzo: Shirika la Biashara la Dunia-WTO,
2020
26.
Mheshimiwa
Spika, Usafirishaji wa bidhaa duniani kwa kipindi cha mwaka 2018 ulifikia USD 19.48 trilioni, ambapo ni sawa na
ongezeko la asilimia 10
ikilinganishwa na usafirishaji uliofanyika mwaka 2017. Katika kipindi cha mwaka
2019 uagiziaji kwa nchi za Marekani ya Kaskazini umeonesha kupungua kwa kasi
ndogo wakati nchi za Marekani ya Kusini, Ulaya na Asia imeonesha kupungua kwa
kasi kubwa. Hata hivyo kwa nchi nyengine zimeendelea kuonesha ongezeko la
uagiziaji kutoka asilimia 1.9 mpaka asilimia 4.9 kwa mwaka 2019.
Mheshimiwa Spika, Mwenendo huo wa
usafirishaji na uagiziaji wa bidhaa duniani ni kwa mujibu wa taarifa ya makisio
ya Shirika la Biashara la Dunia (WTO) kwa kipindi cha mwaka 2019.
2.2
Hali ya Biashara Zanzibar
Usafirishaji na Uagiziaji wa Bidhaa:
27.
Mheshimiwa
Spika, Hali ya biashara kwa ujumla imeonesha kuimarika kwa mwaka 2019,
ambapo Zanzibar imefanya biashara yenye thamani ya Shilingi bilioni 478.52 ikilinganishwa na biashara ya Shilingi bilioni 394.04 mwaka 2018 sawa
na ongezeko la asilimia 21.4. Biashara
hiyo ilikuwa ni usafirishaji wa bidhaa kwenda nje ya Zanzibar na uagiziaji wa
bidhaa kuja Zanzibar. Bidhaa ambazo Zanzibar ilisafirisha nchi za nje ni pamoja
na karafuu, mwani, dagaa na majongoo ya pwani.
28.
Spika,
Katika kipindi cha mwaka 2019,
Zanzibar ilisafirisha nje bidhaa zenye
thamani ya Shilingi bilioni 131.65.
Kiwango hicho cha usafirishaji ni sawa na ongezeko la asilimia 126.2 kwa
kulinganisha na usafirishaji wa bidhaa zenye thamani ya Shilingi bilioni 58.19uliofanyika kipindi cha mwaka 2018. Katika
usafirishaji huo, zao la karafuu lilikuwa na thamani ya Shilingi bilioni 19.85 sawa na asilimia
27.7 ya usafirishaji wote. Ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa
usafirishaji wa tani za karafuu katika kipindi cha mwaka huu ukilinganisha na
mwaka 2018. Mnunuzi mkubwa wa karafuu za Zanzibar ni nchi ya India ikifuatiwa
na Singapore.
29.
Mheshimiwa
Spika, Kwa upande wa uagiziaji bidhaa, nchi yetu iliagiza bidhaa zenye
thamani ya Shilingi bilioni 346.88
kwa mwaka 2019 ikilinganishwa na uagiziaji wa Shilingi bilioni 335.84 mwaka 2018. Bidhaa ambazo Zanzibar imeagiza
kutoka nchi za nje ni pamoja na vyombo vya usafiri, bidhaa za elektroniki, nguo
na chakula ikiwemo mchele, sukari na unga wa ngano. Mwenendo wa biashara
umeonesha kuimarika kwa urari wa biashara kwa kupunguza nakisi yake kutoka Shilingi milioni 277,660.6 hadi Shilingi milioni 215,231.1 kwa mwaka
2019 Mchoro Namba 2 hapa chini
unatoa ufafanuzi zaidi.
Mchoro Namba 2:
Mwenendo wa Biashara Zanzibar (2010 – 2019)
2.3
Biashara Baina ya Zanzibar na Tanzania Bara (InterState Trade Balance):
30.
Mheshimiwa
Spika, Biashara baina ya Zanzibar na Tanzania Bara inahusisha utoaji wa
bidhaa kutoka Zanzibar kwenda Tanzania Bara na uingizaji wa bidhaa kutoka
Tanzania Bara kuja Zanzibar. Biashara
hiyo inahusisha bidhaa za vyakula, vifaa vya elektroniki, magari, madawa na
vinywaji. Kwa miaka ya hivi karibuni, biashara kutoka Zanzibar kwenda Bara
imeendelea kupungua na hivyo kusababisha urari mkubwa wa biashara kati ya
Zanzibar na Tanzania Bara. Hali hii ilitokana na vikwazo vya biashara
visivyokuwa vya kiushuru hasa vibali vya ruhusa ya kuingiza bidhaa na masuala
ya usajili wa bidhaa.
31. Spika, Kwa
kipindi cha mwaka 2019, Zanzibar
ilipeleka bidhaa Tanzania Bara zenye thamani ya Shilingi bilioni 21.56, ikilinganishwa na bidhaa zenye thamani ya Shilingi bilioni 24.29 zilizopelekwa
mwaka 2018. Aidha, Zanzibar iliagizia kutoka Tanzania Bara bidhaa zenye thamani
ya Shilingi bilioni 260.67
ikilinganishwa na uagiziaji wa bidhaa zenye thamani ya Shilingi bilioni 269.67 mwaka 2018. Mchoro Namba 3 hapa chini unatoa ufafanuzi zaidi.
Mchoro Namba 3:
Biashara Baina ya Zanzibar na Tanzania Bara: TZS.(Milioni )

Chanzo: Wizara ya Biashara na Viwanda,
2020
2.4 Hali ya Chakula na Bei katika Soko la Zanzibar
:
32. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka 2019
Takwimu za uingizaji chakula kutoka nje zinaonesha kwamba jumla ya
Tani 100,331 za
mchele, Tani 30,362 za sukari na Tani 41,904 za unga wa ngano zilikuwepo katika
kipindi hicho kwa ajili ya matumizi ya soko la ndani, kama inavyoonekana katika
Mchoro Namba 4 hapa chini.
Mchoro Namba 4:
Wastani wa Uingizaji
wa Chakula Muhimukatika Soko la Zanzibar 2019
(Tani):

!
Chanzo: Wizara ya Biashara na Viwanda,
2020
33. Mheshimiwa Spika, Uwepo wa chakula pia
ulichangiwa na uzalishaji wa bidhaa hizo nchini. Kwa kipindi cha Januari mpaka
Oktoba 2019, uzalishaji wa Sukari nchini ulifikia tani 6,674 ambazo
zilinunuliwa na kutumika ndani ya Zanzibar. Kwa upande wa unga wa ngano tani
37,143 zilizalishwa kwa kipindi cha Januari mpaka Disemba 2019.
34. Spika, Bei za bidhaa muhimu kama za
mchele na unga wa ngano ziliongezeka
kidogo katika soko la ndani kwa mwaka 2019 ukilinganisha na mwaka 2018. Napenda kuliarifu Baraza lako tukufu kwamba
Serikali inaendelea na utaratibu wa kusimamia bei za bidhaa muhimu (mchele,
sukari na unga wa ngano) na kuangalia uwezekano wa kuongeza aina nyingine za
bidhaa zinazowagusa sana wananchi. Kwa jumla wastani wa bei za reja reja za
bidhaa muhimu kwa mwaka 2019 katika masoko ya Zanzibar ni kama zinavyoonekana
katika Jadweli Namba 1 hapa chini:
Jadweli Namba 1:
Wastani wa Bei za Reja
Reja za Chakula Muhimu katika Soko la Zanzibar:
(TZS/Kilo)
Bidhaa
|
Julai - Sept
|
Okt – Dis
|
Jan – Machi
|
Mchele (Tulip,
|
|||
Kasuku)
|
1,533
|
1,620
|
1,564
|
Basmati
|
3,726
|
3,714
|
3,714
|
Sukari
|
1,891
|
1,893
|
1,897
|
Unga Ngano
|
1,363
|
1,387
|
1,387
|
Chanzo:
Wizara ya Biashara na Viwanda, 2020
3
HALI YA VIWANDA :
35. Mheshimiwa Spika, Miongoni mwa
Viashiria vinavyotumika kupima maendeleo ya nchi duniani ni ukuaji na mchango
wa Sekta ya Viwanda katika pato la Taifa. Wizara imeendelea kufanya juhudi
mbali mbali kuhakikisha kwamba sekta ya viwanda inaimarika na mchango wake
katika ujenzi wa uchumi unaongezeka siku hadi siku. Jitihada hizo ni pamoja na
kutafuta wawekezaji kutoka nje ya nchi lakini pia kuwahamasisha wawekezaji
wazalendo waweze kuanzisha viwanda. Lengo ni kuhakikisha bidhaa nyingi zaidi
zinazalishwa hapa hapa nchini pamoja nakuongeza usafirishaji wa bidhaa nje ya
nchi kwa kutambua kwamba uchumi wa viwanda ndio uchumi imara zaidi (Stable
Economy) na himilivu hata pale inapotokea
mdororo wa kiuchumi duniani (Economic Recession), kutokana na athari za
majanga mbali mbali kama maradhi ya mripuko wa COVID-19 yaliyoikumba dunia hivi
sasa.
36. Mheshimiwa Spika, Mchango wa Viwanda
katika pato la Taifa umeendelea kuongezeka kutoka asilimia 17.8 mwaka 2018 hadi
kufikia asilimia 18.3 mwaka 2019 hii ni sawa na ongezeko la asilimia 0.5
iliyotokana na kufanya vizuri sekta ya uzalishaji Viwandani. Mripuko wa ugojwa
wa COVID-19 umeonesha bayana umuhimu wa kuimarisha na kukuza viwanda vyetu
ambapo jitihada zimeonekana.
Mchoro Namba 5:
Mchango wa Sekta za kiuchumi katika Pato la

37. Mheshimiwa Spika, Sekta ya huduma ndiyo
inayokuwa kwa kasi zaidi ukilinganisha na sekta nyengine za uchumi. Hali hii ni
kutokana na kuimarika kwa sekta ya utalii na kuongezeka kwa uwekezaji mkubwa
uliofanyika katika sekta hiyo. Hata hivyo kutokana na hatua mbali mbali
zilizochukuliwa na Serikali ya awamu ya saba chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein ,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kumesaidia sana kuongeza
mchango wa sekta ya viwanda katika uchumi wetu. Juhudi hizo ni pamoja na
kuanzisha kwa Wakala wa Kusimamia na Kuendeleza viwanda vidogo vidogo na vya
kati (SMIDA), kupitisha Sera mpya ya Viwanda
pamoja na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji
kwa ujumla
ambavyo vyote vimefanyika katika kipindi hiki cha awamu ya saba.
38. Mheshimiwa Spika, Hali ya uzalishaji
bidhaa viwandani kwa mwaka 2019/2020 imeendelea kuimarika licha ya kuwepo kwa
changamoto ya soko la Tanzania Bara kwa bidhaa zinazozalishwa na viwanda vyetu
hapa Zanzibar. Tozo ya mifugo (livestock levy) ya shilingi 250 kwa lita moja ya
maziwa yanayozalishwa na kiwanda cha ADPL kilichopo Fumba yanapoingia katika
soko la Tanzania Bara imeathiri kwa kiwango kikubwa mauzo ya bidhaa hiyo na
kusababisha kuporomoka kwa mapato ya kiwanda kiasi cha kushindwa
kujiendesha kibiashara. Hivyo, athari ya tozo hiyo inapelekea maziwa ya ADPL
kuwa ghali zaidi katika soko la Tanzania na kupoteza ushindani wa bei. Kwa
mwaka 2019/2020 Kiwanda kimeweza kuzalisha lita 1,757,982 za maziwa
ukilinganisha na lita 8,028,883 zilizozalishwa mwaka 2016/2017 na kulipa
Shilingi milioni 315 kama mishahara ya
wafanyakazi.
39. Mheshimiwa Spika, Kiwanda cha Zanzibar
Milling Corporation (ZMCL) kilichopo Mtoni kinachozalisha bidhaa ya unga wa
ngano kimeendelea kuimarika kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji. Hadi kufikia
Machi 2020 jumla ya tani 27,070.1 za unga wa ngano na tani 6,690.72 za pumba
(bran) zimeweza kuzalishwa na kuuzwa.
40. Mheshimiwa Spika, Uzalishaji katika
kiwanda cha Sukari (ZSFL) kilichopo Mahonda umeendelea kuimarika kutokana na
muitikio mzuri wa wananchi kulima miwa katika maeneo yao (Out growers) na
kuiuza kiwandani hapo. Kutokana na matokeo hayo ya kupigiwa mfano kiwanda
kimeweza kuvunja rekodi ya kuzalisha jumla ya tani 6,674 za sukari ambazo
hazijawahi kuzalishwa kiwandani hapo tangu kiwanda hicho kilipoanza
uzalishaji. Vile vile kiwanda kimeweza
kuzalisha lita 230,000 za spiriti (Rectified Ethanol) ambayo ni bidhaa muhimu
katika kutengeneza viosha mikono (Sanitizer) na tani 3,600 za Molasses (Energy
Concentrate) ambayo ni bidhaa muhimu kwa ajili ya kutengeneza virutubisho vya
malisho ya mifugo hasa Ng’ombe.
Matarajio kwa mwaka 2020/2021 ni kuzalisha
tani 8,000 za
sukari, lita 800,000 za spiriti na tani 4,500 za molasses.
41. Mheshimiwa Spika, Kuongezeka kwa
uzalishaji katika viwanda nchini kuna manufaa makubwa sana katika kukuza uchumi
na maendeleo ya jamii (Socio-economic Development) ikiwa ni pamoja na
kutengeneza ajira. Kwa mwaka wa fedha 2019/2020 mbali na malipo ya mishahara
kwa wafanyakazi viwandani; zaidi ya shilingi bilioni 3 zimekusanywa na Serikali
kutokana na kodi na tozo mbali mbali kwa viwanda vitatu tu kama inavyoonekana
katika kiambatanisho namba 1
42. Mheshimiwa Spika, Mbali ya uwepo wa
viwanda hivyo vikubwa, vipo viwanda vya kati ambavyo vimeanza uzalishaji katika
kipindi cha 2019/2020. Miongoni mwa viwanda hivyo ni Turky Mifuko
kinachozalisha mifuko (woven carrier bags) kilichopo Mgeni Haji chenye uwezo wa
kuzalisha kilo 500,000 za mifuko kwa mwezi. Kiwanda kipya cha Zanto cha
kusarifu tungule (Tomato Paste) na pili pili (Chilli Sauce) kilichopo Shakani,
Kiwanda cha kuzalisha vifungashio (Messab Packaging) kilichopo Dimani, kiwanda
cha kusarifu zao la chumvi kilichopo Kiembe Samaki, Kiwanda cha kuzalisha
mafuta ya nazi (Virgin Coconut Oil), Kiwanda cha kutengeneza mabati, Kiwanda
cha kusarifu korosho na Kiwanda cha kuzalisha vifungashio vya kuhifadhia
vyakula vilivyopo katika Eneo la Viwanda Amani (AIP).
43. Mheshimiwa Spika, Baada ya Utangulizi
na maelezo hayo ya awali kuhusu hali ya biashara na viwanda, naomba sasa
niwasilishe utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Biashara na Viwanda kwa mwaka wa
fedha 2019/2020 na mwelekeo wa malengo ya mwaka 2020/2021.
4
UTEKELEZAJI
WA BAJETI NA MIPANGO YA WIZARA KWA MWAKA 2019/2020:
4.1 Ukusanyaji wa Mapato:
44. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2019/2020, Wizara ya Biashara na Viwanda ilipangiwa lengo la kukusanya mapato
ya shilingi bilioni 1.896 kutoka katika vyanzo vyake mbali mbali. Kwa kipindi
cha miezi Tisa (Julai 2019 – Machi 2020), Wizara ilikadiria kukusanya mapato ya
shilingi bilioni 1.467. Hadi kufikia mwezi wa Machi, 2020, jumla ya shilingi
milioni 600.13 zilikwishapatikana ikiwa ni sawa na asilimia 41 ya makisio ya
makusanyo ya miezi tisa na kuingizwa katika Mfuko mkuu wa Serikali.
45. Mheshimiwa Spika, Kati ya fedha hizo
jumla ya shilingi milioni 41.3 zilipangwa kukusanywa kwa upande wa Ofisi kuu
Pemba, hadi kufikia 31 Machi, 2020 jumla ya shilingi milioni 28.09 zimekusanywa
ikiwa ni sawa na asilimia 68 ya fedha zilizopangwa kwa kipindi hiki. Kwa upande
wa Idara ya Biashara na Ukuzaji Masoko kupitia kitengo cha Vipimo na Mezani
kilipanga kukusanya Shilingi milioni 525.57 hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2020
jumla ya shilingi milioni
56.01 zimekusanywa
sawa na asilimia 11 ya makadirio ya mapato hayo.
Aidha, Taasisi ya
Viwango (ZBS) ilipangiwa kukusanya Shilingi milioni 545.00 kutoka katika malipo
ya usimamizi wa viwango, hadi kufikia 31 Machi, 2020 jumla ya Shilingi milioni
295.86 zimekusanywa sawa na asilimia 54 ya mapato kwa kipindi hiki. Kadhalika,
Wakala wa Usajili Biashara na Mali (BPRA) ilipanga kukusanya Shilingi milioni
355.30 kutokana na vyanzo vyake mbali mbali vya mapato kwa huduma inazotoa,
hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2020 jumla ya Shilingi milioni 220.17 sawa na
asilimia 62 zimekusanywa kwa kipindi hiki.
46. Mheshimiwa Spika, Mchanganuo wa Mapato
hayo kwa kipindi cha Julai 2019 - Machi 2020, ni kama unavyoonekana katika
Jadweli Namba 2 hapa chini;
47. Mheshimiwa Spika, Sababu kubwa ya
kushuka kwa mapato kwa kipindi cha mwaka 2019/2020, ni kutokana na kupungua kwa
kazi usajili na gharama za malipo ya maombi mapya ya biashara na kufanya
mapitio ya taratibu za usajili na gharama zake. Aidha, kwa kipindi cha robo ya
tatu (Januari – Machi), biashara kwa ujumla imeathirika kutokana na mripuko wa
ugonjwa wa COVID – 19 ambao umesababisha kupungua kwa makampuni ya nje ya nchi
yanayoshajihisha biashara ya huduma na bidhaa nchini.
4.2
Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2019/ 2020:
48. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha
2019/2020, Wizara ya Biashara na Viwanda, iliidhinishiwa matumizi ya jumla ya Shilingi bilioni 15.597 kwa ajili ya
kutekeleza program kuu nne (4) na
program ndogo kumi (10). Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 7.547 zilipangwa kutumika kwa ajili ya kazi za
kawaida na shilingi bilioni 8.050
kwa kazi za maendeleo. Hadi kufikia Machi 2020, Wizara iliingiziwa jumla ya Shilingi bilioni 6.25 ambazo ni sawa na
asilimia 40 ya bajeti ya mwaka.
Mchanganuo wa matumizi hayo kwa kila program ulikuwa kama unavyoonekana katika Kiambatanisho Namba 2.
49. Mheshimiwa Spika, Sababu kubwa ya
matumizi ya asilimia 40 ni kuchelewa kwa upatikanaji wa fedha za kuwaendeleza
wajasiriamali (Khalifa Fund), upatikanaji wa fedha za kuendeleza maeneo ya
viwanda pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya Wizara inayohusu ujenzi
kuchukua muda mrefu kutokana na taratibu zake. Miradi yenyewe ni ujenzi wa
Maabara na Afisi za Taasisi ya Viwango (ZBS) na ujenzi wa Afisi za Wakala wa
Kusimamia na Kuendeleza Viwanda vidogo vidogo na vya kati (SMIDA).
Mheshimiwa Spika, Matarajio ni kuwa kabla ya kumalizika mwaka wa
fedha 2019/2020 utekelezaji utaongezeka kwa asilimia kubwa zaidi.
4.3
Utekelezaji wa Malengo ya Wizara :
50. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa bajeti
ya Wizara ya Biashara na Viwanda ulifanyika kulingana na huduma na shughuli
zilizowekwa katika programu za Wizara kama ifuatavyo:
PROGRAMU KUU YA UENDESHAJI NA URATIBU WA
WIZARA YA BIASHARA NA VIWANDA:
51. Mheshimiwa Spika, Programu kuu ya
Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Biashara na Viwanda imeundwa na Programu
ndogo tatu ambazo ni Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Biashara; Programu
ndogo ya Uratibu wa Mipango, Sera na Tafiti; na Programu ndogo ya Uratibu na
Utekelezaji wa Shughuli za Wizara Pemba. Katika kutekeleza majukumu yake,
program hii ilipangiwa matumizi ya Shilingi bilioni 2.99 kwa mwaka wa fedha
2019/2020.
Napenda kuliarifu
Baraza lako tukufu kwamba, hadi kufikia Machi 2020, programu hii imeingiziwa
jumla ya shilingi bilioni 2.31
ikiwemo mishahara na kazi nyengine za uendeshaji sawa na asilimia77 ya makadirio ya mwaka. Utekelezaji wa huduma
zilizopangwa katika kila program ndogo nilizozitaja ni kama ifuatavyo:
Programu ndogo ya Uendeshaji na Uratibu wa
Wizara ya Biashara:
52. Mheshimiwa Spika, Programu hii ndogo ya
Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Biashara inasimamiwa na Idara ya Uendeshaji
na Utumishi. Kwa mwaka wa fedha 2019/2020, programu hii ndogo ilikuwa na jukumu
la kutoa huduma ya ununuzi wa vifaa vya ofisi na usafiri pamoja na huduma ya
usimamizi wa rasilimali watu na huduma kwa ujumla ambayo inahusisha kazi za
uimarishaji wa mazingira mazuri ya kufanyia kazi, utoaji wa huduma kwa Idara
zote za Wizara na uratibu wa mikutano ya majadiliano ya ndani, ya Kikanda na ya
Kimataifa. Program hii ndogo ilipangiwa matumizi ya shilingi bilioni 2.14 kwa
mwaka wa fedha 2019/2020. Hadi kufikia Machi 2020, programu hii ndogo
imeingiziwa jumla ya shilingi bilioni
1.74 ikiwemo mishahara na kazi nyengine za uendeshaji sawa na asilimia 81 ya makadirio ya mwaka.
Huduma za Program ndogo ya
Utawala na Uendeshaji zilitekelezwa kama ifuatavyo:-
Usimamizi wa Rasilimali Watu na Huduma kwa
Ujumla:
53. Mheshimiwa Spika, Katika kuimarisha
mazingira ya utendaji kazini, Wizara imeendelea kuwalipa mishahara wafanyakazi
217 (Wanaume 108, Wanawake 109) pamoja na stahiki zao kwa mujibu wa muundo wa
malipo wa Serikali. Aidha, Wizara imefanya maombi Tume ya Utumishi Serikalini
ya kubadilishwa kada wafanyakazi watano (5) baada ya kurudi masomoni na
mfanyakazi mmoja (1) tayari ameshabadilishwa. Kadhalika, Wizara iliwapatia
likizo na stahiki zao wafanyakazi 38, kati ya hao wafanyakazi 25 wamepatiwa
likizo la kawaida, 9 likizo la dharura na 4 likizo la uzazi pamoja na kumpatia
mfanyakazi mmoja (1) gharama za mazishi. Pamoja na hayo, Wizara imeajiri
wafanyakazi wapya 44 katika fani ya Uchumi, Biashara, Utawala, Ununuzi, Sheria,
Uhandisi na Katibu muhtasi.
54. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kuratibu na kuwapatia mafunzo wafanyakazi wake kulingana na mahitaji husika
ambapo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 mfanyakazi mmoja (1) amepatiwa mafunzo ya
muda mrefu katika fani ya Uchumi. Wafanyakazi nane (8) wanaendelea na masomo
katika fani ya Uchumi, Takwimu na uendeshaji, Secretarial management, Maendeleo
ya miji (Rural/Urban Development) na Utawala katika ngazi ya Uzamili na
Uzamivu.
Aidha, Wizara imewapatia mafunzo ya muda
mfupi na elekezi wafanyakazi 40, kati ya hao wafanyakazi thelathini na nne (34
waajiriwa wapya) mafunzo elekezi, watano (5) mafunzo ya kujiandaa na maisha
baada ya kustaafu na Mfanyakazi mmoja (1) mafunzo ya Udereva.
55. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
Kuratibu na kushiriki mikutano ya majadiliano ya biashara na viwanda ya
Kitaifa, Kikanda na Kimataifa. Wizara ilishiriki Mikutano tisa
(9) ya majadiliano ya biashara katika
ngazi za wataalamu
na Mawaziri. Mikutano hiyo ni Mkutano wa
mafunzo ya sheria na uchunguzi wa alama za biashara nchini Korea, Mkutano wa
ushiriki wa kuendeleza viwanda vya nguo kanda ya Afrika Mashariki nchini
Rwanda, Mkutano wa soko la pamoja la Afrika (Africa Continental Free Trade
Agreement (AFCFTA) nchini Ethiopia na Mkutano wa kufanya tathmini ya gharama za
uzalishaji wa bidhaa ya sukari nchini Msumbiji, Ethiopia, Dar-es- Salaam na
Dodoma.
Huduma
ya Ununuzi wa Vifaa vya Ofisi
56. Mheshimiwa Spika, Katika kuimarisha
mazingira mazuri ya ufanyaji kazi na upatikanaji wa huduma kwa wakati kwa mwaka
wa fedha 2019/2020, Wizara imeendelea kufanya ununuzi kwa kuzingatia mpango wa
manunuzi wa mwaka. Manunuzi hayo ni pamoja na vifaa vya kuandikia, mafuta,
vifaa vya usafiri, Komputa na vifaa vyake pamoja na vifaa vya usafiri. Aidha,
Wizara imefanya ukarabati wa jengo la Ofisi kuu kwa kupaka rangi, marekebisho
ya mfumo wa maji safi na maji taka na eneo la maegesho ya magari, matengenezo
ya umeme na ukarabati mdogo mdogo.
Programu ndogo ya Uratibu wa
Mipango, Sera na
Tafiti za Wizara:
57. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Uratibu wa Mipango, Sera na Tafiti ilikuwa na jukumu la kutayarisha, kuchambua
na kutathmini utekelezaji wa mipango na malengo
maalum ya Wizara. Huduma ambazo
zimesimamiwa na Programu hii ndogo ni Uandaaji na Uibuaji wa Sera na Tafiti za
Wizara, Uandaaji na Utekelezaji wa Mipango ya Wizara na Usimamizi wa
Takwimu za Biashara na Viwanda. Program
hii ndogo ilipangiwa matumizi ya shilingi
milioni 367.12 kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Hadi kufikia Machi 2020,
programu hii ndogo imeingiziwa jumla ya shilingi milioni 235.55 milioni ikiwemo
mishahara na kazi nyengine za uendeshaji sawa na asilimia 64 ya makadirio ya
mwaka. Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa programu hii ndogo, huduma ambazo nimezitaja hapo juu
zimetekelezwa kama ifuatavyo: -
Uandaaji na Uibuaji wa
Sera na Tafiti za Wizara
58. Mheshimiwa Spika, Katika kuweka
mazingira mazuri ya ufanyaji biashara na uwekezaji, Wizara imeandaa na
kuwasilisha Serikalini Sera ya Maendeleo ya Sekta Binafsi kwa madhumuni ya
kuikuza na kuisimamia sekta binafsi ili iweze kuongeza tija na kushiriki katika
maendeleo ya nchi. Sera hii imepitishwa na kukubalika ianze utekelezaji wake
mara moja. Aidha, Wizara imefanya uzinduzi wa Sera ya Viwanda ya mwaka
2019/2029. Kwa hatua nyingine, Wizara imefanya mapitio ya Sera ya Biashara ya
mwaka 2006 na ipo katika hatua za mwisho za kuiwasilisha Serikalini.
59. Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha
utafiti mdogo wa Mahitaji ya soko la
Uyoga (Demand for Mushroom). Matokeo ya utafiti huo yameonesha kwamba mahitaji
ya uyoga kwa mwezi ni kilo 3,840 ambapo uzalishaji wa ndani
ni kilo 12.
Aidha, utafiti umeonesha kwamba asilimia 64 ya Hoteli zinatumia uyoga wa
Viwandani (Canned) kutoka nje ya nchi na asilimia 26.15 zinatumia uyoga asili
na asilimia 9.23 hazitumii uyoga katika menu zao. Uyoga wa asili unaotumika kwa
wingi Zanzibar ni aina ya ‘Oyster’, ‘Button’ na Portobello”. Utafiti umeonesha
kuwepo na soko kubwa la zao la uyoga hasa katika sekta ya utalii. Aidha, Wizara
itawasilisha matokeo hayo Tume ya Mipango na kwa wadau ili kuhamasisha
uzalishaji wake hapa Zanzibar.
Uandaaji na
Utekelezaji wa Mipango ya Wizara
60. Mheshimiwa Spika, Katika kuhakikisha utekelezaji
wa malengo ya Wizara tuliopanga kwa mwaka wa fedha 2019/2020 yamefikiwa, Wizara
imeandaa mpango kazi wa Wizara na mpango wa ufuatiliaji na tathmini kwa kazi za
maendeleo. Aidha, ripoti za utekelezaji wa miradi na kazi za kawaida kwa kila
kipindi cha robo mwaka zimeandaliwa pamoja na kuandaa vipaumbele kwa sekta ya
Biashara na Viwanda kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
Usimamizi wa Takwimu za Biashara
61. Mheshimiwa Spika, Wizara imefanya
utafiti mdogo (survey) ya kupima soko la bidhaa za viwanda (Maji), pamoja na
mambo mengine, soko kuu la bidhaa ya maji inayozalishwa ni hapa hapa Zanzibar.
Utafiti umeonesha gharama kubwa za usafirishaji; alama ya ubora ya Taasisi ya
Viwango ya Tanzania Bara na cheti cha Wakala wa Chakula
na Madawa ya
Tanzania bara pamoja na vibali mbali mbali ni miongoni mwa vikwazo
vinavyoikumba bidhaa ya maji kupata soko nje ya Zanzibar.
62. Mheshimiwa Spika, Katika usimamizi wa
Takwimu, Wizara imekusanya na kuzihifadhi Takwimu za bidhaa mbalimbali kutoka
Tanzania bara zikiwemo bidhaa za vyakula, mboga, vyombo vya usafiri na
vinywaji. Takwimu hizo hukusanywa kila mwezi kupitia Bandari zetu za Malindi,
Wesha, Wete na Mkoani. Aidha Takwimu zilizokusanywa zimewasilishwa Ofisi ya
Mtakwimu Mkuu wa Serikali kwa uchambuzi zaidi.
Programu ndogo ya Uratibu na Utekelezaji wa
Shughuli za Wizara Pemba:
63. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Ofisi Kuu Pemba ina jukumu la kutekeleza na kusimamia shughuli zote za Wizara
ya Biashara na Viwanda kwa upande wa Pemba. Programu hii ndogo ilipangiwa
matumizi ya shilingi milioni 485.99 kwa mwaka wa fedha 2019/2020, na hadi kufikia
Machi 2020, programu hii ndogo imeingiziwa jumla ya shilingi milioni 342.36 ikiwa ni mishahara na kazi nyengine za
kawaida sawa na asilimia 70 ya
makadirio ya mwaka. Huduma iliyopangwa kutolewa na Programu hii imetekelezwa
kama ifuatavyo:-
Uratibu wa Shughuli za Wizara Pemba
64. Mheshimiwa Spika, Katika kutekeleza
huduma hii,
Wizara ilifanya
shughuli mbali mbali zikiwemo;
i.
Utoaji wa huduma na ununuzi wa vifaa ambapo Wizara
kupitia Afisi Kuu Pemba ilifanya ununuzi wa vifaa vya kufanyia kazi, ununuzi wa
huduma za umeme, maji na mawasiliano, ununuzi wa gari moja (1), ununuzi wa
mafuta na kutoa huduma ya usafiri kwa maafisa wa Wizara kwa ajili ya
ufuatiliaji wa kazi mbali mbali za Wizara;
ii.
Usimamizi rasilimali watu na huduma kwa ujumla katika
kuhakikisha wafanyakazi wanapatiwa stahiki zao, Wizara kupitia Ofisi kuu Pemba
imewapatia likizo jumla ya Wafanyakazi 23. Aidha, Afisi imewapatia mafunzo
elekezi waajiriwa wapya 7 kwa lengo la kuwaongezea ufanisi katika kazi;
iii.
Katika hatua ya kuwakuza na kuwaendeleza wajasiriamali
Wizara kupitia Afisi Kuu Pemba ilitembelea jumla ya vikundi 84 vya
wajasiriamali na kuandaa mikutano mitatu (3) lengo ni kusikiliza changamoto zao
na kuweza kuzitatua katika Wilaya zote za Pemba. Kati ya vikundi hivyo,
arobaini na nane (48) vilipatiwa mafunzo ya utengenezaji sabuni, vikundi kumi
(10) vilipelekwa Tanga kujifunza kivitendo kuhusu usarifu wa bidhaa za viungo
na vikundi kumi
na sita (16)
vilishiriki katika maonesho ya saba saba Tanzania Bara na Tamasha la Biashara
la Zanzibar.
iv. Kufanya
ukaguzi wa mizani na vipimo kwa mujibu wa Sheria ambapo jumla ya mizani
662, mita ndogo za mafuta 44, mita 3 kubwa
za kutolea mafuta katika bandari ya Wesha, magari 8 ya kubebea mafuta na
matangi 4 ya mafuta ya chini yamekaguliwa katika shehia mbali mbali za Wilaya
zote za Pemba na;
v.
Kufanya ukaguzi wa maduka, maghala na bekari. Katika
ukaguzi huo jumla ya maduka 1,906 maghala 31 na bekari 42 zimekaguliwa. Kaguzi
zote hizi hufanyika ikiwa ni sehemu za hatua za kuwalinda watumiaji kwa
kuhakikisha ubora na usalama wa bidhaa zinazouzwa.
PROGRAMU KUU YA MAENDELEO YA VIWANDA NA
UJASIRIAMALI:
65. Mheshimiwa Spika, Programu kuu ya
Maendeleo ya Viwanda na Ujasiriamali ambayo utekelezaji wake unasimamiwa na
Idara ya Maendeleo ya Viwanda na Wakala wa Maendeleo ya Viwanda vidogo vidogo,
vidogo na vya kati (SMIDA) inajumuisha Programu ndogo mbili ambazo ni Ukuzaji
Viwanda na Maendeleo ya Ujasiriamali. Program hii kuu ilipangiwa jumla ya shilingi bilioni 6.85kwa mwaka wa fedha
2019/2020. Hadi kufikia Machi 2020, programu hii kuu imeingiziwa jumla ya shilingi bilioni
1.08 ikiwemo mishahara, kazi za
maendeleo na kazi nyengine za kawaida, sawa na asilimia 16 ya makadirio ya mwaka. Sababu ya asilimia ndogo ya
utekelezaji ni kama nilivyoeleza awali wakati natoa ufafanuzi wa matumizi ya
Wizara kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Program ndogo hizo utekelezaji wake ni
kama ifuatavyo:-
Programu Ndogo ya Ukuzaji Viwanda
66. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Ukuzaji Viwanda ina jukumu la kutoa huduma ya kuimarisha sekta ya viwanda.
Program hii ndogo ilipangiwa jumla ya shilingi
bilioni 3.29 kwa mwaka wa fedha 2019/2020, na hadi kufikia Machi 2020,
programu hii ndogo imeingiziwa jumla ya shilingi
bilioni 1.06 ikiwemo mishahara, kazi za maendeleo na kazi nyengine za
kawaida, sawa na asilimia 32 ya
makadirio ya mwaka. Utekelezaji wa program ndogo ya Ukuzaji Viwanda ulikuwa
kama ifuatavyo:-
Uimarishaji wa Sekta ya Viwanda
67. Mheshimiwa Spika, Katika kurahisisha na
kuweka mazingira mazuri ya uekezaji katika sekta ya viwanda, Wizara kwa
kushirikiana kampuni ya Kunshan Asia Aroma wamefanya ukarabati mkubwa wa
kiwanda cha kuzalisha mafuta ya makonyo huko Wawi, sambamba na kukamilisha
ujenzi wa kiwanda kipya cha kuzalisha mafuta ya mimea yakiwemo mkaratusi,
mchaichai, mrehani na mdalasini. Kutokana na ukarabati huo, Viwanda hivyo vina
uwezo wa kuzalisha tani 300 za mafuta ya makonyo na tani 300 za mafuta ya mimea
kwa mwaka. Kazi inayoendelea hivi sasa ni kuimarisha mashamba kwa ajili ya
kupata malighafi za kulisha viwanda hivyo.
68. Mheshimiwa Spika, Kadhalika, katika
hatua za kuliendeleza zao la mwani Wizara ya Biashara na Viwanda kwa
kushirikiana na wawekezaji kutoka Indonesia imeandaa andiko la mradi
(feasibiliyy study) kwa ajili ya uanzishaji wa kiwanda cha kusarifu zao la
mwani kinachotarajiwa kujengwa katika eneo la Viwanda Chamanangwe Mkoa wa
Kaskazini Pemba. Hatua inayofuata hivi sasa ni kutafuta fedha kwa ajili ya
kuanza ujenzi na taratibu za ununuzi wa mashine za kiwanda.
69. Mheshimiwa Spika, Hatimaye, “hayawi
hayawi sasa yamekuwa” kwa upande wa Kiwanda kipya cha nguo, kwa sasa kipo
katika hatua za mwisho kabisa katika kukamilisha ujenzi na ufungaji mitambo.
Huu ni miongoni mwa uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya viwanda hapa
nchini na Kampuni ya Basra Textiles Mills Co. Limited iliyosajiliwa hapa
Zanzibar. Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mita 200,000 kwa siku za
vitambaa aina ya Khanga, vitenge, mashuka pamoja na vitambaa vya aina mbali
mbali kulingana na mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. Ni matarajio yetu
kwamba, jumla ya wafanyakazi 500 wa kudumu watapata ajira katika kiwanda hicho
vile vile uwepo wake pia utapelekea eneo la Chumbuni kuwa ni miongoni mwa
maeneo muhimu ya kiuchumi hapa nchini.
70. Mheshimiwa Spika, Aidha, Wizara inaendelea kurahisisha uwekezaji wa Viwanda
na kupunguza changamoto zilizopo
kwa kuiombea hati ya ukodishaji ardhi (land lease) Kampuni ya AKM
Glitters limited inayojihusisha na uzalishaji
wa chakula cha kuku na chinjio la kisasa katika eneo la shamba la
Hanyegwa mchana. Lengo ni kuanza ujenzi wa shamba la kuku mama (incubator) la
kutotolea vifaranga, kiwanda cha chakula cha kuku pamoja na chinjio la kisasa (An Integrated Project) ili kuzalisha
bidhaa ambayo itakuwa na viwango vya kimataifa kwa ajili ya soko la ndani,
utalii na nje ya nchi. Aidha, Kampuni hiyo tayari imekamilisha hatua zote za
usajili kama mwekezaji wa mradi na kazi
inatarajiwa kuanza wakati wowote
atakapopatiwa hati hiyo.
71. Mheshimiwa Spika, Katika kuyaendeleza
maeneo maalum ya Viwanda (Industrial Parks) kwa kila Mkoa, kwa mwaka wa fedha
2019/2020, Wizara ya Biashara na Viwanda imekamilisha sehemu kubwa ya ulipaji
wa fidia wa eneo la Viwanda la Chamanangwe, jumla ya Wananchi 127 wenye
mashamba madogo na makubwa katika shehia ya Kiuyu na mchanga mdogo wamelipwa.
Pamoja na kuandaa Mpango wa matumizi (Master Plan) wa eneo la Chamanangwe. Pia,
Wizara imefanya uchambuzi wa utendaji wa Viwanda (Industrial Perfomance) kwa
Viwanda saba vya kimkakati vilivyochaguliwa ambavyo ni Kiwanda cha Sabuni
(Inaya Company LTD), Kiwanda cha Sukari Mahonda (Zanzibar Sugar Factory),
Kiwanda cha Maziwa (Azam Diary Milk), Kiwanda cha Mifuko (Turky Mifuko),
Kiwanda cha Tishu (Allawi Supply LTD), Kiwanda cha Chumvi (Swahili Coast Salt
Company) na Kiwanda cha Unga (Zanzibar Milling Company LTD) ili kuviendeleza na
kuvilinda kwa kuainisha changamoto zinazovikabili Viwanda hivyo. Hata hivyo,
kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Wizara inaendelea na kazi hii kwa kuangalia kwa
kina changamoto zilizopo.
72. Mheshimiwa Spika, Wizara imeratibu na
kushiriki katika Maonesho ya 4 ya Bidhaa za Viwanda kwa kushirikiana na Mamlaka
ya Biashara Tanzania (Tan Trade) yaliofanyika kuanzia tarehe 5-9 Disemba, 2019
katika Viwanja vya maonesho vya Mwalimu Nyerere Sabasaba Dar es Salaam. Aidha,
Viwanda vitatu (3) vilishiriki katika maonesho hayo ikiwemo Kiwanda cha Sukari
Mahonda, Kiwanda cha Sabuni (ZANOP) na Kiwanda cha Nguo (Zanzibar Apparel Co
Ltd).
73. Mheshimiwa Spika, Katika kuongeza
thamani kwa bidhaa zinazozalishwa Zanzibar, Wizara imetenga na kuandaa eneo la
ujenzi (Site Plan) kwa ajili ya kusarifu zao la chumvi katika eneo la
Chamanangwe-Pemba. Kwa sasa Kampuni ya Zanzibar Coast Salt Company Limited
tayari imeshaanza kuzalisha kwa majaribio bidhaa ya chumvi za aina nane kwa
matumizi mbali mbali na kuuza katika masoko ya kitalii. Bidhaa hizo zimetengenezwa kwa kuwekwa viungo
mbali mbali na kupewa majina ya Choma, Kichaa, Zabibu, Kali, Nyota, Cheza,
Tikisa na Kila siku. Kwa sasa timu ya wataalamu kutoka Uingereza inaendelea na
kuandaa mpango mkakati wa kuongeza uzalishaji chumvi ili kukidhi mahitaji ya
kiwanda.
74. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kuhamasisha na kusimamia uanzishwaji wa viwanda vingine mbalimbali katika sekta
za chakula, vifaa vya ujenzi na ushoni. Kiambatanisho
Nambari 3 Kinaonesha baadhi ya Viwanda na hatua mbali mbali za uanzishaji
wake kwa kipindi cha mwaka 2019/2020.
75. Mheshimiwa Spika, Kama tunavyoelewa
Wakala wa Kusimamia na Kuendeleza Viwanda Vidogo vidogo, vidogo na vya Kati
(SMIDA) bado ni taasisi mpya na inahitaji Ofisi na eneo la kufanyia kazi. Kwa
sasa imefanya ukarabati wa majengo yalikuwepo hapo Maruhubi. Kwa mwaka 2019/2020,
Wizara ilipanga kujenga Ofisi ya makao makuu ya Wakala katika eneo la Maruhubi.
Napenda kulijulisha Baraza lako kuwa hatua za Zabuni za kumpata Mshauri elekezi
na Mkandarasi zimekamilika. Kwa sasa Serikali inaandaa mkataba ili kazi za
ujenzi ianze mara moja.
76. Mheshimiwa Spika, Wakala kwa
kushirikiana na Taasisi ya Private Agricultural Sector Support (PASS) Trust ya
Tanzania imeingia makubaliano (MoU) ya kuanzisha kituo cha usarifu wa mazao ya
kilimo Zanzibar “Agribusiness Innovation Centre”. Matengenezo ya kituo hicho
tayari yameshaanza katika eneo la Maruhubi. Wakala inatarajia kuanzisha viwanda
vidogo vidogo 25 vya mfano na kukabidhiwa vijana waviendeshe chini ya usimamizi
wa PASS na SMIDA. Aidha, mafunzo ya utengenezaji wa vitambaa vya vikoi, usarifu
wa matunda, utengenezaji wa dawa ya kutakasa mikono (sanitizer) yametolewa na
uzalishaji umeanza kwa wajasiriamali lengo ni kuzalisha bidhaa zenye ubora na
zitakazoweza kuuzika katika masoko ya ndani na nje ya nchi pamoja na mafunzo ya
udhibiti wa fedha za miradi kwa wajasiriamali kwa Unguja na Pemba.
77. Mheshimiwa Spika, Katika kukuza na
kuendeleza vipaji vya ubunifu kwa wajasiriamali, Wakala imeandaa na kufanya
mashindano ya ubunifu kwenye Tamasha la Sita (6) la Biashara lililofanyika
kuanzia tarehe 2-15 Januari, 2020. Jumla ya wabunifu 44 walitembelewa, kati ya
hao wabunifu 30 waliteuliwa kushiriki katika mashindano hayo. Wabunifu tisa (9)
walipata zawadi pamoja na ushauri wa jinsi ya kukuza bunifu zao kwa ajili ya
kuleta tija kwa maendeleo ya Viwanda Zanzibar. Sambamba na kuvitembelea viwanda
185, kuvipatia ushauri wa kitalaamu na kutengeneza mashine tano (5) za
teknolojia rahisi waliopatiwa wazalishaji.
78. Mheshimiwa Spika, Wajasiriamali tisa
(9) wamepatiwa mikopo yenye jumla ya TZS shillingi 100,000,000. Mikopo
iliyotolewa ni kwa ajili ya kununulia mashine ya kutengenezea chakula cha kuku;
Mashine ya kufumia vikoi; Ununuzi wa vifungashio; Ununuzi wa vifaa vya bekari
na Jenereta; Mashine ya kutotolea vifaranga; na Uimarishaji wa kilimo cha
mbogamboga. Jumla ya Shilingi milioni 35.66 tayari zimerejeshwa. Aidha, Wakala
wamefanya makongamano mawili (2) yenye lengo la kujadili changamoto za viwanda
na taasisi zinazohusiana moja kwa moja na wajasiriamali. Matokeo ya makongamano
hayo ni pamoja na kuandaa programu ya pamoja itakayowezesha kuwapatia huduma
wajasirimali wenye viwanda vidogo vidogo na vya kati katika sehemu moja “One
Stop Center” pamoja na “Business
Clinic”.
79. Mheshimiwa Spika, Katika kutatua
changamoto ya vifungashio kwa Wajasiriamali Wakala wameagiza vifungashio 10,000
vya maziwa pamoja na machine 5 za vifungashio, ili kuwasaidia wajasirimali
wenye viwanda wa sekta ya maziwa kuweza kubadilisha vifungashio kama
walivyoelekezwa na Wakala wa dawa na vipodozi Zanzibar (ZFDA). Kadhalika,
Wakala imekamilisha Muundo wa utumishi na muundo wa mishahara ambao unaendana
na Muundo mpya wa Wakala ulioidhinishwa na Serikali.
Programu ndogo ya Maendeleo ya
Ujasiriamali
80. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Maendeleo ya Ujasiriamali ilipangiwa jumla ya shilingi bilioni 3.57kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Hadi kufikia
Machi 2020, programu hii ndogo imeingiziwa jumla ya shilingi milioni 21.11 kwa kazi za kawaida, sawa na asilimia 1 ya makadirio ya mwaka. Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza
hapo awali kuwa fedha za miradi zilizotarajiwa katika program hii ndogo ni
kutoka washirika wa maendeleo (Khalifa fund) ambazo hazikupatikana kwa mwaka
huu wa fedha. Utekelezaji wa program ndogo ya Maendeleo ya
Ujasiriamali
ulikuwa kama ifuatavyo:-
Kutoa msaada kwa Wajasiriamali
81. Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha
rasimu ya mapitio ya Sera ya Maendeleo ya Ujasiriamali (MSME’s) ambapo mapitio
yake yamezingatia mambo mapya
yanayokwenda sambamba na wakati na mabadiliko ya kiujasiriamali yanayotokea
duniani, pamoja na kutoa muongozo wa kuendeleza na kusimamia sekta ya
ujasiriamali nchini kupitia mikakati mipya iliyowekwa.
82. Mheshimiwa Spika, Katika kusimamia
utekelezaji wa sera ya SME’s Wizara imefanya vikao viwili vya Kamati ya ushauri
ya Ujasiriamali ambayo inaundwa na wajumbe kutoka sekta ya umma na sekta
binafsi. Kupitia vikao hivyo wajumbe walijadiliana juu ya kazi za wajasiriamali
na mafanikio yao, changamoto wanazokumbana nazo pamoja na kutoa ushauri
serikalini juu ya namna bora ya kuendeleza sekta ya ujasiriamali. Pamoja na hayo, imeonekana kwamba kuna mwamko
mkubwa wa wananchi hasa vijana kujiajiri katika shughuli za ujasiriamali hasa
kilimo na uzalishaji bidhaa. Miradi ya wajasiriamali imeanzishwa kwa ushirika
au vikundi vya uzalishaji.
83. Mheshimiwa Spika, Jumla ya miradi 100
ya vikundi vya Wajasiriamali na wenyeviwanda vilikaguliwa ikiwemo miradi ya
uzalishaji viungo, chumvi, sabuni, uhunzi, utengenezaji matofali na kokoto,
miradi ya viwanda vya useremala, wazalishaji dagaa, maji na vyakula kwa ajili
ya kupatiwa ushauri wa kitaalamu na kukusanya taarifa zao. Lengo ni kufanya
ufuatiliaji na kutathmini hali ya sasa ya sekta ya viwanda kwa mwaka 2019/2020
ukilinganisha na mwaka uliopita 2018/2019 pamoja na kuainisha changamoto zao.
Ukaguzi ulionesha, Viwanda 70 kati ya hivyo vipo katika uzalishaji wa bidhaa
(manufacturing/processing) na 30 vipo katika uchimbaji (mining and quarying).
Asilimia 95 ya viwanda hivyo vinamilikiwa na wazawa vimeajiri wafanyakazi
wapatao 1,359 na asilimi 5 iliyobaki ya Viwanda vinamilikiwa na wageni
vimeajiri wafanyakazi 90.
84. Mheshimiwa Spika, Sekta ndogo ya
uchimbaji katika viwanda vinavyotegemea malighali ya mchanga, jasi na kokoto kwa mwaka 2019/2020 imeshuka kutoka
TZS Bilioni 6.23 mwaka 2018/2019 hadi TZS Billioni 4.48 mwaka 2019/2020 sawa na
upungufu wa asilimia 28. Aidha, idadi ya ajira imeshuka kutoka wafanyakazi 325
mwaka 2018/2019 hadi wafanyakazi 256 mwaka 2019/2020 sawa na anguko la asilimia
21, hali hiyo imetokana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ndogo ya
uchimbaji (mining and quarying).
PROGRAMU
KUU YA UKUZAJI NA UENDELEZAJI WA BIASHARA:
85. Mheshimiwa Spika, Programu kuu ya
Ukuzaji na Uendelezaji wa Biashara inajumuisha Programu ndogo nne (4) ambazo ni
Ukuzaji wa Masoko na Usafirishaji, Ushindani Halali wa Kibiashara na Kumlinda
Mtumiaji, Urahisishaji wa Biashara na Ukuzaji Biashara za Ndani pamoja na
Usajili
wa Biashara na Mali. Programu hii
ilipangiwa matumizi ya shilingi bilioni
3.03 kwa mwaka wa fedha 2019 /2020. Hadi kufikia Machi 2020, programu hii
imeingiziwa jumla ya shilingi bilioni
1.79 ikiwemo mishahara, ruzuku, miradi na kazi nyengine za uendeshaji, sawa
na asilimia 59 ya makadirio ya
mwaka. Utekelezaji wa kazi zilizopangwa katika kila program ndogo nilizozitaja
ni kama ifuatavyo:
Programu ndogo ya Ukuzaji wa
Masoko na
Usafirishaji
86. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Ukuzaji wa
Masoko na
Usafirishaji inasimamiwa na Idara ya Biashara na Masoko. Huduma ambazo
zimesimamiwa na kutekelezwa na Programu hii ndogo ni uimarishaji wa mazingira
mazuri ya biashara pamoja na kuongeza Fursa za Masoko na Urahisishaji Biashara.
Program hii ndogo ilipangiwa jumla ya shilingi milioni 754.86 kwa mwaka wa
fedha 2019/2020. Hadi kufikia Machi 2020, programu hii ndogo imeingiziwa jumla
ya shilingi milioni 393.45 kwa ajili
ya mishahara, kazi za maendeleo na kazi nyengine za kawaida sawa na asilimia 52 ya makadirio ya mwaka.
Utekelezaji wa huduma za program ndogo hii ni kama ifuatavyo;
Fursa za Masoko na Urahisishaji Biashara
87. Mheshimiwa Spika, Mojawapo ya jukumu
muhimu la
Wizara ya Biashara na Viwanda ni kuzitafutia masoko bidhaa
zinazozalishwa nchini pamoja na kuangalia changamoto zilizopo katika masoko
hayo. Katika hatua tunazozichukua ni kuandaa, kuratibu na kushiriki katika
maonesho na matamasha mbalimbali. Kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Wizara
iliratibu ushiriki wa Zanzibar katika maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara
(sabasaba) yaliyofanyika Dar es Salaam mwezi wa Julai 2019. Taasisi saba (7) za
Serikali zilishiriki katika maonesho hayo ambazo ni Shirika la Taifa la
Biashara (ZSTC), Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS), Shirika la Bima la Zanzibar
(ZIC), Kamisheni ya Utalii (ZCT), Mamlaka ya Ukuzaji Vitega Uchumi ya Zanzibar
(ZIPA), Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokotoni, Wakala wa Maendeleo ya Viwanda
vidogo vidogo na vya Kati (SMIDA) pamoja na wajasiriamali 37 kutoka Unguja na
Pemba. Bidhaa ambazo zilioneshwa na wajasiriamali walioshiriki katika maonesho
hayo ni pamoja na bidhaa za kusindika, vyakula vikavu, kazi za mikono, sabuni,
dawa za asili, bidhaa za viungo (spices), mafuta ya mimea na nyenginezo. Aidha,
Maonesho ya Sabasaba yaliweza kutoa fursa kwa wajasiriamali wetu kutangaza
bidhaa zao na kuweza kupata wateja wengi zaidi.
88. Mheshimiwa Spika, Katika kuhakikisha
kuwa wafanyabiashara na wajasiriamali wanapata masoko ya uhakika ya bidhaa zao,
Wizara pia iliratibu na kutayarisha Tamasha la Biashara ambalo hufanyika kila
mwaka ifikapo Januari ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha sherehe za Mapinduzi ya
Zanzibar. Kwa mwaka huu Tamasha hili lilikuwa ni la sita ambalo lilijumuisha
jumla ya washiriki 389 kati ya hao, kutoka Tanzania bara 51, Kenya 3, Burundi
4, Rwanda 6, Uganda 1, Misri 2 na Uturuki 1. Mauzo yaliyofanyika katika Tamasha
hilo ni wastani wa Shilingi milioni
954.68
Aidha, Tamasha hilo la sita (6) la
biashara, Wizara pia iliandaa majadiliano katika siku maalum 3 zilizowekwa kwa
madhumuni ya kutoa nafasi kwa wafanyabiashara na Taasisi kuweza kujadiliana
kuhusiana na ukuzaji wa sekta ya biashara. Siku hizo ni siku ya Ubunifu
(Innovation Day), Siku ya bidhaa za kimkakati
na Kliniki ya Biashara ambapo ilizinduliwa rasmi siku hiyo. Lengo kuu la
kuweka siku hizi ni kuweza kuwakutanisha watumiaji, wazalishaji wa bidhaa
pamoja na Taasisi zinaohusika na maswala ya biashara na uzalishaji kufanya
majadiliano, kuibua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara na wazalishaji,
na kutoa mapendekezo katika kuboresha sekta ya biashara na uzalishaji nchini.
Aidha majadiliano hayo yameweza kutoa miongozo na maelekezo mbali mbali ambayo
yatawasaidia wazalishaji kwa ujumla.
89. Mheshimiwa Spika, Vile vile, Wizara
imeratibu na kushiriki katika maonesho ya biashara ya kusherekea kutimia miaka
20 ya maonesho ya Kikanda ya Jua kali/Nguvu Kazi yaliyofanyika Fumba Zanzibar
kuanzia mwezi Novemba, 2019. Madhumuni ya maonesho haya ni kuhakikisha kuwa
Wajasiriamali wanapata fursa za kuzitangaza bidhaa zao katika masoko ya Afrika
Mashariki. Zaidi ya Wajasiriamali 120 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
walishiriki katika maonesho haya ambayo hufanyika kila mwaka katika mojawapo ya
nchi katika Jumuiya.
90. Mheshimiwa Spika, Wizara katika hatua
ya kuimarisha Mashirikiano ya kibishara ya Kikanda na Kimataifa imeweza
kushiriki katika mikutano mbali mbali ya kikanda na kimataifa yanayohusiana na
maswala ya Biashara ambapo Mikutano hiyo ni pamoja na vikao vya majadiliano ya
uanzishwaji wa biashara huru barani Afrika (Continental Free Trade Africa), vikao
vya itifaki ya biashara ya huduma Afrika Mashariki, vikao vya kuondosha vikwazo
visivyo vya kiushuru (NTBs), vikao vya urahisishaji biashara (Trade
Facilitation), vikao vya usimamiaji wa maswala ya TBT na SPS kwa lengo la kurahisisha ufanyaji biashara katika
soko la kikanda na Kimataifa. Katika mikutano fursa na changamoto mbali za
kibiashara za kikanda na kimataifa ziliweza kujadiliwa na baadhi yake kupatiwa
maamuzi katika ngazi za Wakuu wa Nchi.
91. Mheshimiwa Spika, Katika kufanya
majadiliano ya bei za bidhaa muhimu Wizara ya Biashara na Viwanda imeweza kufanya mikutano
mbalimbali na Wafanyabiashara wakubwa, wa kati na wadogo ili kuweza kujadiliana bei za bidhaa muhimu kwa lengo la kuweka bei ambayo
itakidhi kwa kila mfanyabiashara bila ya kumbana mwananchi. Mheshimiwa Spika,
kutokana na majadiliano haya na wafanyabiashara, kumekuwepo na utulivu wa bei
kwa bidhaa muhimu za chakula kama vile mchele, sukari, mafuta ya kupikia na
unga wa ngano. Aidha, Wizara imeratibu uanzishwaji wa Kamati ya mashauriano ya
kibiashara pamoja na vikao vyake. Kamati hio imeshirikisha wataalam kutoka
ZFDA, ZBS, Idara ya Biashara na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) ili kuweza kutoa
ushirikiano pamoja na mashauriano ya kibiashara.
92. Mheshimiwa Spika, Katika hatua nyengine
ya kuhakikisha kuwa tunakuwa na eneo maalum la kudumu la kuonesha na kutangaza
bidhaa za wajasiriamali hapa nchini, Wizara ya Biashara na Viwanda inaendelea
kulitangaza eneo la Nyamanzi kwa ajili hiyo. Kwa kipindi hiki, Serikali kwa
kushirikiana na Benki ya Dunia imefanya upembuzi yakinifu (feasibility study)
na kuandaa ripoti ya matumizi ya eneo pamoja na kupata gharama za uwekezaji wa
Kiwanja hicho. Mradi huu unategemewa kutekelezwa kwa utaratibu wa mashirikiano
baina ya Serikali na sekta Binafsi (PPP).
93. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Biashara na
Viwanda kwa kushirikiana na Tume ya Mipango pamoja na MKURABITA imetoa mafunzo
kwa wajasiriamali 210 walioko katika Wilaya ya Magharibi ‘B’, Unguja, na Wilaya
ya Wete Pemba. Mafunzo hayo yamewalenga wajasiriamali kupata uwelewa kuhusiana
na umuhimu wa kusajili biashara zao ili kuweza kutambulika kisheria na kuweza
kupata fursa zinazopatikana katika kuendesha biashara kwa mfumo rasmi.
Programu ndogo ya Ushindani Halali wa
Kibiashara na Kumlinda Mtumiaji
94. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Ushindani Halali wa Kibiashara na Kumlinda Mtumiaji inasimamiwa na Idara ya
Biashara (Kitengo cha Mizani na Vipimo) na Tume ya Ushindani Halali wa
Biashara. Program ndogo hii ilipangiwa jumla ya shilingi milioni 344.81 kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Hadi kufikia
Machi 2020, programu hii imeingiziwa jumla ya shilingi milioni 219.72 kwa ajili ya mishahara na kazi nyengine za
kawaida sawa na asilimia 64 ya
makadirio ya mwaka.
Uimarishaji
Ushindani Halali wa Kibiashara
95. Mheshimiwa Spika, Tume ya Ushindani
Halali wa
Biashara na Kumlinda Mtumiaji (ZFCC) ni
Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria Namba 5 ya mwaka 2018. Lengo la Taasisi ni kuhamasisha, kuimarisha na kulinda Ushindani
halali wa Biashara na kumlinda Mtumiaji hapa Zanzibar kwa kuhakikisha kwamba
kila muekezaji, mwenye kiwanda, mfanyabiashara na mjasiriamali anafanya shughuli
zake bila ya kumkwaza mwengine kwa ajili ya ustawi wa uchumi wa Zanzibar.
96. Mheshimiwa Spika, Katika kuzitekeleza
shughuli zilizopangwa kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Tume ilipangiwa jumla ya TZS Shilingi milioni 145.0. Hadi
kufikia Machi 2020 jumla ya TZS Shilingi
milioni 92.8 ziliingizwa sawa na asilimia
64 ya matumizi kwa kipindi hicho.
97. Mheshimiwa Spika, Katika kuimarisha
ushindani halali wa kibiashara kwa maeneo ya biashara, Wizara ya Biashara na
Viwanda imesimamia miungano ya Makampuni ambapo jumla ya taarifa za miungano
sita (6) ya Makampuni zimefanyiwa kazi kwa kipindi hiki. Kati ya hizo, Mheshimiwa Spika, Taarifa za miungano
kwa Makampuni matatu (3) zimekamilika na kuidhinishwa. Kadhalika, Tume
imeendelea kutatua migogoro ya wafanyabiashara inayohusu ushindani wa
kibiashara usio halali katika maeneo ya kughushi, kutumia jina na muonekano
ambayo huathiri ushindani wa soko. Malalamiko hayo yamefanyiwa kazi na kutolewa
maamuzi ya umiliki halali wa majina na muonekano wa biashara hizo.
98. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Biashara na
Viwanda inajukumu la kumlinda mtumiaji kutokana na bidhaa bandia zilizopo
sokoni. Wizara kupitia Tume imefanya ukaguzi wa bidhaa mbali mbali katika
maeneo ya biashara na bandarini. Ukaguzi
huo ulilenga kuangalia utambulisho wa bei na ubora wa bidhaa, maelezo ya bidhaa,
dhamana kwa watumiaji, bei elekezi kwa
bidhaa zinazodhibitiwa, udhibiti wa bidhaa
bandia, bidhaa zisizo salama na Mikataba kwa Watumiaji. Katika ukaguzi
huo jumla ya maduka ya kawaida 341, maghala 30, bekari 5 na maduka makubwa
(Supermarket) 10 yamekaguliwa. Katika ukaguzi huo bidhaa zenye thamani ya
shilingi milioni 17,217,000 zikiwa zimepitwa na muda wa matumizi zimekosa
maelezo ya utumiaji na bidhaa bandia zilikamatwa na kuondolewa madukani. Bidhaa
hizo ni pamoja na vyakula (nafaka na
juisi) na
kemikali. Vile vile Tume kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)
imeharibu bidhaa za kuchezea watoto zenye kemikali hatarishi zinazoweza
kusababisha miripuko katika eneo la Unguja Ukuu Zanzibar.
99. Mheshimiwa Spika, Kwa kutambua umuhimu
wa sekta ya biashara katika kukuza uchumi pamoja na kuhakikisha utekelezaji wa
majukumu unakwenda sambamba kwa mujibu wa mipango tuliojipangia, Tume imeandaa
Muundo wa taasisi, muundo wa utumishi, Mpango Mkakati wa miaka mitano (5)
pamoja na kuwapatia mafunzo wafanyakazi ili kuhakikisha kuwa sekta ya biashara
inaleta tija na maendeleo yaliyotarajiwa.
Ukaguzi wa Mizani na Vipimo
100. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Biashara
imefanya mapitio ya sheria na kanuni mbali mbali za biashara kwa lengo la
kuweka utaratibu mzuri wa usimamizi wa masuala ya biashara nchini. Mojawapo ya
sheria muhimu iliyoandaliwa na kuwasilisha Serikalini ni Sheria ya Mizani na
Vipimo ambapo sheria hiyo inapendekeza kuanzisha kwa Wakala wa vipimo ili
kuongeza ufanisi katika kazi za uhakiki na ukaguzi wa vipimo katika maeneo yote
yaliyoanishwa na sheria hii.
101. Mheshimiwa Spika, Mbali na ukaguzi wa
mizani na vipimo vya mafuta katika vituo, magari, matangi na pampu, Wizara ya
Biashara na Viwanda imeanza kuongeza kazi zake za ukaguzi na kwa sasa, ukaguzi
unafanyika katika bidhaa zinazozalishwa katika viwanda mbali mbali vilivyopo
hapa Zanzibar ili kuhakikisha vipimo vinavyotumika vinafanyika kwa usahihi.
Katika ukaguzi wa vipimo hivi, jumla ya shilingi 60,370,000 zimekusanya ikiwa
ni ada inayotokana na ukaguzi huo. Idadi ya huduma za ukaguzi zilizofanywa kwa
kipindi cha mwaka 2019/2020 inaonekana katika
kiambatanisho namba 4.
Programu ndogo ya Urahisishaji Biashara na
Ukuzaji Biashara za Ndani
102. Mheshimiwa Spika, Program ndogo ya
Urahisishaji Biashara na Ukuzaji Biashara za Ndani inatekelezwa na Baraza la
Kusimamia Mfumo wa Utoaji Leseni (BLRC) na Baraza la Taifa la Biashara (ZNBC)
ambapo ilipangiwa kutumia jumla ya shilingi
bilioni 1.11 kwa mwaka wa fedha
2019/2020. Hadi kufikia Machi 2020, programu hii ndogo imeingiziwa jumla ya shilingi milioni 622.91 kwa ajili
matumizi ya kazi za kawaida, ruzuku na kazi za maendeleo sawa na asilimia 56 ya makadirio ya mwaka.
Programu ndogo ya Urahisishaji Biashara na Ukuzaji Biashara za Ndani ina jukumu
la kutekeleza huduma zifuatazo:-
Usimamizi wa Mamlaka zinazotoa Leseni
103. Mheshimiwa Spika, Huduma hii
ilitekelezwa na Baraza la kusimamia Mfumo wa Utoaji Leseni ambalo lilipangiwa
matumizi ya jumla ya shilingi milioni 745.5 kwa kipindi cha mwaka wa fedha
2019/2020 ambapo shilingi milioni 345.5
kwa ajili ya kazi za kawaida na shilingi
milioni 400 kwa kazi za maendeleo. Hadi kufikia Machi 2020, Baraza
liliingiziwa jumla ya shilingi milioni
288.2 kwa matumizi ya kazi za kawaida na kazi za maendeleo sawa na asilimia 39 ya makadirio ya mwaka.
104. Mheshimiwa Spika, Baraza limefanya
utafiti wa kutathmini Mfumo wa Utoaji leseni mwaka 2019. Utafiti umeonesha
kwamba taratibu za utoaji leseni
zimepungua kutoka hatua kumi (10) za
awali na kufikia hatua tatu mpaka nne (3 – 4)
katika utoaji wa leseni za
utalii, usafiri, kazi za sanaa na wasanii, biashara, mazao ya kilimo na mifugo,
vibali vya ujenzi na usalama wa chakula, vibali vya usafirishaji, uvuvi,
nishati na mawasiliano. Aidha, leseni
zinazohusiana na uendeshaji wa hospitali, uvuvi wa bahari kuu, huduma za
bandari na uwekezaji zinatumia hatua nne
mpaka tano (4 -5) katika utoaji wa leseni na vibali. Vile vile, utafiti
unaonesha kwamba leseni za utalii, usafiri, kazi za sanaa na wasanii, biashara,
mazao ya kilimo na mifugo, vibali vya ujenzi na usalama wa chakula zinatolewa
ndani ya siku moja (1).
105. Mheshimiwa Spika Katika kuhakikisha
usimamizi wa Mamlaka zinazotoa leseni unasimamiwa ipasavyo, Baraza imefanya
vikao vinne (4) vya Baraza na vikao viwili (2) vya Kamati na kujadili ripoti za
utekelezaji, mapitio ya sheria, mapitio ya ada na tozo za leseni na huduma
nyenginezo
kwa lengo la
kutathmini utekelezaji wa majukumu ambao unaimarisha mfumo wa upatikanaji wa
leseni. Aidha, Vikao vitatu (3) vya majadiliano vya sekta binafsi na Mamlaka
vimeitishwa ambavyo vilijadili mapitio ya ada na tozo za leseni na huduma
nyenginezo ili kuhakikisha kwamba utaratibu wa utoaji leseni unaendana na
Sheria ya kusimamia utoaji leseni na kanuni zake. Aidha, Wajumbe kumi (10) na
wafanyakazi wa watano (5) wa Baraza wamepatiwa mafunzo yanayohusiana na mfumo
wa utoaji leseni, sheria, kanuni za Baraza na urahisi wa ufanyaji biashara.
106. Mheshimiwa Spika, Katika kuweka
mazingira wezeshi ya ufanyaji kazi, Baraza limefanya matengenezo ya vyombo vya
usafiri, ununuzi wa huduma za umeme, mafuta na vifaa vya ofisi.
Uimarishaji wa Mashirikiano baina ya Sekta
ya Umma na Sekta Binafsi
107. Mheshimiwa Spika, Katika juhudi za
Serikali kuhakikisha kwamba inajenga Sekta binafsi iliyokuwa imara imeanzisha
Chombo maalum ambacho kimeweka misingi ya kufanya majadiliano baina ya Sekta ya
Umma na Sekta Binafsi. Chombo hicho (Baraza la Taifa la Biashara la Zanzibar -
ZNBC) kilianzishwa
na Sheria iliyopitishwa na Baraza lako Tukufu Namba 10 ya mwaka 2017. Katika
kipindi cha mwaka 2019/2020 Baraza la Taifa la Biashara la Zanzibar lilipangiwa
kutumia Jumla ya shilingi milioni 360.0kama
ni ruzuku kwa kazi za kawaida ambapo hadi kufikia mwezi wa Machi, 2020 jumla ya
shilingi milioni 334.71 zilipatikana
sawa asilimia 93.
108. Mheshimiwa Spika, Naomba kuliarifu
Baraza lako Tukufu kwamba Baraza liliratibu mikutano kumi ya Mabaraza ya
Biashara katika Mikoa yote mitano ya Zanzibar. Aidha, vikao vitano vya Kamati
Tendaji ya Baraza vilikutana kwa ajili ya kupitia utekelezaji wa maazimio
yaliyofikiwa katika Jukwaa la Tisa la Biashara pamoja na kufanyika kwa mikutano
ya Kamati za Baraza la Biashara. Baraza pia linaendelea kufanya mapitio ya Sheria Nam. 10 ya mwaka 2017, ili iweze
kukidhi mahitaji mapya yaliyojitokeza wakati wa utekelezaji wake.
109. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Biashara na
Viwanda imeandaa Mkutano wa Tatu wa Baraza la Taifa la Biashara ambao unatakiwa
kufanyika mara moja kwa mwaka. Mkutano huo ulifanyika chini ya Mwenyekiti wake
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi. Mkutano ulihudhuriwa na wajumbe wote kutoka Sekta ya Umma pamoja na
wajumbe kutoka Sekta Binafsi. Aidha, baada ya kukamilika kwa Mkutano huo,
Jukwaa la Kumi la Biashara lilifanyika na kuhudhuriwa na washiriki wasiopungua
350, kutoka katika Taasisi za Serikali, taasisi za Sekta binafsi, Mabalozi
pamoja na waalikwa wengine kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
110. Mheshimiwa Spika, Jukwaa la kumi la
Biashara ambalo lilikuwa na Kauli mbiu isemayo “Maendeleo Endelevu ya Zanzibar
Kupitia Uchumi wa Bahari (Buluu)” , lilikuja na maazimio 14. Maazimio hayo
yalijikita katika maeneo ya uimarishaji wa ulinzi katika bahari kuu, kuandaliwe
Sheria ambayo itaweka mfumo mzuri wa usimamizi na ufuatiliaji wa michango
inayotolewa na wawekezaji na wafanyabiashara (CSR), kuanzisha Mkakati wa
kupeleka huduma za kifedha ikiwemo matawi ya benki na ATM ndani ya kilomita 5
ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wateja na wananchi, Serikali ifungue
‘refund account’ au iweke utaratibu mwengine ulio bora wa marejesho ya VAT kwa
wafanyabiashara na maazimio mengine yanayohusu kodi.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeanza kufuatilia utekelezaji wa
maazimio hayo yaliyofikiwa katika Jukwaa hilo la Kumi la Biashara.
Programu ndogo ya Usimamizi wa
Usajili wa
Biashara na Mali
111. Mheshimiwa Spika, Huduma hii
ilitekelezwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali (BPRA) ambayo ilipangiwa
matumizi ya jumla ya shilingi milioni
820.9 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 na hadi kufikia Machi 2020,
Wakala iliingiziwa jumla ya shilingi
milioni 550.99 kwa matumizi yakiwemo ya kazi za kawaida na matumizi
mengineyo sawa na asilimia 67 ya
makadirio ya mwaka.
112. Mheshimiwa Spika, Lengo kuu la
kuanzishwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali Zanzibar (BPRA) ni kufanya
usajili wa biashara na mali ikijumuisha hati za mali ubunifu pamoja na usajili
wa nyaraka mbalimbali zinazowahusu wananchi na wageni wanaofanya shughuli zao
Zanzibar. Kwa kipindi cha Julai hadi Machi 2019/2020, BPRA imeweza kusajili
Kampuni 636, Majina ya Biashara 884,
Alama za biashara 519 na Nyaraka 791.
113. Mheshimiwa Spika, Katika kuimarisha
uwezo wa watendaji wa kutekeleza majukumu ya kazi ikiwemo usajili, uhifadhi
kumbukumbu na utoaji wa taarifa (information services) kwa kutumia TEHAMA,
wafanyakazi 2 wamepatiwa mafunzo ya muda mrefu katika fani ya “Tehama” na
“Intellecttual Property and Development
Policy” (MIPD) na Wafanyakazi 2 wamepatiwa mafunzo ya muda mfupi ya
“Umuhimu na
wajibu wa ukusanyaji wa mapato” na “Audit Tax International”. BPRA imekamilisha
rasimu ya awali ya mapitio ya sheria ya ufilisi (Insolvency) kwa sasa rasimu
hiyo iko katika hatua ya kutafsiriwa kwa lugha ya kiswahili, rasimu ya sheria
ya ubia (Partnership) pamoja na kufanya marekebisho ya sheria ya Usajili wa
taasisi za biashara. Aidha, BPRA imeshiriki katika uzinduzi wa program mpya ya
shahada ya pili ya Mali ubunifu (Intellectual Property) katika chuo kikuu cha
Dar es Salaam.
114. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa
kuhamasisha wananchi kufanya usajili wa kisasa wa kutumia mfumo wa usajili wa
mtandao (Online Registration System), Wizara ya Biashara na Viwanda kupitia
BPRA imetoa elimu kuhusu usajili wa mali bunifu, usajili wa dhamana za mali
zinazohamishika na usajili wa taasisi za biashara kupitia ZBC-TV. Pamoja na
kufanya mikutano na wadau ya kuhamasisha uingizaji taarifa kwa waliosajiliwa
kabla ya kuanza kutumika mfumo wa usajili kwa njia ya mtandao kwa Unguja na
Pemba.
PROGRAMU
KUU YA VIWANGO NA TATHMINI YA UBORA:
115. Mheshimiwa Spika, Programu kuu ya
Viwango na Tathmini ya Ubora inasimamiwa na Taasisi ya Viwango Zanzibar,
inajumuisha Programu moja ndogo ambayo ni Viwango na Uthibiti wa Ubora.
Programu hii ilipangiwa matumizi ya shilingi
bilioni 2.72 kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Hadi kufikia Machi 2020,
programu hii imeingiziwa jumla ya shilingi
bilioni 1.07 ambayo ni ruzuku ya
mishahara ya kazi za kawaida na kazi za maendeleo sawa na asilimia 39 ya makadirio ya mwaka. Utekelezaji wa huduma
zilizopangwa katika program ndogo niliyoitaja hapo juu ni kama ifuatavyo:
Uandaaji na Ukuzaji wa Viwango
116. Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Viwango
imeendelea na jukumu lake la kuandaa viwango ambapo jumla ya viwango 103
vimeandaliwa na kuidhinishwa sawa na asilimia
172 ya lengo la uandaaji viwango. Viwango hivyo ni pamoja
na viwango vya
chakula 31, Uhandisi mitambo 11, vifaa vya ujenzi 3, Kemikali 29, Umeme 9,
Mazingira 11, Utalii 3 na nishati 4. ZBS imeendelea na kazi yake ya uchunguzi
wa kimaabara ili kuhakikisha ubora wa bidhaa ambapo sampuli 662 zimekusanywa na
kupelekwa maabara kwa hatua za upimaji wa ubora. Matokeo ya ripoti hizo
yameonesha kwamba sampuli 528 zimekidhi
vigezo, sampuli 60 zimebainika kutokidhi vigezo na sampuli 74 bado hazijapatiwa
majibu.
Ukaguzi na udhibiti ubora
117. Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Viwango
imefanya ukaguzi wa bidhaa na imefanikiwa kutoa Vyeti vya ubora wa bidhaa 876
na magari yaliyotumika 34 kwa mfumo wa ukaguzi nje ya nchi (PVoC). Jumla ya
shehena 2,155 za mizigo na gari 4,516 zimekaguliwa kupitia mfumo wa ukaguzi wa
ndani ya nchi (DI). Aidha, shehena 120 za mafuta ya nishati zimekaguliwa, kati
ya hizo shehena 42 za Dizeli, 37 za Petroli, 28 za mafuta ya taa na 13 za
mafuta ya ndege (Jet A1). Katika hatua za kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa na
zinazoingia nchini zimezingatia viwango katika nchi yetu, ZBS imepokea maombi
24 ya Uthibiti Ubora wa bidhaa pamoja na matumizi ya alama ya ubora. Kwa
kipindi cha Julai – Machi Taasisi imetoa leseni 7 za alama ya ubora kwa bidhaa
mbalimbali zinazozalishwa nchini na nje ya nchi na hatua za ufuatiliaji
zinaendelea kwa maombi ya bidhaa zilizobakia.
Uthibiti
wa Ubora wa Bidhaa
118. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
mradi wa Maendeleo wa kuimarisha Taasisi yetu ya viwango, imefanya ununuzi wa
vifaa vya maabara ya chakula na tayari vimeshafungwa pamoja na kutoa mafunzo
kwa wafanyakazi juu ya utumiaji wa vifaa hivyo. Hivyo, kufanya jumla ya maabara
tatu zinazotoa huduma hapo eneo la Amani kukamilika. Aidha,awamu ya pili ya
ujenzi wa Ofisi na Maabara katika eneo la Maruhubi unatarajiwa kuendelea baada
ya kukamilisha taratibu za Zabuni. Kwa upande wa Pemba matengenezo ya Ofisi ya
Mkoani na Chake Chake yamekamilika ikiwa ni pamoja na kuwekewa mazingira mazuri
ya kiutendaji na kuanza kutoa baadhi ya huduma za msingi.
SHIRIKA
LA BIASHARA LA TAIFA (ZSTC):
119. Mheshimiwa Spika, Shirika la Biashara
la Taifa (ZSTC) lilifanyiwa mageuzi makubwa ya kiuendeshaji chini ya Sheria
Namba 11 ya 2011, ambayo imelipa uwezo Shirika kukuza, kuendeleza na kusimamia
sekta nzima ya karafuu pamoja na mazao mengine ya kilimo hususani mazao ya
viungo, pamoja na kuanzisha Sheria ya Maendeleo ya Mfuko wa Karafuu Namba 2 ya
mwaka 2014. Huduma zilizotekelezwa kwa mwaka 2019/2020 ni kama zifuatazo:
Uvunaji
na Usafirishaji Karafuu:
120. Mheshimiwa Spika, Shirika liliendelea
kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Mpango Mkakati wa Shirika (Corporate
Strategic Plan) ambao uliweka dhamira ya utekelezaji wa Mpango wa Mageuzi wa
miaka 10 kuanzia 2011 hadi 2021. Kwa mwaka wa fedha 2019/20 Shirika
lilijipangia kununua jumla ya tani 5,100 za karafuu ukilinganisha na mwaka
2018/2019 ambapo lilipanga kununua tani 3,000 na tani 1000 za makonyo. Hadi
kufikia tarehe 31/03/2020 Shirika limenunua jumla ya tani 4,361.8 zenye thamani
ya shilingi bilioni 61.0 na Makonyo
tani 624.06 yenye thamani ya Shilingi milioni
926.2.
121. Mheshimiwa Spika, Shirika bado
linaendelea kununua Karafuu kwa bei ya TZS 14,000, TZS 12,000 na TZS 10,000 kwa
kilo za daraja la kwanza, pili na tatu. Aidha,kwa mwaka wa fedha 2019/2020
Shirika limefanya mauzo ya tani 5,640 za karafuu zenye thamani ya USD
26,661,620 sawa na Shilingi bilioni
61.05 kwa nchi ya India na Singapore.
Uzalishaji wa Mafuta ya Makonyo na Mimea
122. Mheshimiwa Spika, Shirika limefanikiwa
kuzindua mtambo mpya wa uzalishaji wa mafuta ya Mkaratusi katika kiwanda cha
mafuta ya Makonyo na Arki za mimea Wawi Pemba. Uzinduzi huo ulifanyika tarehe
6/01/2020 ambapo mgeni rasmi alikuwa Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamo wa
pili wa Rais wa Zanzibar. Vile vile, Shirika limefanikisha mpango wa kuanzisha
kiwanda cha kuchakata majani makavu ya karafuu kwa ajili ya kupata mafuta
kilichojengwa eneo la Mgelema huko Pemba na tayari kimeanza uzalishaji. Kiwanda
hiki ni makubaliano ya mkopo nafuu baina ya ZSTC na Kampuni ya INDESSO ya
nchini Indonesia.
123. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa
matumizi kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Kiwanda cha Makonyo kilijipangia kutumia
jumla ya shilingi bilioni 1.0 hadi
kufikia tarehe 31/03/2020 Kiwanda cha Makonyo kimetumia jumla ya shilingi milioni 539.3 sawa na asilimia 53.9 ya makadirio ya mwaka.
Uzalishaji wa mafuta kwa Kiwanda cha Makonyo ni kama inavyoonekana katika Kiambatanisho namba 5.
Mapato
na Matumizi ya Shirika
124. Mheshimiwa Spika, Shirika lilipanga
kukusanya shilingi bilioni 76.6 kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato
ikiwemo mauzo ya mafuta ya mimea, ukodishaji wa ukumbi na nyumba za wageni
pamoja na mapato kutoka Shamba la Mtakata. Hadi kufikia tarehe 31/03/2020 jumla
ya shilingi bilioni 53.8 zimekusanywa kutoka kwa vyanzo hivyo vya
mapato sawa na asilimia 70 ya
makadirio ya mwaka.
125. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa
matumizi, Shirika lilikadiria kutumia jumla ya shilingi bilioni 14.1 ikiwa ni gharama mbali mbali za uendeshaji,
wakati matumizi halisi kwa kipindi cha Julai-Machi, 2019/2020 ni shilingi bilioni
7.1.
Mradi
wa PiliPili
126. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa mradi
wa kuwapatia ajira vijana kupitia kilimo cha pilipili, Serikali iliunda Kamati
Maalum ya kufanya tathimini ya utekelezaji wake. Baada ya uwasilishaji wa
ripoti ya Kamati, Serikali ilitoa uamuzi wa kukabidhiwa mradi wa pilipili kwa
Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa uratibu na kuendelea na hatua
za utekelezaji kwa kuzingatia kuwa walengwa wa Mradi huu ni Vijana.
5 CHANGAMOTO ZA UTEKELEZAJI WA MALENGO KWA
MWAKA 2019/2020:
127. Mheshimiwa Spika, Pamoja na mafanikio
makubwa katika utekelezaji wa malengo na majukumu mbali mbali ya Wizara kwa
mwaka 2019 /2020, pia zipo changamoto zilizoathiri utekelezaji wa malengo
yaliyopangwa katika sekta ya biashara na viwanda. Miongoni mwa changamoto
hizo ni kama ifuatavyo:-
i. Kushuka kwa bei ya Karafuu katika soko
la Dunia ii. Vikwazo vya kibiashara katika soko la Tanzania Bara iii.
Kutokuwepo na eneo la kuandaa Tamasha na maonesho mbali mbali hapa Zanzibar.
iv. Kutokuwa na mfumo rasmi wa
ukusanyaji wa Takwimu za Biashara na Viwanda.
128. Mheshimiwa Spika, Kupitia Baraza lako,
Wizara inawaomba wadau wote wa biashara na viwanda wakiwemo wananchi, Serikali,
Sekta binafsi, Jumuiya mbali mbali kushirikiana katika kutatua changamoto
zinazoikabili sekta hizi ili kuwapa unafuu wananchi wa Zanzibar.
6 PROGRAMU
ZA WIZARA KWA MWAKA 2020/2021
129. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2020/2021, Wizara ya Biashara na Viwanda inatarajia kuendeleza azma yake ya
kukuza Viwanda kama inavyoelezwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015
– 2020 ibara namba 84 (a, b mpaka h). Pia maazimio yaliyomo katika Mkakati wa
Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUZA III 2016 – 2020) pamoja na miongozo
ya Viongozi Wakuu wa nchi yetu. Maeneo mengine makuu yatakayopewa kipaumbele ni
pamoja na kuweka mazingira mazuri ya Biashara, utafutaji wa masoko na usaidizi
wa wajasiriamali na wazalishaji wadogo wadogo.
130. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Biashara na
Viwanda inatarajia kutekeleza shughuli mahsusi zifuatazo katika bajeti ya mwaka
wa fedha wa 2020/2021 kama vipaumbele vyake:-
i.
Kuyaendeleza
na kuyapima maeneo ya viwanda, Mheshimiwa Spika, Wizara inatarajia kuandaa
Mpango wa matumizi (Master Plan) na upembuzi yakinifu (feasibility study) kwa
eneo la Dunga ili wawekezaji waliokuwa tayari kuwekeza wapimiwe na kuanza
ujenzi. Pamoja na kufikisha miundombinu ya umeme, maji na kukata barabara za
ndani. Vile vile Wizara, itaendelea kuyapima maeneo mapya yatakayoanishwa na
Kamisheni ya Ardhi kwa ajili ya viwanda.
ii.
Kuendeleza
ujenzi wa Ofisi na Maabara za ZBS kwa awamu ya pili
Mheshimiwa Spika, Kutokana na kukamilika
kwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa Ofisi na maabara, Wizara itaendelea na awamu
ya pili ili kukamilisha ujenzi wa maabara na Ofisi za ZBS Maruhubi. Aidha,
Kuimarisha utekelezaji wa Mfumo wa Ubora ndani ya ZBS (QMS) kwa kutumia kiwango
cha ISO 9001:2015 na kuweka mfumo wa TEHAMA utakaorahisisha na kuimarisha
ufanisi wa utekelezaji wa kazi.
iii. Kuliendeleza eneo la Nyamanzi na kuandaa
Matamasha mbalimbali
Mheshimiwa Spika, Eneo la
maonesho la Nyamanzi limewekwa katika orodha ya Miradi ya kuendelezwa
kwa kushirikiana na sekta binafsi (PPP), Wizara inakusudia kuliandaa eneo hilo
kwa kufanya Tathmini ya kimazingira na kijamii (ESIA) pamoja na kulisafisha
eneo hilo. Pia, Wizara inatarajia kuongeza vifaa vya kufanyia matamasha ikiwemo
matenti na magazebo.
iv. Kuandaa Mfumo wa Kitaifa wa Usajili wa
Biashara na Utoaji leseni na kuunganisha Mamlaka za utoaji leseni (NOBS)
Mheshimiwa Spika, Ili kuendelea
kurahisisha ufanyaji biashara hapa Zanzibar, Wizara itaimarisha mfumo maalum wa
kitaifa wa usajili wa Biashara na Utoaji wa leseni (NOBS) pamoja na
kuziunganisha Mamlaka za utoaji leseni. Mfumo huu wa Tehama utatoa taarifa na
huduma muhimu za usajili, uwekezaji na leseni au vibali vinavyotakiwa na
wawekezaji na wafanyabiashara.
v.
Kuanzisha na
Kuimarisha Wakala wa Vipimo na Mizani
Mheshimiwa
Spika, Kutokana na kupitishwa kwa sheria na kuanzishwa kwa Wakala wa
vipimo, kwa mwaka 2020/2021, Wizara inatarajia
kuanzisha taasisi hiyo na kuiimarisha kwa kuipatia vifaa vya kutendea
kazi kama vile wafanyakazi, kanuni ambazo zitaongoza ufanyaji kazi pamoja na
sehemu ya Ofisi.
vi. Kuimarisha Tume Ushindani Halali wa Biashara
na Kumlinda Mtumiaji:
Mheshimiwa
Spika, Katika kuimarisha mazingira mazuri ya ushindani halali wa kibiashara
na kumlinda mtumiaji, Wizara itaendelea kuimarisha mazingira ya ufanyaji kazi
kwa kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na sheria ya ushindani halali wa kibiashara
na kumlinda mtumiaji. Pia, kufanya chunguzi, utafiti, kusikiliza mashauri
yanayoathiri Ushindani katika soko na Miungano (Merger).
vii. Kuimarisha Wakala wa Kusimamia wazalishaji
wadogo wadogo na wa kati:
Mheshimiwa
Spika, Wizara inatarajia kuendeleza ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya SMIDA
iliopo Maruhubi, kuanzisha kituo cha usarifu wa mazao ya kilimo (Agribusiness
Innovation Center) huko Kizimbani na Maruhubi kwa kushirikiana na PASS.
viii. Kuimarisha Takwimu za Biashara na Viwanda:
Mheshimiwa Spika, Wizara inatarajia kuweka mfumo maalum utakaotumika
kukusanya takwimu za Biashara na Viwanda ambazo zitatumika katika mipango ya
maendeleo na mengine ya Serikali na sekta Binafsi hatimae zitawasilishwa kwa
Mtakwimu Mkuu wa Serikali.
ix. Kuwaendeleza wajasiriamali na wazalishaji
wadogo:
Mheshimiwa
Spika, Kupitia program ya kuwaendeleza wajasiriamali na wazalishaji wadogo
wadogo na wa kati, Wizara itatoa mafunzo na mikopo kwa wazalishaji wadogo
wadogo kutoka Halmashauri na Miji ya Zanzibar na makundi maalum ya vijana na
wanawake ili kuwapatia mitaji na kuweza kujiajiri.
x.
Kuendeleza
usarifu wa mwani:
Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia ZSTC
inatarajia kuanzisha kiwanda cha kusarifu mwani kwa kushirikiana na wawekezaji
kutoka Indonesia. Kiwanda kinatarajiwa kuwepo katika eneo la Chamanangwe Pemba.
xi. Kuendeleza na kufanya tafiti mbalimbali za
biashara na viwanda
Mheshimiwa
Spika, Kwa mwaka 2020/21, Wizara itaendelea na utafiti wa Mazingira Mazuri
ya Biashara (Easy of Doing Business), Utafiti wa bidhaa kwa soko la AGOA na
utafiti wa bidhaa za madawa asilia.
xii. Uimarishaji wa Mashirikiano baina ya Sekta
ya Umma na Serikali
Mheshimiwa Spika, Wizara inatarajia
kuendeleza mashirikiano haya kwa kuyasimamia na kuyaendeleza Mabaraza ya
Biashara ya Mikoa, kuandaa Mkutano wa nne (4) wa Baraza la Biashara na Jukwaa
la Kumi na moja (11) la Biashara kwa mwaka wa fedha 2020/21.
xiii. Kwa
upande wa Shirika la Biashara la Taifa, linatarajia kununua Karafuu tani 4,000
na Makonyo tani 800 kwa msimu wa mwaka 2020/21, kuendelea uzalishaji wa mafuta
ya Makonyo na mimea mengine pamoja na kuratibu uzalishaji wa wa mafuta ya
karafuu kwa kufunga vinu sita vya kusindika majani makavu ya karafuu kwa upande wa Pemba.
6.1 Matumizi ya Wizara kwa Mwaka 2020/2021
131. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2020/21, Wizara ya Biashara na Viwanda imepangiwa matumizi ya jumla ya shilingi bilioni 23.570. Kati ya fedha
hizo Jumla ya shilingi bilioni 8.77
zimetengwa kwa ajili ya Matumizi ya kazi za kawaida na Mishahara na shilingi bilioni 14.80 kwa kazi za
Maendeleo. Fedha za maendeleo ni pamoja na Shilingi
bilioni 4.6 tunazotarajia kutoka kwa washirika wa maendeleo kwa programu ya
kuwaendeleza wajasiriamali na wazalishaji wadogo wadogo na wa kati ( Khalifa
Fund ).
Mheshimwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2020/21 Wizara ya Biashara na Viwanda imepanga kutekeleza miradi mikuu mitano
(5) ya maendeleo ambayo ni: - Kuimarisha maendeleo ya viwanda, Kuimarisha
Mazingira bora ya biashara, Kuimarisha Taasisi ya Viwango Zanzibar, Mfumo wa
utowaji leseni kwa maendeleo ya sekta binafsi na kuimarisha wajasiriamali.
132. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2020/2021, Wizara ya Biashara na Viwanda itaendelea kutekeleza program kuu nne
(4) na program ndogo kumi (10). Programu kuu hizo kama zifuatavyo:
i. Programu
ya Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ii. Programu
ya Maendeleo ya Viwanda na Ujasiriamali iii. Programu
ya Ukuzaji na Uendelezaji Biashara
iv. Programu ya Viwango na Uthibiti Ubora
PROGRAMU YA UENDESHAJI NA URATIBU WA WIZARA YA
BIASHARA NA VIWANDA
133. Mheshimiwa Spika, Programu kuu ya
Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Biashara na Viwanda imegawika katika
Programu ndogo tatu kwa mujibu wa huduma ambazo inazitoa. Program hizo ndogo ni
kama zifuatazo:
i. Utawala na
Uendeshaji wa shughuli za Wizara ya
Biashara
na Viwanda; ii. Uratibu wa
Mipango, Sera na Tafiti za Wizara; na iii. Uratibu
na Utekelezaji wa Shughuli za Wizara Pemba
134. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Utawala na Uendeshaji wa shughuli za Wizara ya Biashara na Viwanda ambayo
inatekelezwa na Idara ya Uendeshaji na Utumishi itakuwa na jukumu la kutoa
huduma ya usimamizi wa rasilimali watu na huduma za kiofisi kwa ujumla pamoja
na ununuzi wa vifaa. Ili kutekeleza majukumu yake, programu hii ndogo
imepangiwa matumizi ya shilingi bilioni
2.29 kwa mwaka wa fedha 2020/ 2021.
135. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa program
ndogo ya Uratibu wa Mipango, Sera na Tafiti za Wizara ambayo utekelezaji wake
utasimamiwa na Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, itakuwa na jukumu la uandaaji
na uibuaji wa sera na tafiti za Wizara, uandaaji na utekelezaji wa mipango
ya Wizara pamoja
na usimamizi wa takwimu za Biashara na Viwanda. Katika kutekeleza huduma hizo,
programu ndogo ya uratibu wa Mipango, Sera na Tafiti imepangiwa matumizi ya shilingi milioni 579.08 kwa mwaka wa
fedha wa 2020/2021.
136. Mheshimiwa Spika, Program ndogo ya
Uratibu na Utekelezaji wa Shughuli za Wizara Pemba ambayo inaratibu shughuli za
uendeshaji wa Wizara ya Biashara na Viwanda kwa upande wa Pemba imepangiwa
matumizi ya shilingi milioni 652.94
kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021.
137. Mheshimiwa Spika, Ili kuweza kutekeleza
shughuli zilizopangwa katika Programu kuu ya Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya
Biashara na Viwanda kwa mwaka 2020/2021, naliomba Baraza lako tukufu
kuidhinisha matumizi ya shilingi bilioni
3.53 kwa program hii kuu.
PROGRAMU
YA MAENDELEO YA VIWANDA NA UJASIRIAMALI
138. Mheshimiwa Spika, Programu kuu ya
Maendeleo ya Viwanda na Ujasiriamali imegawika katika Programu ndogo mbili kwa
mujibu wa huduma ambazo inazitoa. Program hizo ndogo ni kama zifuatazo: i.
Ukuzaji Viwanda ii. Maendeleo ya
Ujasiriamali
139. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Ukuzaji Viwanda itakuwa na jukumu la kutoa huduma ya Uimarishaji wa Sekta ya
Viwanda ikiwemo kusimamia ujenzi wa maeneo maalum ya viwanda (Industrial
Parks), Ujenzi wa Makao Makuu ya Ofisi ya SMIDA, pamoja na kuimarisha kitengo
cha inteligensia ya viwanda ambapo utekelezaji wake utasimamiwa na Idara ya
Maendeleo ya Viwanda na SMIDA. Ili kutekeleza huduma hii, programu hii ndogo
imepangiwa matumizi ya shilingi bilioni
3.61 kwa mwaka 2020/2021.
140. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa
programu ndogo ya Maendeleo ya Ujasiriamali ambayo ina jukumu la kutoa mafunzo,
msaada na mikopo kwa wajasiriamali, Ili kutekeleza huduma hii, programu hii
ndogo imetengewa shilingi bilioni 9.17
kwa mwaka 2020/2021.
141. Mheshimiwa Spika, Ili kutekeleza
majukumu ya Program kuu ya Maendeleo ya Viwanda na Ujasiriamali kwa mwaka
2020/2021, naomba Baraza lako tukufu liidhinishe matumizi ya shilingi bilioni 12.78 kwa ajili ya
kutekeleza shughuli za programu hii kuu.
PROGRAMU YA UKUZAJI NA UENDELEZAJI
BIASHARA
142. Mheshimiwa Spika, Programu ya tatu
itakayotekelezwa na Wizara kwa mwaka 2020/2021 ni Ukuzaji na Uendelezaji
Biashara. Kwa ajili ya utekelezaji mzuri wa malengo yake, programu hii
imegawanyika katika Programu ndogo nne
(4) kama
zifuatavyo:
i. Ukuzaji Masoko na Usafirishaji ii. Ushindani Halali wa Biashara na Kumlinda
Mtumiaji iii. Urahisishaji
Biashara na Ukuzaji Biashara za Ndani iv. Usajili
wa Biashara na Mali
143. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Ukuzaji Masoko na Usafirishaji itakuwa na jukumu la kutoa huduma za uimarishaji
wa mazingira mazuri ya biashara, kuongeza fursa za masoko pamoja na
urahisishaji biashara ambapo utekelezaji wake utasimamiwa na Idara ya Biashara.
Ili kutekeleza huduma hizo, programu ndogo ya Ukuzaji wa Masoko na Usafirishaji
imetengewa shilingi milioni 856.30 kwa
mwaka 2020/2021.
144. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa
programu ndogo ya Ushindani Halali wa Kibiashara na Kumlinda Mtumiaji ambayo
itakuwa na jukumu la kuimarisha ushindani halali wa kibiashara na kumlinda
mtumiaji kwa kuendelea kutoa huduma za ukaguzi na uhakiki wa vifaa vya mizani,
vipimo, ukaguzi wa biashara na maghala pamoja na ushajihishaji na utoaji wa
elimu kwa watumiaji, ambapo utekelezaji wake utasimamiwa na Tume ya Ushindani
Halali wa Biashara na Idara ya Biashara (baadae Wakala wa Vipimo na Mizani).
Ili kutekeleza huduma hizo, naliomba Baraza lako tukufu liidhinishe matumizi ya
shilingi milioni 376.87 kwa mwaka wa
fedha 2020/2021.
145. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Urahisishaji Biashara na Ukuzaji Biashara za Ndani itakuwa na jukumu la kutoa
huduma za usimamizi wa mamlaka zinazotoa leseni kwa kufanya utafiti na kuweka
vigezo vinavyohusu leseni chini ya Baraza la Kusimamia Mfumo wa Utoaji leseni.
Aidha, Baraza la Taifa la Biashara litasimamia uimarishaji wa majadiliano baina
ya sekta ya umma na sekta binafsi kwa kuandaa majukwaa mbalimbali ya biashara
nchini. Ili kutekeleza huduma hizo zilizopangwa chini ya Programu hii ndogo,
naliomba Baraza lako tukufu liidhinishe matumizi ya shilingi bilioni 1.22 kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
146. Mheshimiwa Spika, Programu ndogo ya
Usajili wa Biashara na Mali ambayo itakuwa na jukumu la usimamizi wa usajili wa
biashara na mali kwa Mfumo wa kielektroniki na kuimarisha mifumo ya usajili wa
biashara na mali. Ili kutekeleza huduma hizo, naliomba Baraza lako tukufu
liidhinishe shilingi milioni 867.7
kwa mwaka 2020/2021.
147. Mheshimiwa Spika, Ili kutekeleza huduma
zilizopangwa katika Programu kuu hii ya Ukuzaji na Uendelezaji Biashara kwa
mwaka 2020/2021, naliomba Baraza lako tukufu liidhinishe jumla ya shilingi bilioni 3.32 kwa program hii
kuu.
PROGRAMU
YA VIWANGO NA TATHMINI YA UBORA
148. Mheshimiwa Spika, Programu
kuu ya nne itakayotekelezwa na
Wizara kwa mwaka 2020/2021 ni Viwango na Tathmini ya Ubora. Kwa ajili ya
utekelezaji mzuri wa malengo yake, programu hii imepangiwa kuwa na programu
ndogo moja ya Viwango na Uthibiti wa Ubora ambayo itakuwa na huduma za Uandaaji
na Ukuzaji wa Viwango pamoja na huduma za Tathmini ya Ubora wa Bidhaa.
Utekelezaji wake utasimamiwa na Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS). Ili
kutekeleza shughuli zilizopangwa katika programu hii, naliomba Baraza lako
liidhinishe shilingi bilioni 3.94
kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kwa program
hii kuu.
149. Mheshimiwa Spika, Taarifa kamili ya
Wizara hii imeelezwa katika kitabu cha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha
kwa Bajeti inayotumia Programu (PBB) kwa mwaka wa fedha 2020/2021 – 2022/2023
kutoka ukurasa wa R01 mpaka ukurasa wa R018.
SHIRIKA LA BIASHARA LA
TAIFA – ZSTC
Shughuli za Shirika
kwa mwaka wa fedha
2020/2021
150. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
mwaka wa fedha 2020/ 2021, Shirika la Biashara la Taifa linatarajia kutekeleza
shughuli kuu zifuatazo;
i. Ununuzi wa karafuu tani 4,000 na
makonyo tani
800 ; ii. Kuongeza uzalishaji wa mafuta
ya mimea kwa kuimarisha shamba la Mtakata, mashamba ya mkaratusi na
kukiimarisha Kiwanda cha Makonyo;
iii.
Kuimarisha vitega uchumi vya Shirika vikiwemo; jengo la
Madungu, Malindi na eneo la Saateni.
iv.
Kukamilisha taratibu za uanzishwaji wa kiwanda cha
kusarifu mwani.
Ununuzi na Mauzo ya Karafuu
151. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2020/2021, bei ya kununulia Karafuu kutoka kwa wakulima inatarajiwa
kutobadilika kutoka TZS 14,000 kwa kilo moja daraja la kwanza, TZS 12,000 kwa
daraja la pili na TZS 10,000 kwa daraja la tatu.
152. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha
mwaka wa fedha 2020 /2021, Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Biashara la Taifa
limeidhinisha matumizi ya Jumla ya shilingi
bilioni 73.67 katika kutekeleza kazi za kawaida, Maendeleo pamoja na
ununuzi wa karafuu na makonyo.
7 SHUKRANI:
153. Mheshimiwa Spika, Mafanikio ya Wizara
yaliyopatikana ni matokeo ya mashirikiano makubwa ya Wajumbe wa Baraza hili
chini ya uongozi wako mahiri. Ninakushukuru wewe binafsi, Wenyeviti wa Kamati
za kudumu za Baraza
na Wajumbe wote
kwa ushauri na michango mliyotupatia katika kipindi cha utekelezaji wa bajeti.
Shukrani zangu pia ziende kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo
Mheshimiwa Mwinyihaji Makame Mwadini, Mwakilishi wa Jimbo la Dimani, wajumbe na
Makatibu wote wa Kamati hiyo kwa ushauri na miongozo waliyoitoa katika
mapendekezo ya Bajeti ya Wizara ya Biashara na Viwanda na hatimae kuridhia
mapendekezo haya yawasilishwe katika Baraza hili.
154. Mheshimiwa Spika, Mafanikio ya
kiutendaji yaliyojitokeza katika kipindi cha mwaka 2019/2020 ni matokeo ya
ushirikiano mkubwa uliopatiwa Wizara ya Biashara na Viwanda kutoka kwa wadau
mbali mbali wa ndani na nje ya nchi yetu. Kwa madhumuni ya kutambua mchango
mkubwa wa Wadau mbali mbali kwa Wizara, naomba kutoa shukrani zangu za dhati
kwa nchi na taasisi za ndani na nje zifuatazo; Jamhuri ya Watu wa China, India,
Jumuiya ya Ulaya (EU),USAID, Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP),
Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO), Shirika la
Kimataifa la Tasnia ya Malibunifu (WIPO), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB),
Benki ya Dunia (World Bank), Shirika la Biashara Duniani (WTO), TANTRADE, Tume
ya Sayansi na Teknolojia ya Tanzania (COSTECH), Zanzibar Seaweed Cluster
Initiative (Zasci), Milele Foundation, Jumuiya ya Wafanyabiashara Zanzibar
(ZNCC) na Wafanyabiashara wote wakubwa, wadogo na Wawekezaji wa Viwanda.
Aidha, napenda kuishukuru Wizara ya
Viwanda na Biashara na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, kwa mashirikiano yao kwenye shughuli mbali mbali tulizofanya.
155. Mheshimiwa Spika, Napenda nichukue
fursa hii kwa mara nyingine tena kuwapongeza kwa dhati viongozi na wafanyakazi
wote wa Wizara ya Biashara na Viwanda kwa kazi kubwa yenye ufanisi mzuri
wanayoifanya kila siku licha ya kukabiliwa na changamoto mbali mbali, ni
matarajio yangu kwamba wataongeza juhudi zao ili kuzidisha ufanisi kwa
kuwahudumia wananchi na kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Kadhalika, napenda
kuwapongeza wafanyakazi wote walioshiriki katika maandalizi ya Hotuba hii kwa
kazi nzuri waliyoifanya, nawaombea dua njema katika kazi zao za sasa na zijazo.
156. Mheshimiwa Spika, Naomba niwashukuru
wafanyabiashara na wenye viwanda wote wakubwa, wakati na wadogo kwa juhudi zao
kubwa za kuwahudumia wananchi kwa kuwapatia huduma mbali mbali pamoja na bidhaa
muhimu za chakula, nguo, vyombo vya moto, na vifaa vya ujenzi. Nawaomba waendelee kushirikiana na Wizara ya
Biashara na Viwanda kwa kufanya kazi pamoja kwa lengo la kuimarisha biashara na
kutoa huduma bora kwa wananchi.
8 MAOMBI YA FEDHA KWA PROGRAMU KWA MWAKA
WA FEDHA 2020/2021
Mapato
ya Serikali:
157. Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha
2020/2021, Wizara ya Biashara na Viwanda imepanga kukusanya jumla ya shilingi bilioni 2.36. Mapato hayo
yatakusanywa kutoka vianzio tofauti kama inavyoonekana katika
Jadweli Namba 3:
Mapato ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2020 - 2021
Mapato
ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2020 - 2021
KIFUNGU
|
MAELEZO
|
MAKADIRIO
|
R0104
|
Idara
ya Biashara na Ukuzaji Masoko
|
154,400,000
|
1422014
|
Ukaguzi wa
Mezani na Vipimo
|
154,400,000
|
R0109
|
Tume
ya Ushindani Halali wa Kibiashara na Kumlinda Mtumiaji
|
250,000,000
|
1422077
|
Malipo ya kazi
za biashara
|
250,000,000
|
R0105
|
Idara ya Uendeshaji na Utumishi
|
197,268,000
|
1422078
|
Malipo kwa ajili ya Ukodishwaji wa Maeneo ya
kibiashara
|
197,268,000
|
R0106
|
Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali
|
709,827,719
|
1146002
|
Ada ya Utunzaji
Urithi
|
1,200,000
|
1422030
|
Alama za
Biashara
|
350,700,000
|
1422031
|
Uandikishaji wa
Makampuni
|
234,327,719
|
1422032
|
Uandikishaji wa
Majina ya Biashara
|
72,400,000
|
1422034
|
Ujira wa
kutengeneza nyaraka
|
51,200,000
|
R0107
|
Taasisi ya Viwango Zanzibar
|
976,000,000
|
1112008
|
Malipo ya
usimamizi viwango
|
976,000,000
|
R0101
|
Afisi Kuu-Pemba
|
80,301,281
|
1422014
|
Ukaguzi wa
Mezani na Vipimo
|
42,901,281
|
1422078
|
Malipo kwa ajili ya Ukodishaji wa Maneneo ya
kibiashara
|
12,000,000
|
1422031
|
Uandikishaji wa
Makampuni
|
2,200,000
|
1422032
|
Uandikishaji wa
Majina ya Biashara
|
1,200,000
|
1422034
|
Ujira wa
kutengeneza nyaraka
|
22,000,000
|
Jumla
Kuu
|
2,367,797,000
|
Chanzo: Wizara ya Biashara na Viwanda, 2020
Matumizi:
158. Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa
matumizi ili Wizara ya Biashara na Viwanda iweze kutekeleza programu zake
ilizojiwekea kwa mwaka wa fedha 2020/2021, naliomba Baraza lako tukufu liidhinishe matumizi ya jumla ya shilingi
23,569,700,000 kwa programu nne (4) kama
inavyoonekana katika Jadweli Namba 4:
Jadweli Namba 4:
Maombi
ya Fedha (TZS Mil)
Maombi
ya Fedha (TZS Mil)
Geresho (Code)
|
Programu Kuu/Programu ndogo
|
Makadirio 2020 - 2021 (mil)
|
PR0101
|
Uendeshaji wa Uratibu wa Wizara ya
Biashara na Viwanda
|
3,526.98
|
SR010101
|
Utawala
na Uendeshaji wa Wizara ya Biashara na Viwanda.
|
2,294.98
|
SR010102
|
Uratibu
wa Mipango, Sera na Tafiti za Wizara
|
579.07
|
SR010103
|
Uratibu na Utekelezaji wa shughuli za
Wizara Pemba
|
652.93
|
PR0102
|
Maendeleo
ya Viwanda na Ujasiriamali
|
12,782.15
|
SR010201
|
Ukuzaji wa Viwanda
|
3,612.75
|
SR010202
|
Maendeleo ya Ujasiriamali
|
9,169.40
|
PR0103
|
Ukuzaji
na Uendelezaji wa Biashara
|
3,316.77
|
SR010301
|
Ukuzaji wa Masoko na Usafirishaji
|
856.30
|
SR010302
|
Ushindani Halali wa Kibiashara na
Kumlinda Mtumiaji
|
376.87
|
SR010303
|
Urahisishaji biashara na Ukuzaji
Biashara za Ndani
|
1,215.90
|
SR010304
|
Usajili wa Biashara na Mali
|
867.70
|
PR0104
|
Viwango
na Tathmini ya Ubora
|
3,943.80
|
SR010401
|
Viwango na Uthibiti Ubora
|
3,943.80
|
JUMLA KUU
|
23,569,700
|
Chanzo: Wizara ya Biashara na Viwanda, 2020
9 HITIMISHO:
159. Mheshimiwa Spika, Baada ya maelezo
niliyatoa, naomba waheshimiwa wajumbe wa Baraza lako tukufu kuidhinisha
mapendekezo ya kukusanya mapato ya shilingi bilioni 2.36 kutokana na huduma
zinazotolewa na Wizara. Aidha ili Wizara ya Biashara na Viwanda iweze
kutekeleza shughuli zilizopangwa kwa mwaka wa fedha 2020/20221, naomba Wajumbe
wa Baraza lako tukufu kuidhinisha matumizi ya shilingi 23,569,700,000 kwa fungu
la R01.
160. Mheshimiwa Spika, Nakushukuru wewe
binafsi, Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza lako pamoja na wananchi kwa kunisikiliza.
161.
Mheshimiwa
Spika, Naomba kutoa hoja.
10VIAMBATANISHO
Kiambatanisho
Namba 1.
Michango
na kodi zilizokusanywa na Mamlaka za mapato ZRB, TRA na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar
(TZS).
ZRB
|
TRA
|
ZSSF
|
Jumla
|
|
ZMCL
|
596,650.14
|
507,363.30
|
117,662.54
|
1,221,675.98
|
ZSFL
|
1,278,409.60
|
278,814.03
|
230,093.71
|
1,787,313.34
|
ADPL
|
186,723.84
|
95,100.00
|
75,600.00
|
357,423.84
|
JUMLA
|
2,061,783.58
|
881,277.33
|
423,356.25
|
3,366,413.16
|
Chanzo: ADPL, ZSFL,
ZMCL April 2020
Kiambatanisho
Namba 2.
Matumizi
ya Fedha kwa kipindi cha Julai 2019 – Machi 2020
S/N
|
Programu
Kuu
|
Fedha
Zilizotengwa
kwa Mwaka wa
Fedha
2019/2020 TZS
|
Fedha
Zilizopatikana kwa Kipindi cha Miezi
Tisa (Julai -
Machi,
2019/2020)
TZS
|
Asilimia ya
Fedha
Iliyopatikana
|
PRO1
|
Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya
Biashara
|
2,992,621,800
|
2,313,908,658
|
77
|
Utawala na Uendeshaji wa Wizara
|
2,139,511,316
|
1,735,995,907
|
81
|
|
Uratibu wa Mipango, Sera na Utafiti
|
367,121,800
|
235,553,221
|
64
|
|
Uratibu na Utekelezaji wa
|
||||
shughuli za Wizara Pemba
|
485,988,684
|
342,359,530
|
70
|
|
PR02
|
Maendeleo ya
Viwanda na
Ujasiriamali
|
6,853,911,000
|
1,083,451,605
|
16
|
Ukuzaji Viwanda
|
3,286,514,000
|
1,062,342,353
|
32
|
|
Maendeleo ya Ujasiriamali
|
3,567,397,000
|
21,109,252
|
1
|
|
PR03
|
Ukuzaji na
Uendelezaji wa
Biashara
|
3,026,067,200
|
1,787,057,972
|
59
|
Ukuzaji Masoko na Usafirishaji
|
754,857,200
|
393,450,075
|
52
|
|
Ushindani Halali wa
|
||||
Kibiashara na Kumlinda Mtumiaji
|
344,810,000
|
219,716,550
|
64
|
|
Urahisishaji wa Biashara
|
||||
na Ukuzaji biashara za ndani
|
1,105,500,000
|
622,906,000
|
56
|
|
Usajili wa Biashara na Mali
|
820,900,000
|
550,985,347
|
67
|
|
PR04
|
Viwango
na Tathmini ya Ubora.
|
2,724,800,000
|
1,066,438,052
|
39
|
Viwango na Udhibiti Ubora.
|
2,724,800,000
|
1,066,438,052
|
39
|
|
40
|
||||
JUMLA KUU
|
15,597,400,000
|
6,250,856,287
|
Chanzo: Wizara ya Biashara na Viwanda, 2020
!Kiambatanisho Namba 3.
Baadhi
ya Viwanda na hatua mbali mbali za uanzishaji wake kwa kipindi 2019/2020.
NA
M
|
JINA
LA KIWANDA
|
MAHALI
|
BIDHAA
|
HALI
YA KIWANDA
|
MUELEKEO/MATEGEMEO
|
|||
1.
|
Kiwanda cha Chumvi
|
Chamanang we Pemba
|
Chumvi
|
Uzalishaji
mdogo umeanza katika sehemu nyengine
kwa muda
|
Ulipaji wa
fidia kwa wenye vipando umekamilika na
ujenzi wa kiwanda unaendelea
|
|||
2.
|
Kiwanda Cha Mwani
|
Chamanang we Pemba
|
Karajina
|
Site plan ya kiwanda
hichi imeshaandaliwa
|
Utaratibu wa mashirika ya Serikali kushirikiana
kujenga
kiwanda hicho
ndio utakaotumika
|
|||
3.
|
Kiwanda cha Mafuta ya Majani ya Karafuu
|
MgelemaPemba
|
Mafuta ya majani
makavu ya karafuu
|
Kiwanda kipya tayari kimejengwa na
tayari kimeanza uzalishaji
|
Kiwanda kimetoa ajira za moja kwa moja
15 kwa Wananchi wa Pemba na ajira nyingi zisizo za moja kwa moja.
|
|||
4.
|
Kiwanda cha Maziwa
|
Chamanang we Pemba
|
Maziwa
|
Bado wazalishaji samli ya ng’ombe wanaendelea
na uzalishaji katika eneo lao la awali liliopo kisiwani kwa
Binti Abeid
|
Hatua za kuwashajiisha kufanya uzalishaji
katika eneo lililotengwa la viwanda
Chamanangwe
zinaendelea.
|
|||
5.
|
Kiwanda cha Bomba
za Plastic
|
Maruhubi
|
Mabomb
a
|
Mwekezaji anaendelea na ujenzi wa
kiwanda
|
Kiwanda kinatarajia kuanza kazi mwisho
wa mwaka 2020
|
|||
6.
|
Kiwanda cha Tungule
na Pilipili
|
ShakaniUnguja
|
Tungule
na Pilipili
|
Kiwanda kipya kinatarajiwa kufunguliwa
rasmi mwezi wa April
|
Kiwanda
kitatumia malighafi kutoka kwa wakulima wetu hapa hapa Zanzibar
|
|||
7.
|
Kiwanda cha
Vifungashio
|
Uzini-
Unguja
|
Vifungas hio
|
Kiwanda kinafanya kazi
|
Bidhaa zake tayari ziko sokoni
|
|||
8.
|
Kiwanda cha
Vifungashio
|
NyamanziUnguja
|
Vifungas hio(Mifuk o ya karatasi)
|
Kiwanda kinafanya kazi
|
Bidhaa zake tayari ziko sokoni
|
|||
9.
|
Kiwanda cha
Vifungashio
|
Wilaya ya kati-Unguja
|
Vifungas hio
|
Kiwanda tayari kimeanza na uzalishaji wa mifuko
(carrier bags)
|
Bidhaa zake
tayari ziko sokoni Zanzibar na Tanzania bara. Matarajio ni kulifikia soko la
Comoro.
|
|||
10.
|
Kiwanda
cha Vibiriti
|
Wilaya ya kati-Unguja
|
Vibiriti
|
Mwekezaji
anaendelea
na kulifanyia kazi jambo hili ili kuona kama ataendelea na uwekezaji huo au
atawekeza kwenye mradi mwengine
|
Ukosefu wa umeme wa uhakika ni tatizo
kubwa kwa sasa
|
|||
11.
|
Kiwanda cha minofu ya kuku
|
Wilaya ya Kati-Unguja
|
kuku
|
Usajili wa kampuni
BPRA na ZIPA tayari Hatua za kupatiwa
hati ya ardhi (land lease) zinaendelea kazi
|
Mradi huu utajumuisha ujenzi wa kiwanda cha
kuzalisha chakula cha kuku pamoja na
chinjio la
kisasa
|
|||
12.
|
Kiwanda cha Chakula cha Mifugo
|
Wilaya ya Kati-Unguja
|
chakula cha mifugo
|
Usajili wa kampuni
BPRA na ZIPA tayari Hatua za kupatiwa
hati ya ardhi (land lease) zinaendelea kazi
|
Kitaanza kazi
baada ya kumaliza taratibu zote.
|
|||
13.
|
Kiwanda cha kutotolea Vifaranga vya Kuku
|
Wilaya ya
Kati
|
Vifarang
a vya
kuku
|
Usajili
wa kampuni BPRA na ZIPA tayari Hatua za kupatiwa hati ya ardhi (land lease)
zinaendelea
kazi
|
Wizara
imefanya mkutano wa wadau ili kupata maoni na kukusanya sheria za taasisi
mbali mbali zitakazosaidia wawekezaji wa mradi huo
- Memorandum of
|
|||
understanding
(MOU) kwa ajili ya kuweka makubaliano ya pamoja kati ya Wizara ya kilimo na
wawekezaji wa mradi huo ili kuhakikisha mradi unaendelea
|
||||||||
14.
|
Kiwanda cha Ushoni
|
Buyu-
Unguja
|
Nguo
|
Mazungumzo
bado yanaendelea baina ya Serikali na Muwekezaji kutoka China.
|
Mwekezaji anaendelea
kufanyia kazi
jambo hili
|
|||
15.
|
Kiwanda cha kuzalisha Vitambaa
|
Basra-
Textile Mills-
Chumbuni
Unguja
|
Nguo
|
Awamu
ya kwanza ya mashine tayari zimeshawasili kiwandani. Shehena iliyobaki
ilitarajiwa kuwasili ndani ya mwezi wa April 2020
|
Kiwanda
kinatarajiwa kuanza uzalishaji kwa majaribio kabla ya mwezi Agosti 2020.
Hatua zimesita kutokana Covid 19 imechelewesha kufika kwa shehena iliyobaki
pamoja na wataalamu.
|
|||
16.
|
Kiwanda cha Kukaushia
Dagaa
|
Fungurefu
Mkokotoni
|
Dagaa na Samaki
|
Kampuni
ya Uvuvi ya ZAFICO imeshaanza taratibu za awali za kumtafuta Mshauri elekezi
atakaebuni michoro ya kiwanda hicho.
|
Timu
iliyofanya tathmini imetoa mapendekezo kwa bodi juu ya kufanya uhakiki wa
kampuni zilizojitokeza kabla ya kufanya maamuzi ya kumpa tenda mmoja kati ya
hao.
|
|||
17.
|
Kiwanda
cha Mafuta ya mkaratusi
|
Wawi-
Pemba
|
Mafuta
|
Kiwanda
kimekamilika na kiko tayari kwa uzalishaji
|
Kiwanda kinasubiri malighafi kutoka shambani
|
|||
18.
|
Kiwanda cha kusarifu
Ndimu
|
Chwaka
|
Sirapu ya Ndimu
|
Jengo la Kiwanda limeshamalizika,
imebaki kuweka
milango na
Madirisha
|
Mashine
imeshafika na uzalishaji utaanza mara moja ujenzi utakapokamilika
|
|||
19.
|
Kiwanda cha Kusarifu Tungule
|
Mtule Paje
|
Tomato sauce
|
Kinafanya kazi
|
Kiwanda
kimeanza uzalishaji
|
|||
Kiambatanisho Namba 4.
Huduma ya Ukaguzi
Eneo la Ukaguzi
|
Jumla
|
Mezani ndogo
|
2,146
|
Mezani kubwa
(Platform)
|
27
|
Mezani (Weigh
bridge)
|
0
|
Mita za Depot
(Flow Meter)
|
50
|
Pampu za
kuuzia mafuta
|
307
|
Fillers
|
0
|
Magari ya
kusambaza mafuta
|
20
|
Matangi ya
mafuta
|
19
|
Uthibitisho wa
tanks (Certification)
|
0
|
Usajili wa
Kampuni za mafuta
|
0
|
Bidhaa za Viwandani
zilizofungashwa
|
6
|
Chanzo: Wizara ya Biashara
na Viwanda, 2020
Kiambatanisho
Namba 5. Hali ya Uzalishaji Kwa Mwaka 2019/2020
Aina
ya Mafuta
|
Lengo
2019/2020
(Kg)
|
Uzalishaji
Halisi (Kg)
|
Thamani (TZS)
|
Makonyo
|
46,875.0
|
6,003
|
194,473,188.00
|
Mchaichai
|
150.0
|
142.546
|
22,847,500.00
|
Mdalasini
|
37.5
|
2.0
|
650,000.00
|
Mrehani
|
18.75
|
4.25
|
1,381,250
|
Mkaratusi(manukato)
|
750.0
|
156.5
|
12,520,000.00
|
Mkaratusi(madawa)
|
243.75
|
86.0
|
6,880,000.00
|
Majani ya mkarafuu
|
375
|
369.2
|
29,536,000.00
|
Unga wa
Karafuu
|
0
|
4,561.5
|
232,216,842.00
|
Chanzo: Shirika
la Taifa la Biashara (ZSTC), 2020

Mhe. Zubeir
Ali Maulid akizinduwa rasmi Tamasha la Sita la Biashara lililofanyika Januari 2020
katika Viwanja vya Maisara

Mhe.
Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara - Tanzania Bara, akipokea
maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Biashara kuhusu Kliniki ya Biashara,
Januari 2020.

Muonekano
Mpya wa Kiwanda cha nguo cha Basra Textile Ltd kilichopo Chumbuni baada ya
ukarabati

Mashine za
kiwanda kipya cha Basra Textile zilizowasili Nchini hivi karibuni

Maafisa wakiwa katika kazi za upimaji wa vifaa vya
elektroniki ndani ya Maabara za ZBS - Amani

Mfanyakazi
wa Kiwanda cha Ushoni (ZQTL) kilichopo Amani akiwa katika ukataji wa Barakoa

Bidhaa za Chumvi inayozalishwa kutoka Pemba na kusarifiwa na
Kampuni ya Swahili Coast Salt Ltd

Miongoni
mwa muonekano wa bidhaa za Chumvi katika ujazo na ladha tofauti
No comments:
Post a Comment